Je, Dkt. Mpango ana Afya njema kushika wadhifa wa Makamu wa Rais?

Je, Dkt. Mpango ana Afya njema kushika wadhifa wa Makamu wa Rais?

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Linapokuja suala la Afya ya viongozi hilo ni suala mujarabu kabisa kwa umma kuhoji.

Leo akiongea bungeni, Dkt. Mpango ameonyesha kwamba hata yeye alikuwa hana taarifa zozote za kuteuliwa kwake kuwa Makamu wa Rais, hii maana yake ni kwamba hili suala limefanyika kwa usiri mkubwa bila hata yeye kujua.

Tunajua ni majuzi tu Dkt. Mpango alikuwa hoi bin taaban kwa maradhi yanayohusishwa na ugonjwa wa Korona, Tulimuona akikohoa kwa nguvu huku akioneana mchovu sana.

Swali ambalo mimi kama raia ningependa kuuliza, Je Dkt. Mpango yuko physically fit kushika majukumu mazito ya kumsaidia Rais katika nafasi hii aliyopewa?

Tuliona mathalani, Hayati Magufuli alikuwa ni mgonjwa wa muda mrefu wa Ugonjwa wa Moyo, na kama mnavyojua kazi ya Urais ni kazi nzito yenye stress nyingi na bila shaka siyo rafiki kwa watu wenye ugonjwa wa moyo, Je Vetting process ililifikiria hilo suala kabla ya kumpa Magufuli green light ya kugombea urais?

Je, na mfumo wa vetting nchini umelifikiria suala la Dkt. Mpango kuwa makamu wa Rais, Je wamejiridhisha kuwa yuko fit kwelikweli baada ya kuugua Covid-19?

Kitu kingine ninachomshangaa Dkt. Mpango ni kuwa havai barakoa kwenye mikusanyiko, Je akipata Covid tena katika mazingira ya sasa, ukilinganisha na athari ambazo Covid ya kwanza iliupa mwili wake je atakuwa katika hali gani?

Ni wakati muafaka sasa afya za viongozi wetu ziwe ni factor mojawapo kwenye vetting, la sivyo hii ni disaster kwa nchi
 
Mambo mengine tusubirie majibu yapo mbeleni.

hata hivyo wagonjwa si wanatibiwa?
 
Kusikia Kwa Kenge Mpaka Atoke Damu Puani Na Masikioni.
😁😀😂😃😄😄😅😆😆😅😃😂😊
Habari Za JPM Zilianza Hivi Hivi

Wengine Siyo Waandishi Wa Habari Utawasikia Vigogo Wafa
 
Hatujasema kuhusu kifo, tunazungumzia afya njema ya kumudu mikikimikiki ya kazi. Unaweza usife lakini ukawa dhoofu bin hali
Mtu akiugua covid huwa anajenga usugu wa mwili dhidi ya huo ugonjwa(immunity). Philipo Mpango huko fit sasa hivi .waziri mkuu uingereza alikaa ICU kwenye ventilator kwa wiki nzima leo anadunda. Mpango ametumia oxygen tu hakufika hatua ya ventilator . Yukou vizuri muda huh.
 
1. Kuumwa ni kawaida, kwani hata hao viongozi ni binaadam. Usijisahaulishe.
2. Hilo swali halipo mahala husika, anayefahamu hali yake ya kiafya ni yeye binafsi pamoja na daktari wake-kama anaye.
3. Anayepanga maisha ya mtu ni muumbaji wake pekee (Mungu) unaweza kuanza kutilia mashaka afya ya mtu ukajikuta wewe ndio unatangulia kuaga dunia. Acha kubashiri maisha ya watu.
 
Kwa sababu amekubali uteuzi maana yake yuko fiti.

Wamarekani wamemchagua Biden vile alivyo bwashee!
 
Ulikuwa unapendekeza yupi boss? Mwenye afya njema na nguvu ya kufanya kazi.
 
Kwani kuna uhakika gani ukichagua mtu mzima leo kuwa kesho na keshokutwa hataugua (na hata kufa)? Wewe hapo (japo uko mzima kabisa kwa sasa) una uhakika gani kuwa kesho na kesho kutwa hutaugua (na hata kufa)?
 
Linapokuja suala la Afya ya viongozi hilo ni suala mujarabu kabisa kwa umma kuhoji...
Raisi akipatwa tatizo atakayerithi kiti makamu na makamu akipatwa ni waziri mkuu chama ni sisi wenye mamlaka leo tunamipango mathubuti mama yetu mpendwa samia tunakuombea sana😎😎
 
Duh, hii sinema acha tu mpango hata hapo alipo leo hayuko fit sijui huko mbele 🤔
 
Mtu akiugua covid huwa anajenga usugu wa mwili dhidi ya huo ugonjwa(immunity). Philipo Mpango huko fit sasa hivi .waziri mkuu uingereza alikaa ICU kwenye ventilator kwa wiki nzima leo anadunda. Mpango ametumia oxygen tu hakufika hatua ya ventilator . Yukou vizuri muda huh.
Mhu.... Alitumia okisijeni tu hakufikia hatua ya kutumia ventilator.....hebu tufafanilie sisi maleiman wa mambo ya tutabibu.
 
Kwani kuna uhakika gani ukichagua mtu mzima leo kuwa kesho na keshokutwa hataugua (na hata kufa)? Wewe hapo (japo uko mzima kabisa kwa sasa) una uhakika gani kuwa kesho na kesho kutwa hutaugua (na hata kufa)?
Kwa hiyo leo unaamini kwamba Mwendazake alikosea kujiita Jiwe hata kama ulimuunga mkono?
 
Watu wengi wanabeza maono ya mtoa mada Ila IPO siku tutakuja kusadiki haya mawazo yake....
wasiwasi ndiyo akili
 
Back
Top Bottom