Je, Dunia ni battle field ya UJASUSI kati ya ufalme wa Nuru vs ufalme wa Giza?

Ulichoandika ni uongo
Kabla ya shetani kuasi kulikua na maisha mfano ni uwepo wa mifupa ya dinasaurs na viumbe wengine

Baada ya shetani kuasi vita vilipiganwa kwenye universe yote dhidi ya malaika mikaeli- ila malaika mikael alizidiwa Mungu akampa damu yake ambayo zaman hizo ilikua inaitwa damu ya mwana-kondoo ambayo baadae ikaitwa damu ya Yesu

Ndo maana ukiangalia sayari ya mars, venus, mercury na nyinginezo kulikua na maisha ila yaliharibiwa yote baada ya vita hata uwepo wa black holes ambazo ni nyota zilizokufa ziliharibiwa wakati wa vita kati ya malaika mikael na shetani

Baada ya vita unaona Mungu akirudisha nuru ya jua ndo maana akasema na iwe nuru baada ya hapo akatengeneza dunia kwa kutengeneza dunia kupitia kuweka ozone layer mpaka siku ya sita akawa amemaliza dunia kumbuka sayari nyingine zilikua bado hazijatengenezwa baada ya kuharibiwa na lengo ni mwanadamu aje aendeleze kazi aliyoianza

Kwa hiyo unavyoona mwanadamu anakua na kiu ya space exploration ni lengo la Mungu kabla mwanadamu hajaasi kuendeleza sayari nyingine kumbuka lengo la Mungu hakukua na mauti watu walikua wanazaliwa tu hawafi kabla ya kuasi kwa hiyo sayari zilikua zijae makazi ya wanadamu lakin akakorofisha kupitia adam
 
Ni rahisi sana kutengeneza DHANA ambazo hazipo kuliko kubainisha FACT

Wanaotawala dunia kila siku wako busy kufanya tafiti za kisayansi kutafuta namna ya kuzidi kuboresha maisha yetu wakati wengine wanaamini mafanikio yako kwenye code from ancient scriptures zilizoandikwa na ignorant people ili ku fit era yao
 
Hata wewe ni muongo tu

Sayari pekee inayo sapoti life kwa viumbe vilivyopo duniani ni dunia peke yake
 
A very deep and profound explanation.

However, i wish to challenge it on grounds of some factual contradictions which stand in your line of argument.

Today at night. See you.
 
Acha uvivu wa kusoma soma tena uzi kwa umakini
Unasoma tu juu juu alafu unacomment

Bibilia haijui chochote kuhusu Solar system wala kuhusu milky way wala kuhusu black hole

Milky way, Bkack hole na sayari zilizokufa bado ni theories za kisayansi tu na hazijawa scientific proof

Mnapotumia ancient books zenu kuanza kutafuta namna ya kutafuta aya ku fit kwenye vumbuzi mpya za kisayansi hapo mnakua mnatudanganya

Ni bora mbaki kwenye mambo yenu ya “kiroho”
 
Bibliq imeelezea vizuri dunia na universe kuliko kitabu chochote kile hapa duniani
Kama huiamini pole
 
Hii elimu umeitoa wapi?

Please tell me that its from the holy spirit and i will instantly believe you...pleeeease
Bibliq imeelezea vizuri dunia na universe kuliko kitabu chochote kile hapa duniani
Kama huiamini pole
Mkuu, nnaomba code..
 
Habari Mkuu! Man Jau..
Kuhusu maandiko Kuwa Ni mfano wa Yesu si mimi niliesema Ni biblia..

Waebrania 5:5-6

"Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia,
Ndiwe mwanangu,
Mimi leo nimekuzaa.
kama asemavyo mahali pengine,
Ndiwe kuhani milele
Kwa mfano wa Melkizedeki."



Waebrania 6:20

"alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele
kwa mfano wa Melkizedeki."


Waebrania 7:11

"Basi, kama ukamilifu ulikuwapo kwa ukuhani wa Lawi; (maana watu wale waliipata sheria kwa huo);
kulikuwa na haja gani tena ya kuhani mwingine ainuke, kwa mfano wa Melkizedeki, wala asihesabiwe kwa mfano wa Haruni?"


Waebrania 7:15

Tena hayo tusemayo ni dhahiri sana zaidi, ikiwa
ametokea kuhani mwingine mithili ya Melkizedeki;


ninaweza Kumention alot of Verse lakin hazitasaidia kama hutaelewa

Naweka Angalizo swala la Melchizedek liliwashinda walimu na Mafarisayo na hasa Wanafunzi wa Paulo na wanafunzi wengi hawakuelielewa Sio swala Dogo kama tunavyofikiria na Kusema tu ni fulani..

mwandishi wa Waebrania anasema kuhsu swala la Melchizedek akiwaambia Wenye Elimu na wanafunzi wake pia...


Waebrania 5:10-14

"kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.

Ambaye tuna maneno mengi ya kunena katika habari zake; na ni shida kuyaeleza kwa kuwa mmekuwa wavivu wa kusikia.

Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.

Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga.

Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya"
 
Mimi nami niweze ku share kidogo ktk mapito yangu na Maisha ya imani . Miaka 5 hivi iliyopita nilipokutana na nguvu isiyo ya kawaida ni kapata Neema ya kuona( Macho ya kiroho) na kujua ya kuwa kuna Ulimwengu usionekana na Falme mbili zinazotikisa na kuongoza Ulimwengu huu. Mimi nilipata uwezo wa kuona in short dunia ina mafumbo mengi ila kama wew ni mwanadamu na hujui kuhusu Ulimwengu wa Roho , kiwango chako cha Siri na mambo mengi ktk Dunia hii uko chini sana. Nitazungumzia Tukio la kimuujiza ktk siku mbili , siku ya kwanza nilijaribu kulala, nilikuwa nimechoka sana kutoka Kwenye kazi ya usiku ,(night shift)so nilipiga magoti nikasali kwa dk kama 5 tu then nikilala, kiasili mimi ni mtu wa vita sana ktk Ulimwengu wa Roho nimezoea hali hio. So mwili ukaanza kuwa na mtetemo kuna hali ya kujazwa Roho mtakatifu so nikaona sasa Roho yangu inaenda juu kutoka mbingu ya kwanza, ikaja mbingu ya pili mpaka mbingu ya tatu. Mimi sasa akilini inaniambia kuwa dunia hii ndo basi tena, Sasa nikawa nasikia sauti watu wana imba kama kwa chini hali ya mbingu hio ni uzuri wa ajabu sana, ghafla Roho ikaanza kushuka chini , Sasa kuna maneno nikawa nayatamka ya ukiri wa ukuu na utukufu wa huyo Mungu aliyeumba vitu vyote , so Roho ikashuka chini mpaka nikaona watu wanaenda kanisani ni baba na binti.Hapo sasa nikashituk kutok katik Ulimwengu wa Roho na kuwa katika hali ya kawaida hio ni Jumanne Asubuhi so nikapumzika nikaenda ktk kazi yangu kama kawaida Jumanne ya siku hio nikalala tu, sikutaka kufanya maombi niliwaza hawa wachawi na mapepo sio size yangu so nikalala tu , Asubuhi yake Jumatano kama Muda ya saa tatu kikaja kiumbe kina umbo la buibui ( Spider) kwa macho ya kiroho kikaanza Kutema Moshi chumba kizima nikapata hali ya kupaliwa na kukohoa. Hii ni moja ya attempt ya Roho ya mauti nilifanyiwa ktk Maisha yangu ya kiroho 🙏🏾🥲 . Sasa nikawa nimezidiwa sana , halafu ni kama imani ilitikiswa sana . Hapa kuna code mbili mnajua maana ya Spiders 🕷️ na imani ( faith)
Hizo ni code spider ni symbol kubwa ya adui na wafuasi wake hupenda kuitumia. Imani ni weapon ktk Maisha ya ukristo , ukiwa na imani you can do any thing at any time.
Rejea Math 17:20 , pia rejea ktk umbaji jinsi kwa imani Mungu alivyokua akiumba vitu Mwanz 1:3-5 hapa sasa kuna suala la imani pamoja na kutamka hii kitu wanadamu wengi Hawajui. Sasa ktk hali hio nikaona nguvu na sauti isiyo ya kawaida ikizungumza ndani yangu , Ilisema kwa Mamlaka niliyopewa na Baba , Mwana na Roho mtakatifu nakuamuru (command) uache .Hapa ulitajwa utatu mtakatifu ktk hali ya ajabu sana kwa kweli .Wakati huo mkono wangu wa kulia( kiume) uliunuliwa kwenda juu , kuelekea kwa kile kiumbe ghafla kikata kona kwa maana ya kugeuka na kuanza kurudi nyuma, sauti ikasema……… .. Mwanangu hapa lilitajwa jina langu na Mwanangu . Sasa hapa nikaambiwa na pole . Hapo machozi yalikuwa yanatoka sasa nikawa najiuliza kwanini kile kiumbe kije kunishambulia na kwanini hii mamlaka ya juu iliruhusu na inalijua jina langu kiukweli nina majibu ya maswali yote , sema ni kwa kuwa hali ya Tukio lilivyokuwa. Kwa upande wa hio mamlaka iliyoniokoa Sikuona kitu chochote zaidi ya hio sauti kuwa ndani yangu ,yaani maelekezo yanatoka ndani kwa ndani Sasa hapo ndo ujiulize pia soma..
“Je, hamjui kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, ambaye mlimpokea kutoka kwa Mungu? Nyinyi basi, si mali yenu wenyewe.”
‭‭1 Wakorintho‬ ‭6‬:‭19‬ ‭BHN‬‬
Hapo kiukweli nilishangaa sana pia code ya pili ni jina , jina la kiroho ndio msingi wa Maisha na utambulisho wako tuwe makini na majina yetu na ya watoto wetu.
Hivyo sio tu uwanja wa ujasusi ila kuna vita kali na kuna mambo mengi sana .
Mwisho kama mtu anataka ushahidi wa code au Alama ya buibui Nitaweza weka huku kwa ufananuzi fulani wa picha , watu watashangaa sana wale wasio amini.
Mwaka huu Mungu akinipa kibali nitaandika kitabu kuweza ku share Siri na mafumbo ktk Ulimwengu huu na na namna Ulimwengu wa kiroho ( usionekana unavyo fanya kazi). Kitabu kitakuwa bure kabisa Nikifanikiwa kuandika .
Yako mambo mengi sana. Mungu tusaidie wanao 🙏🏾
 
Ahsante Kwa mchango wako 🙏

Share nasi zaidi ukiridhia kufanya hivyo.
 
Ujasusi unaendelea,

Kumbe aketiye katika KITI Cha enzi Mbinguni, mikono yake Ina matundu ya misumari. Na ni mfano wa mtu kabisa!!

Sasa waliomchoma mkuki na kumsulubisha nini kitawakuta🤔
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…