Je, huu ni mwanzo na mwisho wa Kagame?? Marekani kuisaidia kijeshi DRC!

Je, huu ni mwanzo na mwisho wa Kagame?? Marekani kuisaidia kijeshi DRC!

Ndicho walichotaka siku zote. Waliwaza wataingiaje DRC kuyachuma madini haya adimu na adhimu duniani? Kwanza wakamfadhili Rwanda ili kumchomganisha rasmi na jumuiya ya kimataifa. Wakampa effective equipment za kujilinda na mashambulizi ya anga. Kagame akavimba kichwa. Baada ya hapo mataifa wakaanza kumshushia lawama kwa kuivamia DRC wakamwekea vikwazo halafu sasa wameamua kuingia upande wa pili DRC ili rasmi wapewe migodi wachimbe wao wenyewe. Kumbuka walichotaka kwa Ukraine, Zelensiky akajifanya kukataa, lakini baadaye akaomba radhi na muda siyo mrefu atarudi Marekani kuitoa rasmi Ukraine kwa Marekani. Marekani ndiyo tatizo kubwa duniani. No peace with America but neo colonialism.
Umeandika ukweli mtupu, ila Afrika hatujielewi. Mmarekani na nchi za ulaya kwa ujumla hawatoi msaada bila wao kufaidika, na wao ndiyo chanzo cha kukosekana kwa amani duniani. East Afrika tumefikiwa na uchonganishi wa hao jamaa dah! inauma sana.
 
Umeandika ukweli mtupu, ila Afrika hatujielewi. Mmarekani na nchi za ulaya kwa ujumla hawatoi msaada bila wao kufaidika, na wao ndiyo chanzo cha kukosekana kwa amani duniani. East Afrika tumefikiwa na uchonganishi wa hao jamaa dah! inauma sana.
Watu badala ya kujifunza jinsi ya kutumia malighafi zako kujenga nchi kama PK alivyofanya, sisi tupo busy kuombea aharibikiwe...
 
sisi wenyewe tuna nguvu za kukabiliana na taifa lolote kubwa au dogo duniani, tuna utisho mkuu hakuna wa kuweza kutamani rasilimali zetu kwa kutuchonganisha sisi kwa sisi au kenge yeyote jirani yetu. Tuko imara tangu zama za Mwalimu Nyerere hakuwaogopa wakoloni aliwapa makavu na walituogopa. Rasimali zetu tutatoa kwa makubaliano maalum kwa faida ya nchi yetu na sio wezi toka nje waje wajichukulie watakavyo, cha moto watakiona kutoka ardhi yetu ikiwa wataingia kibabe kuvuna madini yetu
Wameyavuna toka mwaka 95 we unaishi wapi ndugu, fuatilia nchi gani inaongoza kuuza Tanzanite ndo utajua kama tulishaliwa mda tena bila nguvu.
 
Back
Top Bottom