Je, Katiba yetu inamruhusu Rais Samia kukaa miaka 15 Ikulu?

Je, Katiba yetu inamruhusu Rais Samia kukaa miaka 15 Ikulu?

Mleta mada umetumia neno “kukaimu” vibaya na neno hilo linaweza kupotosha mada nzima. Kukaimu ni kushikilia madaraka kwa muda. Rais SSH alikaimu siku toka JPM alipokufa mpaka siku anaapishwa! Baada ya kuapa alishika madaraka ya uRais.

Katiba ya Tanzania inatambua muhula kuwa miaka mitano na hairuhusu kuongoza kwa zaidi ya mihula miwili, bila kujali mhula mmoja kati ya hiyo miwili ni miaka mitano kamili au pungufu. Ndio maana inaeleza kitakachotokea kama Rais aliye madarakani atakufa na atarithiwa na makamu wake. SSH angekuwa na nafasi ya kuongoza zaidi ya miaka 10 kama Rais JPM angekuwa amekuwa madarakani kwa zaid ya robo tatu ya muhula (JPM alitufa takribani miezi 6 baada ya kuapishwa) na hivo kipindi kilichobaki kitahesabiwa kwa Rais SSH (ndio maana inaitwa Serikali ya awamu ya sita)!! Na awamu ya Rais haizidi mihula miwili.

Namna pekee ya SSH kuwa mgombea wa 2030-35 ni kufanya kama wengine walivofanya - kutumia Bunge kubadilisha matakwa ya Katiba.

Hii ni awamu ya sita na kama anataka kuwa mgombea 2030 aanze kusema hii bado ni awamu ya tano na kwamba bado anakaimu madaraka ya Rais (jambo gumu kusema kwa sababu hawezi kuwa anakaimu wakati yeye sio Makamu wa Rais kama Katiba inavyotaka).

umeiweka vizuri sana chief, shukrani
 
Ni kweli kabisa, hii Jf imejaa viazi vingi sana. Hasa viazi ufipa, aaaaaah vile viazi havifai kabisa.

Watu hawajui chochote zaidi ya matusi, wabishi wenye kujiona wako sawa kwa kila kitu.
Wao wanadhani hii inchi ni kama club tu😅.
Kifungu 40(4) "....Endapo Makamu wa Rais anashika kiti cha Rais kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 37(5) kwa kipindi kinachopungua miaka mitatu ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara mbili, lakini kama akishika kiti cha Rais kwa muda wa miaka mitatu au zaidi ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu...."
 
Mkuu Dr Akili, kiukweli kabisa, kwenye hili, hakuna utata wowote. Ndio maana kule mwanzo nilisema elimu ya katiba inahitajika sana kwa Watanzania wengi. Katiba imeandikwa kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili ila watu ni wavivu kusoma, hawasomi katiba na very unfortunately katika mitaala yetu hakuna somo la katiba!. Tumewaachia wanasheria kitu ambacho sio right, sio fair. Kila mtu anapaswa kusoma katiba na kuijua katiba.

Mambo ya haki ya kuchaguliwa tena kwa kipindi cha pili kwenye nafasi ya uraisi wa JMT yanaongozwa na ibara ya 9 kufungu cha 15 cha sheria namba 34 ya mwaka 1984 iliyofanyiwa mapitio mwaka 1994 na kuingizwa kwenye Ibara ya 40 ya Katiba ya JMT ya mwaka 1977, kwenye kifungu kidogo cha 4, imeelekeza vizuri na wazi kabisa na bila utata wowote.
4) "Endapo Makamu wa Rais anashika kiti cha Rais kwa
mujibu wa masharti ya ibara ya 37(5) kwa kipindi kinachopungua miaka mitatu ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara mbili, lakini kama akishika kiti cha Rais kwa muda wa miaka mitatu au zaidi ataruhusiwa kugombea nafasi ya Rais mara moja tu".

Hii maana yake, kwa vile Samia anashika madaraka kwa kipindi cha zaidi ya miaka mutatu, hivyo hii inahesabiwa ndio awamu yake ya kwanza, bado anayo fursa ya awamu nyingine moja ya mwisho.

