JT2014
JF-Expert Member
- Jan 18, 2014
- 1,863
- 1,368
Swali langu ni hili kama hivyo vyote ni feki,AIDS haswa ni nini?Wakuu,mada hii ni pana mno,kuiandaa na kuiweka yote hapa hata kwa summary bado ni kubwa mno kwa kuwa inajumuisha mambo mengi sana,na ndio maana huwa natumia njia hii ya kutoa dokezo halafu watu huuliza maswali ambayo wanadhani yana utata nami huyajibu.
Nikiweka mada yote huku kama inavyotakiwa wana JF kwa jinsi ninavyowafahamu,hawataisoma yote na badala yake watakimbilia kupinga kwanza,utake usitake,hivyo ndivyo wana JF wengi walivyo,hii ni mojawapo ya tabia inayonivunja moyo sana,na ndio maana najitahidi kunusuru muda wangu pia.Nilitoa vidokezo 4 kusema kwamba ugonjwa huu ni feki katika nyanja hizo,hivyo mtu ambaye ana swali kwenye kidokezo chochote kati ya hivyo anaweza kuniuliza nami nitamjibu na kumpatia evidence pale anapohitaji ingawa najua pia hata nikitoa evidence bado watu hawataamini kwa kuwa tumepumbazwa akili zetu na taarifa hizi za uongo kwa muda mrefu sasa mpaka imefikia wakati tunaona ni kweli.Uongo ukiurudia rudia mara kwa mara mwishowe watu watauona ni ukweli(ukweli wa uongo).
VIDOKEZO;
1.Historia ya HIV/AIDS ni feki
2.Hypothesis ya HIV/AIDS ni feki
3.Vipimo vya HIV/AIDS ni feki
4.Dawa zinazotumika za HIV/AIDS yaani ARVs ni feki pia.
Karibuni kwenye elimu ya bure,ni muda wako tu.
Ikumbukwe miaka ya 1980s UKIMWI umeua watu wengi uganda
na hatimaye mkoa wa kagera,na ARVs zilikuwa bado
hazijagunduliwa.Na pia mkoa wa Njombe kipindi hicho
ikiwa wilaya sehemu za makete ukimwi umeua watu wengi sana.
sasa je,ukimwi ni nini na unasababishwa na nini?
maana hao walioleta majibu 'feki' kwa akili yangu
nadhani wameyaleta kwa sababu ya majanga
makubwa yaliyosababishwa na ugonjwa huu.
Naomba majibu,asante.