Tetesi: Je, huyu ndiye Mwenyekiti mpya wa CHADEMA ajaye?

Tetesi: Je, huyu ndiye Mwenyekiti mpya wa CHADEMA ajaye?

ANT - NYONDENYONDE

Senior Member
Joined
Jul 29, 2024
Posts
154
Reaction score
173
Swali, Je, huenda Freeman Mbowe akajitoa ili kulinda heshima kidogo aliyonayo au yuko tayari kubeba aibu kwa gharama ya chawa wake||

Taarifa za chinichini ni kwamba,

Mtia nia wa nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA ngazi ya Taifa Bwana Tundu Lissu ameshamaliza Uchaguzi tayari kinachosubiriwa kwa sasa ni wanachama ambao ni wajumbe wa mkutano mkuu kupiga kura tu tarehe 21.01. 2025.

Watu wake wa karibu wanasema mtiania wao huyo huenda akashinda Uchaguzi huo kwa zaidi ya asilimia 70 ya kura zote zitakazopigwa kwani wanachama wa CHADEMA hasa wale walioduni sana kimaisha na kielimu ambao ni wengi wanaonesha kumuhitaji zaidi Tundu Lissu kwa sasa kuliko Freeman Mbowe kwa sababu wanazozijua wao wenyewe.

Lissu anayeungwa mkono kwa karibu na makundi yote hasa BAWACHA, BAVICHA , BAZECHA pamoja na idadi kubwa ya wajumbe wa mkutano mkuu Kuna kila dalili atashinda kwa kishindo na KUWEKA rekodi mpya katika siasa za CHADEMA ngazi ya Taifa.

Pitia hapa pia KURA: Je, ni nani kati ya Freeman Mbowe na Tundu Lissu anayefaa zaidi kuiongoza CHADEMA kwa Sasa?

Hata hivyo,Tundu Lissu anaonekana kupata nguvu zaidi kwa karibu kila siku tangu atangaze nia yake hiyo ya kutaka kumrithi Freeman Mbowe aliyehudumu kwa zaidi ya miaka 20 madarakani ambaye mpaka Sasa bado hajasema kama atagombea au laa.

Freeman Mbowe anayeonekana kuyapoteza kabisa malengo ya kuanzishwa kwa CHADEMA na kijiegemeza zaidi kwenye kutafuta kukubalika kwake na dola pamoja na Viongozi wa CCM akiwemo Mwenyekiti wa Taifa wa CCM kuliko kwa Wafuasi na Wapenzi wa CHADEMA jambo hili linawakasirisha zaidi wanachama wa CHADEMA walio wengi kiasi Cha kutamani kubadili Mwenyekiti kwa gharama yeyote.

"Mbowe anakabiliwa na anguko Kali la imani toka kwa wapenzi na Wanachama wa CHADEMA ndio maana Lissu hata asipofanya kampeni yoyote sisi tutamchagua na nilazima" imeelezwa hivyo na kamanda mmoja toka Kilimanjaro jina tunalihifadhi,

Freeman Mbowe Mwenyekiti anayemaliza muda wake anakabiliwa na kosa la ukosefu wa Uaminifu na Uadilifu kwa wanachama na Wafuasi wa CHADEMA hasa baada ya kuonekana akiwa na ukaribu zaidi na Mwenyekiti wa Chama tawala kiasi Cha kupatiwa pesa kwa mamilioni ili apeleke kwenye makanisa pamoja na matumizi binafsi mathalani kwa Askofu Dkt Shoo alikopeleka zaidi ya Mil 150 za ununuzi wa gari pesa toka kwa Rais Samia ambae pia ni Mwenyekiti wa CCM.

IMG-20241215-WA0346.jpg

Je, huyu ndiye Mwenyekiti mpya wa CHADEMA ajae?​

 
Lisu anatafuta huruma sana, yani yeye kulia lia tuu muda wote, TLS hivyo hivyo ilikuwa, sasa CHADEMA hivyo hivyo. Mbowe agombee waache hii tabia ya kumbeba beba Lisu, kila anachotaka yeye apate, atakuwa mtu wa ajabu sana huyu.
 
