Je, kanisa la mhubiri Christopher Mwakasege liko wapi?

Je, kanisa la mhubiri Christopher Mwakasege liko wapi?

Mi hata mnipige mawe nitazidi kusema mwalimu mwakasege ni yule wa zamani wa leo ni mchumi.
 
Kasome Waefeso 1:5. Ally nimeipenda hii ya kutaka andiko. Kumbe unajua kuwa kila kitu kinathibitishwa na andiko. Mungu akubariki.

..kurahisisha, ungeandika waefeso 1:5 inasema nini ?
 
Mi hata mnipige mawe nitazidi kusema mwalimu mwakasege ni yule wa zamani wa leo ni mchumi.

Nadhani unashindwa kuelewa kwamba,Biblia imejaa mafundisho ya uchumi mfano 2Wakorintho8:9,Mithali22:7, 3Yohana1:2, Isaya48:17
 
Ni mwizi .... kupitia sadaka za waumini "walio zaliwa upya" kwa kumwamini Kristo kuwa Bwana na Muokozi wao
 
yote kwa yote msimhukumu maana Mungu ndo anaijua vizuri mioyo ya watu ilivyo,cha msingi unachokipata kitumie kwa faida na siyo kumsema mtu kwa kitu ambacho huna uhakika nacho
 
Ukiacha waalimu wote wa dini ambao wanahudumiwa na taasis zao kama CCM..ah samahani kama Wakatoliki, waluther, adventsta, anglicn., na baadh ya taasis za kiislam.. wengine wengi.. hasa wa madheheb ya kilokole.. njaa zimewapanda kichwani siku nying mno..!
 
Mi hata mnipige mawe nitazidi kusema mwalimu mwakasege ni yule wa zamani wa leo ni mchumi.

uko sahihi, zamani alifundisha mambo machache, ila siku hizi ame-advance anafundisha hata mambo ya uchumi, hivyo kumuita mchumi hujakosea dada yangu.
 
Hata unipe mistari mingapi,
simkubali mimi tu lakini.

Usimkubali kwa kuwa wewe sio Mrs wake. Wacha atulishe neno la Mungu kwa ujumla bila kusaau mafundisho mengine ambayo watumishi wa wengine hawawezi kusimama kuyaongelea kwa kuwa hawana elimu hiyo.
 
Kwakweli mi sina la kuongea zaidi ya kuwaomba kuwa TUZIDI KUMUOMBEA mtumishi wa Mungu.
Mwaka jana ilifanyika toba ya kitaifa pamoja na maombi mbali mbali pale Biafra kinondoni.
Nashukuru sana nilikuwa mmoja wa watu tuliokwenda kuliombea taifa letu.
Tena kuna kitu ambacho NILIOMBA kuhusu nchi yetu, nashukuru hicho kitu kinaanza kijidhiliriha, kweli Mungu mkubwa.
Hiki cha wasiojulikana?

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu naona una hoja nzito hapo kwenye rangi. Nakusihi utudadavulie kwa undani kidogo

1. Rangi Nyekundu & kijani : Jinsi yeye Mwl Mwakasege binafsi anavyowahiza watu na kuwaandalia yeye binafsi safari za kwenda Israel kama njia ya hao watu kuponywa au haja zao zingine kujibiwa na Mungu.

2. Rangi ya Blue : Jinsi yeye Mwl Mwakasege alivyoona kwenda Israel kungemfanya Lowasa atakasaswe katika kashifa ya Richmond ambayo ilisemekana yeye kuwaa muhusika mkuu. Ningefurahi pia kama ungetuambia jinsi wewe ulivyo karibu (uhusiano wako) na Mwl Mwakasege

Nasubiri maelezo yako kwa hamu sana.

Ahsante

Mwalimu Mwakasege yuko juu sana huwezi kumlinganisha na watumishi wengi kwasababu moja kubwa,hafungwi na minyororo ya madhehebu.Nimewahi kuhudhuria semina nyingi za Bwana Mwakasege sikuwahi kumsikia hata siku moja akiwaelekeza watu waende kwenye dhehebu fulani fulani.

Kuna kasoro moja kubwa ambayo nimeiona kwa Bwana Mwakasege siku za karibuni amejikita sana kuwahimiza watu kwenda Israel.Amefikia hatua ya kuandaa safari za kwenda Israel kwa wanandoa as if uponyaji unapatikana unapokwenda Israel.Bwana mwakasege ndiye aliyemshauri E Ngoyai Elowassa kwenda Israel mara baada ya kuitia hasara kubwa nchi yetu na mkataba wa RICHMOND badala ya kumshauri aombe radhi watanzania kwa uzembe anamshauri aende Israel.
 
Ni mjanja mjanja tu wa hapa mjini ana taasisi yake nje ya kanisa lake kwa ajiri ya kupiga hela
 
Back
Top Bottom