Baada ya kuona Klabu ya JKU ya Zanzibar ina Umasikini ( Ukata ) hasa katika Kushiriki Michuano ya Kimataifa Klabu ya Pyramid kutokea nchini Misri imeamua kutumia Umasikini wa JKU ya Zanzibar kwa kuwaomba Wakubali kucheza Mechi zao zote Mbili huko Misri na kwamba wasikubali kuja Kucheza mchezo wao wa Marejeoano Kisiwani Zanzibar.
Klabu ya Pyramid ambayo inatambia Jeuri yake ya Pesa na Utajiri mkubwa iliyonayo haijaishia tu Kuishawishi Klabu ya JKU kufanya watakalo Wao bali wameenda mbele pia na kuamua Kuwatafutia Hoteli ya Kimataifa na ya Kifahari ya Kukaa kwa muda wote watakaokuwa huko nchini Misri, kuwakarimu kwa mambo madogo madogo wakiwa huko na kubwa ni kuwapa 30% ya Mapato ya Mechi zao zote Mbili.
Je, ina maana Serikali ya Zanzibar na pia hata TFF ( Tanzania ) zimekubali hii Dharau na Jeuri ya Klabu ya Pyramids?