Je, ilichukua muda gani kuanza kupata faida katika biashara yako?

Je, ilichukua muda gani kuanza kupata faida katika biashara yako?

Ukitaka kufanikiwa kwa njia za ki-Mungu ufuate kanuni zifuatazo.
1.uanze kuishi maisha ya kumpendeza Mungu, kwa nje na sirini
2.kosea vyote ila usizini.ukikosea mengine ukaomba toba,Mungu atakusamehe na biashara itaendelea.
Ila ukizini lazima ufirisike kwanza,uaibike na ndio adhabu yako.
Ndio uje uanze mwanzo tena
3.Usiibe hela au kumdhulumu mtu Mali yake au kuiibia serikali then uje uanze biashara ukategemea Mungu ataibariki,NEVER

3.
Hebu twende mbele turudi nyuma kweli unaweza kuishi miaka mitatu au miwili bila kuzini ili tu ufanikiwe kwenye biashara au mimi ndio sijui maana ya kuzini?
 
Hakuna shida.

Kwanza inategemea upo eneo gani maana maeneno yanatofautiana,hapa namaanisha kuna maeneno kama mbagala,buguruni nk upatikanaji wa material sio ghali hivyo kuifanya biashara inakua unfauu kidogo.

1.Eneo nililopo mimi(hapa sitataja jina) vyakula vinavyopikwa wanauza elfu 1500 ila shida havina ubora hata kidogo.Mimi nikaamua kitu cha kwanza kuzingatia ni ubora wa chakula kwa bei ile ile.Kuna sehemu nafanya kazi wanauza ugali buku mzuri sana na faida wanapata sasa nikajiuliza kwanini kule buku jero na material rahisi kupatikana lakini chakula kibaya.

[emoji117]Wapishi wangu niliwaambia wapike chakula kizuri na kitamu(hapa sasa lazima uwe na mpishi mzuri maana kuna wengine kupika hawajaui)..niliwaambia waweke viungo vyote vinavyohitajika ili chakula kiwe na ladha nzuri,kitu ambacho wanafanya

[emoji117]Jambo la pili kwenye kila sahahni mimi naiongezea thamank kwa kuweka tunda(kipande cha ndizi au tikitikiti au tunda lolote huwa nabadilisha badilisha).

[emoji117]Hapa niliweza kufanya hivyo kwa sababu sinunui mahitaji reja reja nanunua jumla kuanzia mchele,unga na vitu vingine kisha nawauzia kwa kupima mfano wakitaka kupika wali labda kilo kumi watapima kilo kumi na baada ya biashara watatoa hela ya kilo 10.

[emoji117]Supu yangu nauza buku(nyama tatu) standard ila naweka na viazi hata kimoja au viwili pia na karoti kidogo(nina mpango wa kuongeza kipande cha mkate huko siku za usoni).

2.Usafi,hapa ni muhimu zaidi migahawa mingi usafi ni sifuri hawazingatii kabisa.Mimi niliwaambia nikienda nikakuta sehemu chafu basi watawajibika(hapa upate watu wasafi maana wengine hawana usafi hata ufanyaje ni wachafu).Sehemu yangu usafi ni wa hali ya juu kuanzia mazingira ,vyombo mpaka wahudumu(wawili tu).

3.Nidhamu,wanaongea na watu vizuri na pia nimewapiga marufuku kuhusu tabia ya umalaya(hapa nimewachukua watu ambao umri umesogea kidogo 25+ hivyo hawana utoto utoto..wanaongea na mteja vizuri na kwa nidhamu.

4.Muonekano wa sehmu yako hapa ndo kuna usafi,fenicha unazotumia na jengo..

Nimeandikwa kwa ufupi lazima ujiulize inawezekana vipi lakini jibu ni hili
[emoji117]Wakati naanza kufanya sikua na lengo la faida kwanza ,mimi niliangalia huduma kwanza ndo maana nilitaka kutoa kile ambacho nilikikosa nikenda kwenye mgahawa mingine.

[emoji117]Faida inakuja kadri unavyouza ukiuza sahani nyingi basi unapata pesa nyingi..kwa sasa wafanyakazi nimewaambia tunafanya kwa miezi mitano tuone trend ikoje na ninaboresha vitu kidogo kidogo na biashara inapokua nzuri zaidi basi na malipo yatapanda.

[emoji117]Faida ninayopata ukiondoka pesa zao na mahitaji mengine kwa siku inabik si chini ya elfu 10k+ kutegemea na siku, kitu ambacho kwangu nimeridhika na nina ona mafanikio hivyo nafanya jitihada kuongeza thamani.

[emoji117]Mpaka sasa nauza chakula tu,siuzi juice soda wala vitafunwa.Pesa hiyo inapatikana kwa kuuza wali,ugali na supu pekee.Nikianza kuuza vinywaji nk itapanda mara dufu maaana wateja wakija juice,soda na maji huwa nanunua kwingine(najichanga nipate friza kubwa).

Ukweli wakati naanza sikufikiri kama nitapata faida ila mimi binafsi napenda biashara,hivyo sikuwaza faida kwanza ila huduma.

