Huyo Aziz akiumwa au akiwa majeruhi nani anacheza?, FEISAL na Mabosi wake inaonekana Walikuwa wanabishana juu ya issue ya mshahara wa FEISAL. Na inaonekana walimtishia kuleta hizo fedha ili mkataba wake uvunjwe, Sasa alipoleta ndio wakaenda kwenye kipengele cha Sheria za mikataba.
Kwasababu, mtu mwenye akili timamu hawezi kuamuka tu, na kupeleka milioni 112, benki bila kuwa na kutoafikiana katika suala la maslahi.
NB
Umesaini mkataba mwaka juzi na gharama za maisha zinapanda kila uchao, kwanini maboresho yasifanyike ili mchezaji awe na Ari na morali ya timu yake?( Kumbuka, malipo duni ndio yanamfanya FEISAL kutaka kuhama YANGA. Dawa yake ni kuboresha maslahi yake, siyo kumwambia akumbuke masharti ya mkataba).
KIFUPI: FEISAL naye anapenda kutanua kama wengine. Kwahiyo, tuache kumtwisha misalaba isiyomhusu.