Mimi nimeexperience kinyume
Nishawahi kukata tiketi gari la kuelekea Dodoma (nadhani ilikuwa alsaedy au super champion)
Nimekata tiketi saa 2 na walisema litaondoka saa 2 ½, kibaya naingia ndani nakuta abiria kama watano tu nikasema leo nimeyakanyaga
Nimejaribu kwenda Kwa konda akawa anakazia abiria wapo wengi tu wametoka nje na akanionyesha kitab Chao Cha tiketi kweli kilikuwa kinakaribia kujaa
Tukikaa kwenye gari kuanzia saa 2 hadi saa 5, kibaya zaidi gari lilikuwa lipo limewashwa likazimwa na wakalipaki pembeni kabisa kuonesha hakuna ratiba ya kuondoka
Kuna jamaa mmoja, akawafuata makonda akawaka sana na akawaambia wamrudishie nauli yake huku wengine tupo kimya tu tunasapoti kimoyomoyo
Jamaa wakataka kumrudishia Hela yake akagoma akasema yeye atakuwa wa mwisho kupewa, yaani Hela Kila mtu apewe nauli yake ili akapande gari lingine
Jamaa wakapagawa wakaamua kuanza safari.
NILICHOJIFUNZA
1. Hutakiwi kuwasikiliza maagent vishoka maana waliniongopea gari kama kimbinyiko, shabiby nk zimejaa kumbe uongo
2. Sikuwahi kukata tiketi mpaka niingie ndani ya gari nijirishishe kuwa lina abiria wa kutosha
3. Kusafiri na kampuni za uhakika sio magari mabovumabovu /ya zamani