Kwa machache hayo nadhani umeelewa.

Nb:ila inakupasa ufatilie mzee usikae kama muhindi kuagiza tu ,kwangu faida ya 10K+ sio ndogo hivyo nafatilia kama roho yangu na katika hao wafanya kazi jitahidi umtafute mtu anayeijua hiyo biashara manaa kwenye upimaji hapo ndo kuna bao.
Asante sana mzee baba. Mafanikio ya kwenye biashara yyt yapo kwny hizo point ulizozieleza
 
Ukitaka kufanikiwa kibiashara ni ama uwe mshirikina au umche Mungu, kauli hii aliniambia ndugu yangu mwaka 2017 nilipoenda kufanya biashara X mkoa wa Iringa. Asee kwa yaliyotokea nimeamini jamaa alikua sahihi sana 100%
 
Ahsante sana mkuu,Nimekuelewa vzr sana
Ila ni kwa nini dhambi ya kuzinzi ikawa na nguvu sana? Kuliko nyingine...

Kwa sababu tunaona hata Yusufu alikataa zigo la mke wa Kigogo wa serikali ya Misri (Potifa). Mungu akambariki Yusufu mpaka akawa waziri mkuu

Hii dhambi kwenye ulimwengu wa Roho inanguvu gani?

au ni kwa sabbu ya transmition kati ya Ke na Me????

Mtume Paulo anatuasa kuwa tuiogope sana dhambi ya uzinzi mana ni dhambi pekee inayo fanyika ndani ya miili yetu.
 
Mkuu sijasema napata hasara maabara haina hasara mkuu...nimemaanisha hivi nimetumia pesa nyingi kufungua ila sasa nafanya kazi napata pesa 10-30k inategemea na siku na maaabara yenyewe ni changa sasa hiyo ninayopata kwangu sihesabu kama faida mpaka nirudishe pesa niliyotumia kugharamia.
Hiyo biashara ni nzuri sana ukiwa mjanja na kama hyo proffesion ni yako mkuu.
 
Hili jibu lili-deserve likes nyingi na quotes za maana.

Ni jibu linaloweza hata kuwasaidia watu wengine kwny biashara zao hata kama sio za mambo ya misosi,maana ume-add value kwny karibu kila kitu unachokifanya kwny biashara.

More future success brother.
Yes, indeed...
 
Nimetumia 984K

Japo pesa imekua kubwa kutokana naukarabati ambao imenigharimu 320k
Mkuu kumbe kuanzisha mgahawa sio kazi ngumu

Maana mimi nilifikiria gharama za kodi ya pango, vyombo, jiko la mkaa + gesi, viti, meza, na mpishi lazima milioni mbili ikutoke,

Wewe uliwezaje kufanya yote hayo plus ukarabati kwa gharama ya 980k

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Yote 9 hapa "Ila ukitaka kufuata kanuni hii, uwe na uhakika hutafanya madhambi Mungu anayochukia, ukifanya tu unafirisika to zero. Trust me haswa uzinzi." Panachangamoto
una vijisenti halafu watoto wakali wanapita pita uwaangalie tu km zombi,sasa hizo pesa za nini.....
 
Mkuu hakuna ugumu na gharama inategemea na eneo.

[emoji117]Mimi kodi nimelipa 150k ni kodi ya miezi mitatu mbele ya ile fremu kuna eneo kubwa tu(hili eneo ndo lililokula pesa ya ukarabati vinginevyo ingekua chini ya hapo).
[emoji117]Meza plastic kampuni ya jambo meza 2 kila moja nilinunua elfu 37.
[emoji117]Viti vya plastic 8 kila kimoja nilinunua elfu 14
[emoji117]Sufuria ,sahani,vijiko,vikombe,bakuli nk nilitumia laki 1(hapa baadhi ya vitu nilichukua nyumbani)
[emoji117]Plate ya jiko la gesi nilinunua kwa mtu kwa elfu 30 na mtungi nilichukua wa nyumbani.
[emoji117]Jiko kubwa la chuma(yale yanatengenezwa kwa rim) rim nilichukua kwa bro fundi nilimpa elfu 20(fundi ni baba wa rafiki yangu)
[emoji117]Jiko la mkaa madogo mawili(nilichukua home)
[emoji117]Feni ndogo 1 ya elfu 45
[emoji117]Ukarabati(rangi,tofali,cement,mchanga na ufundi) laki 320
[emoji117]Mahitaji ya misosi(mafuta,mkaa,mchele nk) laki 130+

Nb:Siku 6 za Mwanzo nilifanya biashara ya kanisa nilipata hasara kubwa[emoji16][emoji16][emoji16]..nikifika home nitakupigia picha kitabu cha mahesabu.

