Je, DPP atalazimika kuiondoa Kesi ya akina Halima Mdee kama alivyofanya kwenye Kesi ya ugaidi ya Mbowe?

Je, DPP atalazimika kuiondoa Kesi ya akina Halima Mdee kama alivyofanya kwenye Kesi ya ugaidi ya Mbowe?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Kwa namna ya hili sakata la Hawa wanaojiita wabunge wa viti maalum, kupitia chama kilichowavua uanachama wao cha Chadema na namna Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson, anavyojaribu kuendelea kuwakumbatia hao akina Halima Mdee, naziona dalili zote za kutokea kile kilichotokea kwenye ile Kesi ya kubambika ya ugaidi ya Mbowe na wenzake.

Nasema hivyo kwa kuwa Katika "proceedings" za Mahakama, kila kitu kitakuwa wazi.

Kwahiyo wale waliofoji barua na kupeleka NEC watajulikana.

Hata yule aliyemtoa mfungwa Nusrat Hanje usiku na kesho yake asubuhi akaenda kuapa na kuwa Mheshimiwa Mbunge,naye atajulikana wazi!

Huyo Spika Tulia Ackson, anayefanya sarakasi zote hizi za kuendelea kuwakumbatia wabunge ambao Hawana chama, lazima atambue jinsi anavyojitumbukiza kwenye shimo la kujiangamiza.

Tutarajie tena kushuhudia mashahidi wa akina Halima Mdee, toka NEC na Ofisi ya Bunge, wakiomba udhuru wa mara kwa mara kwenda "maliwatoni" kwenda jisaidia.

Je, DPP kwa mara nyingine tena, atalazimika kuiondoa mahakamani, Kesi hiyo kama ilivyomkuta aibu, baada ya kuiondoa Kesi ya kubambika ya ugaidi ya Mbowe na wenzake?

Yetu macho, tutege masikio yetu kwenye Mahakama Kuu, kushuhudia jinsi jopo la mawakili waliobobea la akina Kibatala, jinsi "linavyowagaragaza" mawakili wa akina Halima Mdee!😄
 
Samia Suluhu anataka ithibitike kuwa yale makesi yoote yeye hahusiki nayo. Ndio maana anayaacha yaendelee ili walioyatunga wawe wanaumbuka wenyewe...
Uko sahihi kwa asilimia 100
 
Kwa namna ya hili sakata la Hawa wanaojiita wabunge wa viti maalum, kupitia chama kilichowavua uanachama wao cha Chadema na namna Spika wa Bunge...

Kwani hii kesi imefunguliwa na Jamhuri mpaka DPP ahusike ktk kuiondoa..!??

Naishauri mamlaka hiki kinywaji cha Double Punch kichunguzwe vizuri aisee 😀
 
Kwani hii kesi imefunguliwa na Jamhuri mpaka DPP ahusike ktk kuiondoa..!??

Naishauri mamlaka hiki kinywaji cha Double Punch kichunguzwe vizuri aisee 😀
Kama haijafunguliwa na Jamhuri, ni kitu gani kinachofanya ionekane "imebebwa" na Bunge letu pamoja na vyombo vyake?

Kwa kuwa siyo siri tena, hata mtoto anayesoma chekechea analijua hilo
 
Kama haijafunguliwa na Jamhuri, ni kitu gani kinachofanya ionekane "imebebwa" na Bunge letu pamoja na vyombo vyake?

Kwa kuwa siyo siri tena, hata mtoto anayesoma chekechea analijua hilo
Hilo nalo neno
 
Kama haijafunguliwa na Jamhuri, ni kitu gani kinachofanya ionekane "imebebwa" na Bunge letu pamoja na vyombo vyake?

Kwa kuwa siyo siri tena, hata mtoto anayesoma chekechea analijua hilo

Hacha mihemko mkuu,kama sio siri Tena twambie nani aliwasainia hao akina Mdee na wenzake,mana kama wasingekuwa chadema walio saini hii ngoma ingekuwa ishaisha.

CHADEMA mnajifanya mna umoja kumbe umoja anao aliyesaini majina ya akina mdee na kuweka muhuri ili wakaapishwe kuwa wabunge viti maalum!
 
Hacha mihemko mkuu,kama sio siri Tena twambie nani aliwasainia hao akina Mdee na wenzake,mana kama wasingekuwa chadema walio saini hii ngoma ingekuwa ishaisha...
Kwani hujawasikia viongozi wa Chadema, wakidai kuwa kuna "forgery" kubwa imefanyika, Katika sakata hili la akina Halima Mdee?
 
Samia Suluhu anataka ithibitike kuwa yale makesi yoote yeye hahusiki nayo. Ndio maana anayaacha yaendelee ili walioyatunga wawe wanaumbuka wenyewe.

Tuliona kesi ya Akina Mbowe mambo yalivyokuwa
Hivi alikuwa BBC SWAHILI na Kikeke akaulizwa akasema ushahidi wanao alikuwa nan? Mbona mnatetea ujinga mpk aliousema kwa kinywa chake mwenyewe?
 
Back
Top Bottom