Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Hilo jina langu mimi ndio limebeba tabia yangu Halisi.........
 
Yangu ni jina la mwigizaji wa muvie ya kikorea inaitwa Choi kan Chi
 
Ndio lina maaana ya majina mawili jina la mama yangu na langu
 
Ata mimi nakuogopa bana!!! Si kwa ukubwa huo wa akili
Mimi ni wakawaida sana kwa watu ambao ni standardized tuuh, hapa jukwaani my best friend naamini ni misschagga, sababu life yake ni natural.

I love those people wanajua to be themselves. I hate pretenders and much knowing kind of people.

Mimi kwako mbwembwe naficha uvunguni akili naficha kabatini kwa matumizi ya badae tunashare akili yako tuu.[emoji8]
 
Bixente Lizarazu ni mchezaji wa zamani aliowahi kuvichezea vilabu vya Bordeaux, Athletic Bilbao, Olympique Marseille na Bayern Munich. Pia alikuwa ni regular stater wa timu ya Taifa ya Ufaransa kwa kipindi chote alichoichezea(1992-2004).

Lizarazu alikuwa ni beki wa kushoto kwa timu zote alizochezea. Umahiri aliokuwa nao ulinivutia sana na kunifanya nianze kujifananisha na yeye na hata rafiki zangu niliokua tangu utotoni nao walipenda kuniita hivyo "mashoto Lizarazu".

Tangu amestaafu soka mwaka 2006 bado sijaona left-back mwingine bora zaidi yake hadi sasa, na hili kumuenzi nguli Huyu wa soka ninae muhusudu niliamua kutumia jina lake kama id kwa hapa JF.
 
Mkwawa Comlex.HILI JINA NIMELITUMIA KAMA KUMBUKUMBU YANGU KWA HIGH SCHOOL NILIYOSOMA HUKO IRINGA MIAKA YA LATE 1980's HADI EARLY 1990's SISI NA AKINA PRESDENT DR.JOHN MAGUFULI.SHULE YENYEWE REAL NAME YAKE NI MKWAWA HIGH SCHOOL(NICK NAME YAKE NI MKWAWA COMPLEX).TULIITA COMPLEX KWA KUWA,ILIKUWA NI HIGH SCHOOL,AT THE SAME TIME NI CHUO CHA UALIMU-DIPLOMA NA CERTIFICATES.MCHANGANYIKO HUO IKABIDI TUIITE HIYO EDUCATION CENTRE KUWA NI "COMPLEX" KWA UTUNDU WA VIJANA ENZI HIZO ZA SEC SCHOOL.
 
mimi jina langu la hapa jamii forum ni la kihindi. ni jina la Boss wangu wa kihindi wakati flani nafanya kazi kwa mhindi nilikuwa namchukia sana nikaona bora nijiite jina lake ili nisimsahau
 
Iruru, hili ni jina la aina mojawapo ya ndizi zinazolimwa mikoa ya arusha na Kilimanjaro. Ndizi hii huwa hailiwi na binadamu iwe ni kwa kupikwa ama ikiwa mbivu, ilinaonekana kama ndizi isiyo na maana na wengine huita ndizi ng'ombe! Aina hii ya ndizi hata hivyo huwa haina faida muda wote, ni ndizi muhimu sana hasa kipindi cha njaa, wakati huu iruru huliwa hata ikiwa mbichi pamoja na ukakasi mwingi iliyonao.

Niliamua kutumia hili jina jf kwa maana kubwa moja, nilijiunga jf mara kadhaa kuanzia 2010 lakini kutokana na magwiji na wataalamu wa hoja niliyowakuta huku niliojiona iruru kwani hoja zangu hazikuwa na mashiko saaana! Hata hivyo, 2012, niliguandua kuwa hata iruru kuna wakati huonekana dhahabu hasa wakati ndizi pendwa zikiwa zimehadimika! Leo nafurahia, nami hujiokotea like kutoka kwa wachache kwenye michango yangu hasa wale magwiji wanapoadimika! Mie ndo iruru bhana hahahaaaaa.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…