Je, ilichukua muda gani kuanza kupata faida katika biashara yako?

Mimi Biashara ya Mgahawa imenichukua wiki moja tu kupata faida...sijaenda kwa mganga.
Mkuu kabla ya mgahawa uliwahi kufanya biashara yeyote? Je hio ndio ilikuwa mara yako ya kwanza kufanya biashara ya mgahawa?
 
Ndio niliuza sabuni baadae nikaanza uza dagaa(hawa ndo walinifanya nirpnde biashara nilipata faida baada ya two month)
Mkuu kabla ya mgahawa uliwahi kufanya biashara yeyote? Je hio ndio ilikuwa mara yako ya kwanza kufanya biashara ya mgahawa?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Maabara pia inanipa faida ila sijaiweka maana imenikosti pesa nyingi mno mpaka irudi hela yote ndo nitaanza kuhesabu faida.

Sabuni za Maji siwezi fanya hiyo biashara tena maana nilisulubika kishenzi...wateja watochi mpaka nikawa nawafosi wakope.

Dagaa nilianza kama mzaha ila nilifanikiwa baada ya miezi miwili japo pia nilikua nachomeka na jua kufuatilia mzunguko..faida ilinifanya nikanunua pikipiki nikampa mtu(nilijuta) nikauza.
Mkuu kabla ya mgahawa uliwahi kufanya biashara yeyote? Je hio ndio ilikuwa mara yako ya kwanza kufanya biashara ya mgahawa?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Chief ulikuwa unauza dagaa gani hao wenye faida za chap?
 
Mkuu unamaanisha maabara uliiendesha kwa hasara kwa muda mrefu now ndio inakulipa?

Vipi changamoto ya kodi ya fremu au lengo haikukupa mawazo.? Maana Fremu zilizokwenye mzunguko mkubwa wa watu zina bei kubwa

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Usemi uongo ndugu yangu
 
Samahani ndugu, kwa kusema kuwa na roho ya paka, unamaanisha nini?
 
Dagaa Nyasa ila nilikua nikishachukua mimi nawasambaza kwenye magenge nawaachia baada ya wiki au wiki mbili nafuata pesa zangu,,,changamoto ilikua dagaa ni wa msimu.
Chief ulikuwa unauza dagaa gani hao wenye faida za chap?
 
Mkuu sijasema napata hasara maabara haina hasara mkuu...nimemaanisha hivi nimetumia pesa nyingi kufungua ila sasa nafanya kazi napata pesa 10-30k inategemea na siku na maaabara yenyewe ni changa sasa hiyo ninayopata kwangu sihesabu kama faida mpaka nirudishe pesa niliyotumia kugharamia.
 
Dagaa Nyasa ila nilikua nikishachukua mimi nawasambaza kwenye magenge nawaachia baada ya wiki au wiki mbili nafuata pesa zangu,,,changamoto ilikua dagaa ni wa msimu.
Hawa. Dagaa sifa yao kubwa ni ipi, ni wale ambao tunaambiwa hawana mchanga?
Wenye magenge ulikua unawalipaje? Maana wao si wanakua na wale dagaa wa kawaida
 
Ndio hao hao hawana mchanga na wakikauka unaweza tafuna bila kupika(ila si vizuri minyoo na bakteria utakula).

Nilikua nauza kilo elfu 6-7 kutegemea na soko kisha nawapelkea wenye magenge labda kilo 5-10 kila genge wao wanauza kwa mafungu wakiisha kila kilo moja anaweza toa elfu 9-10 hivyo nikienda ananipa pesa yangu tu ambayo elfu 6 au 7 kutegemea na makubaliano.

Changamoto ilikua kuna muda napata hasara wakiingia maji halafu akashau kuwaanika unashindwa kumdai maana utaharibu mahusiano ya kibiashara,changamoto nyingine kuna maeneo ilichukua muda wao kuwakubali na nyingine ni dagaa wa msimu na nyingine ilikua kutembea na jua kali kusambaza na kufuata pesa.
Hawa. Dagaa sifa yao kubwa ni ipi, ni wale ambao tunaambiwa hawana mchanga?
Wenye magenge ulikua unawalipaje? Maana wao si wanakua na wale dagaa wa kawaida
 
Ulikua unanunua wapi na wanauza kwa kilo/ gunia tsh ngapi?
 
Nilikua nanua songea kule hawauzi kwa kilo walikua wanauza Dumla elfu 2500-3500 kutegemeana na ubora na upatikanaji wake..kipindi cha mvua hupanda hadi elfu 9 kwa Dumla mpaka 15.

Dumla moja ukipima unapata kilo moja na robo hadi na nusu kutegemea na ujazo wa kuuzaji
Ulikua unanunua wapi na wanauza kwa kilo/ gunia tsh ngapi?
 
Hakuna mfanya biashara wa ukwel ambae hajapitia ushirikina nakumbuka kipindi naanza anza maisha nilienda Sumba wanga wakat wa kurud nikapewa njiwa nije nimchinjie kazin kwangu njiwa kama wanne kweny basi kila mtu alikua ananishangaa Rukwa to dar sio mchezo
 
Nukta nambari moja idumu: miaka 2-3 ya kwanza ni migumu mno!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…