Vitu nilivyoongeza Jana Meza 1 na viti vinne.lakini Pia mkuu kama ningetaka makubwa zaidi ingekua hela zaidi ya hiyo ila mimi nilitenga laki 5 nikajikuta nimetumia milioni kasoro elfu 16 hivyo hela inaweza kuongeza kutokana na upatikanaji wa vitu na mazingiro uliyopo.
Mkuu kumbe kuanzisha mgahawa sio kazi ngumu

Maana mimi nilifikiria gharama za kodi ya pango, vyombo, jiko la mkaa + gesi, viti, meza, na mpishi lazima milioni mbili ikutoke,

Wewe uliwezaje kufanya yote hayo plus ukarabati kwa gharama ya 980k

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
2. Lazima uchague kuwa mtu wa Mungu kweli au uwe mshirikina, bila hivyo hutoboi.
hapa ndio pa muhimu kuliko point zote, either umche Mungu na umtangulize katika biashara zako au uchague kufanya biashara kishirikina, ukichanganya hizo means mbili hutoboi NG'OO.
 
Mkuu hakuna ugumu na gharama inategemea na eneo.

[emoji117]Mimi kodi nimelipa 150k ni kodi ya miezi mitatu mbele ya ile fremu kuna eneo kubwa tu(hili eneo ndo lililokula pesa ya ukarabati vinginevyo ingekua chini ya hapo).
[emoji117]Meza plastic kampuni ya jambo meza 2 kila moja nilinunua elfu 37.
[emoji117]Viti vya plastic 8 kila kimoja nilinunua elfu 14
[emoji117]Sufuria ,sahani,vijiko,vikombe,bakuli nk nilitumia laki 1(hapa baadhi ya vitu nilichukua nyumbani)
[emoji117]Plate ya jiko la gesi nilinunua kwa mtu kwa elfu 30 na mtungi nilichukua wa nyumbani.
[emoji117]Jiko kubwa la chuma(yale yanatengenezwa kwa rim) rim nilichukua kwa bro fundi nilimpa elfu 20(fundi ni baba wa rafiki yangu)
[emoji117]Jiko la mkaa madogo mawili(nilichukua home)
[emoji117]Feni ndogo 1 ya elfu 45
[emoji117]Ukarabati(rangi,tofali,cement,mchanga na ufundi) laki 320
[emoji117]Mahitaji ya misosi(mafuta,mkaa,mchele nk) laki 130+

Nb:Siku 6 za Mwanzo nilifanya biashara ya kanisa nilipata hasara kubwa[emoji16][emoji16][emoji16]..nikifika home nitakupigia picha kitabu cha mahesabu.

Vitu nilivyoongeza Jana Meza 1 na viti vinne.lakini Pia mkuu kama ningetaka makubwa zaidi ingekua hela zaidi ya hiyo ila mimi nilitenga laki 5 nikajikuta nimetumia milioni kasoro elfu 16 hivyo hela inaweza kuongeza kutokana na upatikanaji wa vitu na mazingiro uliyopo.
Hongera chief, uchanganuzi umeshiba.
 
Mkuu hakuna ugumu na gharama inategemea na eneo.

[emoji117]Mimi kodi nimelipa 150k ni kodi ya miezi mitatu mbele ya ile fremu kuna eneo kubwa tu(hili eneo ndo lililokula pesa ya ukarabati vinginevyo ingekua chini ya hapo).
[emoji117]Meza plastic kampuni ya jambo meza 2 kila moja nilinunua elfu 37.
[emoji117]Viti vya plastic 8 kila kimoja nilinunua elfu 14
[emoji117]Sufuria ,sahani,vijiko,vikombe,bakuli nk nilitumia laki 1(hapa baadhi ya vitu nilichukua nyumbani)
[emoji117]Plate ya jiko la gesi nilinunua kwa mtu kwa elfu 30 na mtungi nilichukua wa nyumbani.
[emoji117]Jiko kubwa la chuma(yale yanatengenezwa kwa rim) rim nilichukua kwa bro fundi nilimpa elfu 20(fundi ni baba wa rafiki yangu)
[emoji117]Jiko la mkaa madogo mawili(nilichukua home)
[emoji117]Feni ndogo 1 ya elfu 45
[emoji117]Ukarabati(rangi,tofali,cement,mchanga na ufundi) laki 320
[emoji117]Mahitaji ya misosi(mafuta,mkaa,mchele nk) laki 130+

Nb:Siku 6 za Mwanzo nilifanya biashara ya kanisa nilipata hasara kubwa[emoji16][emoji16][emoji16]..nikifika home nitakupigia picha kitabu cha mahesabu.

Vitu nilivyoongeza Jana Meza 1 na viti vinne.lakini Pia mkuu kama ningetaka makubwa zaidi ingekua hela zaidi ya hiyo ila mimi nilitenga laki 5 nikajikuta nimetumia milioni kasoro elfu 16 hivyo hela inaweza kuongeza kutokana na upatikanaji wa vitu na mazingiro uliyopo.
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
Hamna kitu kinauma kama kufanya biashara ya kanisa,
Mbaya zaidi ndio uwe unaitegemea ikurishe, ikuvishe, ikuripie kodi n.k

Mimi binafsi nakupongeza, ninaplan ya kufungua kibanda cha chipsi faida nitakayo kuwa napata ndio nitaitumia kujikimu ili hii biashara kubwa ninayoifanya nisiivuruge

NB: Nafungua banda la chipsi kwa mtaji wa laki tano (sina hata kijiko)

Je unaushauri wowote?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom