Je, Dkt. Magufuli angelikuwepo, angelikuwa anakandiwa uozo wote unaosemwa?

Paulsylvester

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2021
Posts
1,464
Reaction score
3,379
Najiuliza tuu,

JPM endapo Angelikuwepo kama raisi ama muda wake wa utawala kuisha,

Aliyekuwa makamo wake ambaye ndiye Rais wetu kwa sasa Angelisema hayo kama aliyosema Washington huko kwa wazungu, ama kwa vile mwenzetu katangulia ndio tunasema na kwa bahati mbaya hawezi hata kusema kwamba kwa hilo mnanisingizia

Nimegundua kitu, Raisi yeyote asikubali kufa Kabla ya kumaliza ngwe yake aisee

Akifa katikati ya safari yanazaliwa mengi mpaka mtu unajuta kwa mini uliwahi mapema huko ulikokwenda
 
Kwani kaenda wapi?
 
Nchi hii unakuwa na nguvu ukiwa madarakani, wangemsema japo si kwa kiwango kikubwa

Kumbuka hata yeye alivyokuwa anasema "kuna wastaafu wanawashwa washwa"
 
..."asikubali kufa kabla hajamaliza ngwe yake"...Kwani huwa mtu anaamua tu kufa?😂😂😂😂
 
President Magufuli alikua ni dictator, why hatuongei ukweli?alikua ni one man show, na tukumbuke watanzania wengi wameuliwa,kupotea, kuwa vilema kwenye utawala wake, hivi tunajiuliza family ya Mawazo (rip)wamepata proper closure?je kulikua na uhalali wa yeye kuuliwa?,nimeagiza coal zaidi zipelekwe tena kwa ndege sio lori .
 
Uyo mother kukosa cha kusema .hatoshi na mipasho yake
 
Watanzania wapi hao? Unaweza kutuwekea ushahidi?
 
Hivi kuambiwa ukweli kuhusu mambo uliyotenda ninm kukandiwa?
 
Watanzania wapi hao? Unaweza kutuwekea ushahidi?
Unataka ushahidi upi sasa, maana kifo cha mawazo aliuwawa kisiasa, Yuko wapi Ben Saanane, au Issue ya Lissu je? Ebu weka mapenzi pembeni alafu vaa UTU kaka na ww usiwe kama mzee wako maana yule mzee hakuwa na UTU kabsa...
 
Unataka ushahidi upi sasa, maana kifo cha mawazo aliuwawa kisiasa, Yuko wapi Ben Saanane, au Issue ya Lissu je? Ebu weka mapenzi pembeni alafu vaa UTU kaka na ww usiwe kama mzee wako maana yule mzee hakuwa na UTU kabsa...
Ushahidi uko wapi?
 
Kama alizuia kusemwa akiwa yupo basi watamsema akiwa hayupo.

Ndio kanuni hiyo.
 
Walikuwa hawajipendi eti mpaka wamseme vibaya
Wangeku fyu fyu
Sijui yule dogo na kibri kile yuko wapi

Yaani cheo katumia kupandikiza chuki na atasemwa sana
 
Hii lugha ya: "angekuwepo wangemsema....."mnapenda sana kuisema sema. Magufuli alipokuwepo watu walimsema, lakini utaona walichofanya(rejea Lissu na wengine). Baada ya kuona kumbe ukimsema kwa kumkosoa unafanywa hivi, watu wakanyamaza, Sasa ameondoka wanasema kitu ambacho walikuwa hawafurahi nacho. Kwa mfano, Magufuli alivyowaambia Wakurugenzi mpinzani akishinda eneo lako wakati nakulipa vizuri, sijui utanieleza nini? Matokeo yake wapinzani wanaporudisha fomu, Wakurugenzi wanakimbia ofisi. Je, kwa uchaguzi wa aina hii, unategemea Taifa lipate viongozi wa aina gani? Watu Sasa wanasema akiwa hayupo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…