Je, Jerry Silaa amemgomea Rais Samia kufanya kazi katika Wizara ya Habari?

Je, Jerry Silaa amemgomea Rais Samia kufanya kazi katika Wizara ya Habari?

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Kwanza kabisa nikiri wazi nakubali sana uchapakazi wa Jerry Silaa (Mb) hasa alivyokuwa Wizara ya ardhi. Lakini kama tujuavyo mteuliwa hana maamuzi ni wapi afanye kazi, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu aliamua kumuondoa Wizara ya Ardhi ambapo sote naamini tunakumbuka hekaheka zake akamhamishia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Tangu Jerry apelekwe huku ni kama AMEGOMA au AMEZIRA kufanya kazi, sio tu hajitumi wala kuonesha nia ya kujituma bali pia wenye sekta hiyo, yaani wanahabari WANAMLALAMIKIA.

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limeeleza kusikitishwa na mwenendo wa Waziri Jerry Silaa kutohudhuria matukio muhimu ya kihabari anayoalikwa.

1. Jerry Silaa ameshindwa kuhudhuria Mkutano Mkuu wa TEF uliofanyika jijini Dar es Salaam (alitumwa mwakilishi)
2. Jerry Silaa ameshindwa kuhudhuria Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari (EJAT) zilizotolewa Septemba 28, 2024.
3. Jerry Silaa ameshindwa kuhudhuria Kikao Jumuiya wa Maofisa Uhusiano (PRST) jijini Arusha.
4. Jerry Silaa alialikiwa Mbeya kwenye mkutano wa Wahariri hakwenda


Jerry ninayemfahamu ni mchapakazi lakini anavyoonekana ni kama hajapenda kuletwa kwenye Wizara hii kwani hata ukiangalia Kurasa zake za mitandao ya kijamii hakuna lolote linalohusu Wizara yake hii (Mpya) tofauti na alivyokuwa Ardhi, Kutokana na yote haya swali ni JE, JERRY SILAA AMEMGOMEA RAIS SAMIA KUFANYA KAZI WIZARA YA HABARI?

Pia soma
- Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF): Waziri Silaa ameshindwa kuwa karibu na Waandhishi wa Habari
 
Kwa hili kiukweli Rais alitukosea sanaa raia jamaa alifit sanaa hapo ardhi mapapa walipata kushika adabu
 
Tuanze kujadili kwanza wajibu na majukumu ya kisheria ya waziri katika wizara hiyo na baadae tuangalie kama hayo madai yako ni mojawapo ya wajibu na majukumu yake ya kisheria na ndipo tutakuwa na uwanja mpana wa kujadili hoja yako.
 
Hivi kutokuhudhuria hayo matukio ndio kugoma? Sijui. Huenda kuna sababu za msingi kabisa zilizomfanya ashindwe kuhudhuria na uzuri ni kwamba alituma wawakilishi kwenye matukio yote. Hata rais huwa anaalikwa kwenye matukio mengi, lakini huwa hahudhurii yote, mengine hutuma wawakilishi.
Watu wengine huwa hawana dogo. Wamejaa lawama tu. Wana mhukumu mtu bila hata kumpa nafasi ya kumsikiliza.
 
Siyo kazi zake.
Uliowataja are only pressure groups with their own agenda.
Kama Waziri wa Habari hakutani na Jukwaa la Wahariri, Wahariri wenyewe, Chama cha Maafisa uhusiano, hahudhurii matukio yao na wewe unasema sio kazi yake, nadhani unahitaji kupimwa
 
Hivi kutokuhudhuria hayo matukio ndio kugoma? Sijui. Huenda kuna sababu za msingi kabisa zilizomfanya ashindwe kuhudhuria na uzuri ni kwamba alituma wawakilishi kwenye matukio yote. Hata rais huwa anaalikwa kwenye matukio mengi, lakini huwa hahudhurii yote, mengine hutuma wawakilishi.
Watu wengine huwa hawana dogo. Wamejaa lawama tu. Wana mhukumu mtu bila hata kumpa nafasi ya kumsikiliza.
Inawezekana kabisa hajagoma LAKINI NDIO MATUKIO YOTE ASIHUDHURIE, DELEGATUS NON POTES DELEGARE, SIO KILA KITU UWAKILISHWE TU, WAWAKILISHI NI POWERLESS KWENYE MAAMUZI
 
Tuanze kujadili kwanza wajibu na majukumu ya kisheria ya waziri katika wizara hiyo na baadae tuangalie kama hayo madai yako ni mojawapo ya wajibu na majukumu yake ya kisheria na ndipo tutakuwa na uwanja mpana wa kujadili hoja yako.
Anza sasa kujadili
 
Kama Waziri wa Habari hakutani na Jukwaa la Wahariri, Wahariri wenyewe, Chama cha Maafisa uhusiano, hahudhurii matukio yao na wewe unasema sio kazi yake, nadhani unahitaji kupimwa
Mkuu ninyi ni wepesi sana, mnaandika vile vitu mnavyotumwa tu kuviandika(nyie mnaita self censorship).
Wananchi wanawadharau mnaposhindwa calling a spade a spade.
Nipimwe akili nisipimwe, waandishi wenu wengi ni makanjanja tu.
 
CCM wanapenda kudekezana sana, kwani hakuna wabunge wengine wanaoweza kuchukua hizo nafasi mpaka jamaa abembelezwe
 
Wizara ni mali ya serikali/nchi. Jerry ana arrogance, nashauri wamteme kwenye ubunge 2025 ili akachome mahindi kwa miaka mitano
 
Back
Top Bottom