Uchaguzi 2020 Je, Halima Mdee amefanya nini Kawe kwa miaka 10 ya ubunge wake kustahili kuendelea? Sikia ya Askofu Gwajima, 28 Oktoba fanya uamuzi sahihi

Kina Ngosha hamuwezi kujizuia ukabila, itawagharimu....hiki mnachokitafuta mtakapokipata mtakikimbia wenyewe.
Wala sio Ngosha wote Bali ni wale walioahidiwa Madaraka na wale wanaopata Tenda na ajira za kupeana kwenye miradi yote.
Hawazidi hata familia 20 . Hawa wachache sana ndio wanaojimilikisha nchi .
Wengine wote ni wasindikizaji tu kama wengine. Kinachofanyika hao wachache kwa sababu wananufaika wanaeneza Propaganda na porojo Kila kukicha huku wakiwaumiza wananchi kwa kuwaita Wanyonge ili hali wao hawajui hata kitu kinachoitwa umaskini. Wanaogelea kwenye mihela halafu wanawadanganya Watanzania kuwa wao nao ni maskini.
 
Hivi huwa mnatumia vigezo gani kumchagua mbunge wa jimbo lako? maana hapo ndio utajua mgombea fulani anafaa yupi hafai,mgombea fulani umchague tena au usimchague tena.
 
Kwanini unamuuliza Halima badala yakuiuliza ccm iliyoko madarakani tangu uhuru imefanya nini ikiwa mpaka Sasa watoto bado wanasoma wakiwa wamekaa kwenye matofali ikiwa tuna misitu yakutosha Kama si wehu ninin
 
Naona wewe unajibu swali ambalo halijaulizwa; ingekuwa mtihani ungepata sifuri
Mtoa mada ameuliza atajiwe mambo aliyo yafanya Halima Mdee kwa miaka 10; wewe unaleta swali tofauti kabisa na kulitoa jibu? Jifunzeni basi kujibu maswali
Sijifunzi na pia nimetoa sababu za kumkataa huyo mnaempigia kampeni, nikiwa kama muislam na mkazi wa makongo siwezi kumkubali mtu anaetaka uislam upotee hapa tz
 
Hata wewe ulikuwa na day dreams kuwa ccm itakupitisha kuwa mgombea ubunge kawe, acha kila mtu aishi ndoto zake
 
Duh...!, laiti ungelinijua mimi ni mtu wa type gani!, mimi sio mtu wa ile type ya kukimbia uzi, nasimama nao, swali bado ni very valid, Halima Mdee kafanya nini Kawe kwa miaka 10!.
P
Paskal ulipaswa kutueleza kazi za mbunge kwanza kabla kumpigia debe mtu wako, ila sishangai huyo unaempigia debe una sababu zako kwanza chama kimewataka wote mlioangushwa kuwapigia debe waliopita pili gwajima ni mkristo mwenzio pengine nawewe ungependa misikiti iwe Sunday schools
 
Ukweli upo wazi gwaji hana mpinzani , bi kidude hajafanya chochote cha maana jimboni kawe.

Nilifikiri Ma kada wa CCM mnatumia akili zenu ?? Hivi nani anayekusanya kodi katika jimbo lolote lile Tz?? Mbunge eti mnataka achimbe visima

katikati ya mji , ndiyo mnaita maendeleo hayo ???

Haya kasubiri sahani ya pilau na soda pamoja na paketi ya sigara kali , labda nayo ukipewa utaita maendeleo kaleta Askofu wako Gwajima
 
Paskali sijui wewe unaishi Kawe ipi, ila sisi wakazi wa Kawe tunamuelewa sana Halima Mdee. Hana majigambo ila kazi anapiga kwelikweli huyu Dada. Labda kwa uchache tu nikujulishe haya

1) Kule Mbezi Juu mtaa wa ndumbwi ilikuwa mvua ikinyesha mawasiliano yanakatika kutokana na Mto Ndubwi kujaa, leo kuna madaraja mawili hii kila mkazi wa ndumbwi Anajua ni kazi ya Mdee.

2) Waulize wakazi wa msasani maeneo ya Chama, ilikuwa kila mvua inaponyesha ni mateso kwao, Mdee alipambana usiku na mchana kuhakikisha inajengwa mifereji ya maana ya kupeleka maji Baharini. Wananchi wa maeneo hayo huwezi kuwaambia chochote kinyume Halima.

3) wakazi wa maeneo yaliyokuwa na migogoro ya Aridhi kule chasimba nk, Halima alipambana nao mchana na usiku kuhakikisha wanapata haki zao. Huko Mdee huwa hapigi kampeni huwa anauhakika wa kura zote.

4) Leo shule ya Msingi Mbezi Juu imeshakuwa na sekondari, Mdee alishiriki katika kuanzishwa kwake na kujenga vyumba vya madarasa.

5) Barabara za Kawe nyingi zinapitika na daima amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha Kawe inamiundombinu ya barabara.


Tembelea Kawe, ongeo na wakazi wa kawe, zungumza na mtu mmojammoja, utapata majibu ya kwanini Kawe Halima anashida bila shida. Aliikuta Kawe katika hali mbaya sana kutoka kwa Ritha Mlaki, amejitahidi kwa muda mfupi kuifikisha hapo ubapoiona..
 
Mkuu kifaulongo , kwanza asante kwa mchango wako , umechangia very objectively, kwasababu tangu bandiko hili lianze, hadi linafika posts 344, wewe ndie mtu pekee uliejitokeza na kujibu at last Halima did something Kawe. Thanks for this.

Pamoja na yote hayo, kufuatia kauli thabiti kutoka Juu, za Serikali inapeleka wapi maendeleo, nikitolea mfano mmoja tuu wa barabara za lami za mitaani, nikifanya a comperative analysis ya barabara za mitaa ya Ilala, na Kinondoni, compared to Kawe, utakubaliana na mimi, kuwa Halima Mdee, pamoja na Juhudi zake zote, na kumpenda tunampenda mimi nikiwemo, nampenda Halima na mwenyewe anajua nampenda, lakini Sisi wana Kawe kindakindaki, katika umoja wetu, tumeamua kwa dhati kabisa kuwa i hii miaka 10 ya Halima Mdee Kawe sasa imetosha, tuna lirudisha jimbo la Kawe, nyumbani kumenoga!.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…