Je, halimashauri wangekodi mabasi jua lisingezama? Ni lazima kila mmoja awe na gari Arusha?

SOVIET UNION

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2017
Posts
509
Reaction score
1,391
Kuna gari 400 plus za halmashauri zote Tanzania. Kuna halmashauri unakuta ina gari 3: Mkurugenzi gari lake na watumishi wengine gari zao. Kwa ujumla, Arusha kuna gari 500 na zaidi za halmashauri Tanzania nzima.

Sasa chukulia kwa mfano halmashauri za Mkoa wa Lindi wakaamua kuungana na Mtwara wakachukua Yutong moja safi kabisa wakaja nayo Arusha. Je, jua halitazama? Arusha wakifika wanaweza kodi tax za kuwapeleka mkutanoni na kuwarudisha hotelini, lakini kwa taifa ambalo kuanzia Mkuu hadi Chini ni watu wa matumizi, hili haliwezekani.

Mzigo unaishia kwa kuongeza tozo kwa raia ili kuhudumia halmashauri kwa sababu ya matumizi ya anasa. Ukiwakuta juu ya majukwaa wanalia lilio cha mamba kwa shida za wananchi.

Arusha kwa leo, ukikata kona unakutana na gari za halmashauri mara Kibondo, mara Kishapu, mara Manyoni. Hapo bado, ma V8 ya wakurugenzi ambayo hayana maandishi yoyote.

Na hapo anaye fungua mkutano utasikia anawaambia waongeze juhudi kwenye kuhudumia raia. Huku nje ya ukumbi, kukiwa na magari 400 plus, na hapo hapo vijijini kumejaa project zinazoendeshwa kwa michango ya wananchi wanaochangishwa kwa nguvu na wala sio kwa hiari yao.

Hawa ndio watawala tunangoja watufikishe uchumi sawa na Vietnam au Thailand au Malaysia.

Ukiwakuta viongozi wakuu kama Rais, Waziri Mkuu na Makamu wa Rais wanavyolia, utajua wako serious na kuinua hali za maisha ya wananchi, kumbe ni hadaa tupu. Hakuna kiongozi ndani ya CCM yuko interested kuondoa umaskini.
 
CCM ni "nyonya damu" wa kimya kimya.
Hawana mpango na maendeleo ya Mtanzania.
Hawana mpango na kumsaidia Mtanzania.
Hawana mpango wa kutatua kero yoyote ya Mtanzania.
Mpango wao ni kuendelea kuwafanya Watanzania "misukule" ili waendelee kuneemeka wao na watoto wao, wajukuu wao,ndugu zao na watu wao wa karibu ambao kiujumla ni kakikundi kadogo sana.
 
Machafuko pekee yake ndio yataweza kuleta mabadiliko ya kweli ya kiutawala hapa nchini.
Mhh machafuko sio jambo jema sana labda kama huna miradi wa la hujawekeza sehemu. Kiufupi huna cha kupoteza ndio utatamani machafuko kwakua huna sehemu umeweka hela yako
 
Mhh machafuko sio jambo jema sana labda kama huna miradi wa la hujawekeza sehemu. Kiufupi huna cha kupoteza ndio utatamani machafuko kwakua huna sehemu umeweka hela yako
Mkuu umewekeza kiasi gani nchi hii? Kwa taarifa yako hicho ulichowekeza kitakuwa bora zaidi baada ya wimbi hilo. Labda useme wewe ni mfaidika wa mfumo huu, hivyo unaogopa yakitokea mabadiliko ya kweli utaathirika.
 
Mkuu umewekeza kiasi gani nchi hii? Kwa taarifa yako hicho ulichowekeza kitakuwa bora zaidi baada ya wimbi hilo. Labda useme ww ni mfaidika wa mfumo huu, hivyo unaogopa yakitokea mabadiliko ya kweli utaathirika.
Nimeweleza kidogo sana kwaajili ya maisha ya familia yangu. Kuhusu kufaidi mfumo nafaidi sana na kwa mambo ninayofanya hata ukija mfumo mpya bado nitafaidi kwakua ni mpambanaji
 
Nimeweleza kidogo sana kwaajili ya maisha ya familia yangu. Kuhusu kufaidi mfumo nafaidi sana na kwa mambo ninayofanya hata ukija mfumo mpya bado nitafaidi kwakua ni mpambanaji
Basi kaa kwa kutulia, nilijua umewekeza kwenye uchimbaji wa gas, kumbe una salon ya kunyoa ndio unapata woga hivyo wa mabadiliko.
 
Juzi kwenye msiba wa Malikia Elizabeth viongozi wenu walipokodiwa mabasi na wao kujazana kwenye hayo mabasi ziliandikwa nyuzi lukuki humu kuonesha tulivyokasirishwa.

Lingine ikitokea ajali ndiyo fikiria Serikali itavyopata hasara kupoteza maDed wote kwa wakati mmoja
 
Halimashauri ni kilugha gani? 🤣 🤣 Shame.
 
Lazima tutenganishe Halmashauri na serikali kuu. Na Halmashauri idhibitiwe na wananchi moja kwa moja...wananchi ndo waajiri wakurugenzi wa Halmashauri, na wawe na nguvu za kuwafukuza wakati wowote.
Lol si wataishia kuajiri darasa la Sana 😅 au wazee maarufu huko mawilayani,
 
Ma-DED wana ajabu gani hata wakifa wote nchi nzima kwa pamoja?
Kafa Magufuli maisha yameendelea sembuse cheo cha mtu ambaye hatumjui, sijawahi kumjua DED wangu yeyote hivyo assumption yangu ni yeyote yule anaweza kuwa as long as anamtumikia aliyemchagua
 
Lazima tutenganishe Halmashauri na serikali kuu. Na Halmashauri idhibitiwe na wananchi moja kwa moja...wananchi ndo waajiri wakurugenzi wa Halmashauri, na wawe na nguvu za kuwafukuza wakati wowote.
Sio Kwa nchi hii, wabunge tu hatuwafanyi kitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…