Je, Japan ndiyo nchi inayoongoza kwa kuthamini Utu na Ubinadamu?

Je, Japan ndiyo nchi inayoongoza kwa kuthamini Utu na Ubinadamu?

KENGE 01

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2021
Posts
1,705
Reaction score
4,217
Anaandika KENGE,

Katika ulimwengu wa sasa upendo umeingia doa,Upendo hakuna tena,Visa vya ukatili haviishi.Dharau,Majungu na najigambo kuanzia kwa mtu mmoja kwa mwingine(Individually) mpaka mataifa kwa mataifa(internationally).Mataifa yamekosa utu na kuviziana,kupigana na kuuana imekuwa kama tabia sasa

Lakini Nchini JAPAN mambo ni tofauti kidogo.Hawa watu wamekua wakishika vichwa vya habari kwa nyakati tofauti tofauti kwa matendo yao ya UTU na Ubinadamu

Moja ya habari iliovutia wengi mtandaoni ni picha inayowaonesha wafanya kazi(Staff) wa Japan Airline wakiwaomba abiria wao msamaha baada ya ndege kuchelewa kufika uwanjani kutokana na mvua na hali ya hewa kuwa mbaya.

20230804_202222.jpg
Sio hivyo tu,Kwa wapenzi wa Soka mtakumbuka kombe la dunia lililopigwa nchini Qatar.kuna tukio moja lilifanywa na mashabiki wa japan.Tukio ambalo liliibua hisia za watu wengi na kupelekea Japan kupewa TUZO ya timu yenye nidhamu.

_127757362_whatsubject.jpg
Ilikua ni baada ya ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Germany,baada ya mchezo mashabiki wa Japan walianza kusafisha uwanja kwa kuokota uchafu wa makopo na makaratasi waliotupa wakati wa kuangalia mpira.Huku kauli mbiu yao ikiwa ni 'Triple C' yani Cheer,Chant,Clean wakiwa wanamaanisha tunashangilia,tunafanya lolote lakini mwisho tutaacha tumesafisha

_127757366_whatsubject.jpg
Tofauti na nchi zetu,Africa mchezaji akifunga atatupiwa chupa,mawe na kumulikwa tochi.Na kama ni derby Mfano Simba na Yanga zinacheza pale taifa timu moja ikifungwa shabiki wanang'oa viti yaani ni vurugu mwanzo mwisho.

Matukio ni mengi ya kuelezea UTU wa watu hawa.Miaka ya nyuma walipitisha sheria wafanyakazi wa kucontrol marobot wanatakiwa wawe ni vilema.Ili kusaidia walemavu kwahiyo ukienda viwandani waendesha robot utakuta ni wengi ni walemavu.

Yapo mengi ya kuelezea UTU wa waJAPAN lakini licha ya kuwa nchi zenye acient ya Asia yaani wachina,Wakorea wamekuwa wakitafuta chokochoko na mataifa mengine.Yani kuvimbiana lakini ni tofauti kwa wenzao JAPAN sio watu wa skendo kabisa

JE kwa karne hii JAPANESE ndio watu wanaothamini UTU na UBINADAMU

Nawasilisha
Wako mtiifu
 
Nahisi kuna tofauti kati ya utu na ustaarabu!

Kwa mfano, mashabiki kuokota makopo uwanjani=ustaarabu

Vilema kupewa kazi viwandani=utu

Wafanyakazi wa ndege kuomba radhi=ustaarabu


Hakuna mifano mingine ya utu huko Japan?

Mfano, mtu akiwa mgonjwa yumo ndani anapewa kampani + chakula na jirani yake au mpaka aite mamlaka za serikali zije zimsadie bila hivyo anajifia ndani?

Mayatima wanapewa sapoti na wanajamii?

Wazee wanathaminiwa?

Mtu akiwa hana hela yaani ana maisha magumu anapewa msaada na ndugu, jamaa na marafiki?

Wajapani wanasaidiana kifedha mtu na mtu?

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Kwa kweli Japan ni moja kati ya nchi zilizostarabika sana, ni nchi ambayo raia wake wanaishi kwa kufuata misingi na utaratibu kwa hiari... Utamaduni huu unaanzia ngazi ya chini kabisa mpaka ngazi za juu.

Ni moja kati ya nchi nzuri sana kuishi kwa watu wanaopenda ustaarabu... Nchi zingine nafikiri ni zile zilizokuwa zinaunda umoja wa scandinavia, nazo ziko vizuri.
 
Hujawaona kwenye movie za Chinese vs Japanese [emoji23][emoji23][emoji23]
Zile movie nyingi ni za wachina..Ni kama zile za North na South Korea...Ila kuwa jirani na Mchina lazima mchapane tu siku moja..
 
Back
Top Bottom