Swali, Je, huenda Freeman Mbowe akajitoa ili kulinda heshima kidogo aliyonayo au yuko tayari kubeba aibu kwa gharama ya chawa wake||

Taarifa za chinichini ni kwamba,

Mtia nia wa nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA ngazi ya Taifa Bwana Tundu Lissu ameshamaliza Uchaguzi tayari kinachosubiriwa kwa sasa ni wanachama ambao ni wajumbe wa mkutano mkuu kupiga kura,

Watu wake wa karibu wanasema mtiania wao huyo huenda akashinda Uchaguzi huo kwa zaidi ya asilimia 70 ya kura zote zitakazopigwa kwani wanachama wa CHADEMA hasa wale walioduni sana kimaisha na kielimu wanaonesha kumuhitaji zaidi Lissu kwa sasa kuliko Mbowe kwa sababu wanazozijua wao wenyewe.

Lissu anayeungwa mkono kwa karibu na team nzima ya BAWACHA, BAVICHA , BAZECHA pamoja na idadi kubwa ya wajumbe wote wa mkutano mkuu Kuna kila dalili atashinda kwa kishindo.

Pitia hapa pia KURA: Je, ni nani kati ya Freeman Mbowe na Tundu Lissu anayefaa zaidi kuiongoza CHADEMA kwa Sasa?

Hata hivyo, Lissu anaonekana kupata nguvu zaidi karibu kila siku tangu atangaze nia yake hiyo ya kutaka kumrithi Freeman Mbowe aliyehudumu kwa zaidi ya miaka 20 madarakani ambaye mpaka Sasa bado hajasema kama atagombea au laa.

Mbowe anayeonekana kupoteza kabisa malengo ya kuanzishwa kwa CHADEMA na kijiegemeza kwenye kutafuta zaidi kukubalika kwake na Dola pamoja na kwa Viongozi wa CCM akiwemo Mwenyekiti wa Taifa wa CCM kuliko Wafuasi wa CHADEMA jambo hili linawakasirisha sana wanachama wa CHADEMA walio wengi kiasi Cha kutamani kubadili Mwenyekiti.

"Mbowe anakabiliwa na anguko Kali la imani toka kwa wapenzi na Wanachama wa CHADEMA ndio maana Lissu ata asipofanga kampeni sisi tutamchagua lazima" imeelezwa hivyo na kamanda mmoja toka Kilimanjaro jina tunalihifadhi,

Mbowe anakabiliwa na kosa la ukosefu wa Uaminifu kwa wanachama na Wafuasi wa CHADEMA hasa baada ya kuonekana akiwa na ukaribu zaidi na Mwenyekiti wa Chama tawala kiasi Cha kupatiwa mamilioni ili apeleke kwenye makanisa pamoja na matumizi binafsi ikiwemo kwa Askofu Dkt Shoo alikopeleka zaidi ya Mil 150 za ununuzi wa gari pesa toka kwa Rais Samia.

View attachment 3177680

Je, huyu ndiye Mwenyekiti mpya wa CHADEMA ajae?​

Ni yeye hapana shaka yoyote.
 
Kiukweli Uchaguzi huo utakuwa mgumu Japo Mbowe hajasema kama Atagombea.

baada ya kukusoma nikajiuliza kama unawajua kweli wapiga kura wa kuchagua mwenyekiti wa Chadema?

mkuu mshaurini Mbowe Freeman ampe nafasi Lisu tumuone miaka mitano hii. Alama za nyakati zinatushawishi hivyo. Upande wa pili wamezidisha dharau.
 
Kiukweli Uchaguzi huo utakuwa mgumu Japo Mbowe hajasema kama Atagombea.

baada ya kukusoma nikajiuliza kama unawajua kweli wapiga kura wa kuchagua mwenyekiti wa Chadema?
Siamini hata mara moja kuwa hawa watakuwa ni watu wa kushikiwa akili.
kama unawajua kweli wapiga kura wa kuchagua mwenyekiti wa Chadema?
Itanishangaza sana kama hao watu hawatakuwa tofauti na wenzao waliko kule CCM.
 
Kama Lissu atakuwa mwenyekiti itabidi abadilishe aina ya siasa anazofanya.
Sasa achaguliwe kwa siasa anayo iuza sasa, halafu aongoze kwa kufuata tabia nyingine? Huoni kuwa atakuwa ni mdanganyifu?
Na hao watakao mchagua, una hakika watampenda huyo mwenye "aina ya siasa" tofauti na ile waliyo iona wakati wakimpa uongozi?
 
Write your reply...lisu kuwa mwenyeliti ni sawa lakini tujiandae kisailolojia. Kwani naona akifanya analo taka yeye pasipo ushauri wa yeyote. Na tena anapenda ukuu tu na wala siyo kwa maslai ya chama.
 
Back
Top Bottom