Je, Dkt. Mpango ndiye Rais ajaye?

Je, Dkt. Mpango ndiye Rais ajaye?

Katika mazungumzo yangu na watu nyeti nimedokezwa Jambo la kushangaza. Wanadai kuwa ishaamuliwa baada ya Mama yetu mpendwa, ajaye ni Makamu Rais Dr Philip Mpango.

Niliwaambia mbona Kuna vijana wawili na hata wanne machachari wanatajwa kuwinda nafasi hii? Wakadai kuwinda na kulenga shabaha ni jambo jingine. Nikawauliza tena hadi kipindi tarajiwa Makamu atakuwa Mzee Sana!! Wakanijibu wewe wasema!!

Niliondoka nimeinamisha kichwa chini kwa sababu akiwa Waziri wa Fedha inadaiwa ndiye aliyemshauri Rais Magufuli kuwa kuwapandishia wafanyakazi mishahara kila mwaka sio Jambo la lazima bali ni hiari, "Tuhangaikie miradi Kwanza".
Dr. Mpango fitina za siasa haziwezi labda itokee apate bahati kama aliyopata Dr. Magufuli wakati ule wa kuchakata jina la mgombea wa CCM kwenye vikao vya chama hicho
 
Back
Top Bottom