Endapo JPM angechomoka baada ya kutumikia urais kwa miaka 2 na nusu, hivyo Samia kushika kwa kipindi kisichozidi miaka 3. Then kipindi hicho Samia angehesabiwa kuimalizia ngwe ya JPM, hivyo Samia angekuwa na fursa za kugombea awamu zake zote mbili, kuanzia 2025-2035.
Hivyo hakuna awamu ya less than 3 years .
P

kwahiyo akitaka kugombea kwa awamu nyingine ya tatu kwa katiba hii atakua anaharibu, okay.
 
Ni kweli na ni logical ulichokisema. Awamu ya kwanza ya SSH ni miaka 4 (na nusu). Awamu yake ya pili itakuwa miaka 5 yaani 2025 - 2025.

Ni bahati nzuri (? mbaya) kwamba awamu yake ya kwanza ni miaka 4 na ushee aliyobakiza mtangulizi wake. Sasa kwa mfano mtangulizi wake angekuwa kabakiza miezi 6 au mwaka mmoja ina maana bado awamu yake ya kwanza ingalikuwa miezi 6 au mwaka mmoja tu? Nadhani utata uko hapo. Katiba inasemaje hapo? Ni sawa kwamba awamu ya kwanza inaweza kuwa hata ya mwezi mmoja tu?
Mbona hili li, efafanuluwa huko juu.
 
Ni kweli kabisa Samia hakaimu Urais lakini ni kweli kabisa kuwa katiba haijaweka wazi kwa mtu anayeapishwa baada ya Rais aliyemtangulia kufa kabla ya muda wake kufa, je ndiyo muhula wake wa kwanza au anakamilisha muhula na baada ya hapo ataanza kuwania muhula wake wa kwanza?
Inaonekana una akili nzito Sana.
Si umewekewa hadi vifungu hapo juu vibavyoeleza kuwa kama ataksimu kwa miaka mitatu na kuendelea badi hiyo itahesabiwa kama awamu yake ya kwanza
 
kwahiyo akitaka kugombea kwa awamu nyingine ya tatu kwa katiba hii atakua anaharibu, okay.
Mkuu miller, tuacheni hizi asumption mbofu mbofu za kwa Mama kutaka kugombea awamu tatu!, kwanza hata hiyo awamu ya pili, hajasema atagombea!, sasa hiyo ya awamu ya tatu unaitoa wapi?.

P
 
Mkuu Mwl.RCT , Ukweli mwingine ni mchungu kumeza ila ndio ukweli.
P
 
Mkuu miller, tuacheni hizi asumption mbofu mbofu za kwa Mama kutaka kugombea awamu tatu!, kwanza hata hiyo awamu ya pili, hajasema atagombea!, sasa hiyo ya awamu ya tatu unaitoa wapi?.

P

sawa ni asumption zetu chief, je ikitokea akitaka kugombea katiba itamruhusu au itamfunga?
 
sawa ni asumption zetu chief, je ikitokea akitaka kugombea katiba itamruhusu au itamfunga?
Hoja nyingine kiukweli zinatia hasira!. Katiba imesema mwisho ni awamu mbili. Mama ndio kwanza yuko awamu yake ya kwanza, bado hajasema kama atagombea awamu yake ya pili ya 2025-2030, sasa hili la awamu ya tatu linatokea wapi?!.

Katiba ndio imeweka ukomo wa awamu mbili, mtu unauliza " je ikitokea akitaka kugombea awamu ya tatu, jee katiba itamruhusu?", hili sasa ni swali gani?!. Katiba iko wazi mwisho awamu mbili, haiwezi kutokea mtu kutaka kugombea awamu ya tatu wakati mwisho ni awamu mbili!. Halafu watu wakiitwa viazi humu mnalalamika!.
P
 
Hivi imekaaje kwa utaratibu wa Katiba yetu?

Maana:
Pierre Nkurunziza alikaimu miaka mitano ya mwenzie akaja kukaa kumi yake ikawa 15.

Edgar Lungu alikaimu miaka mitatu akakaa yake mitano na akagombea mitano mingine akashindwa.

Je, kwetu Tanzania SSH kwa kuwa amekaimu mitano ya JPM, sasa anaweza kugombania mitano ya kwake ya kwanza 2025 na pia mitano yakwake ya pili 2030?

Imekaaje wajuzi wa haya mambo kwa utaratibu wa kikatiba ulivyo.
Aliyekudanganya kuwa Katiba inafuatwa ni nani? Tangu awamu ya tano na hii ya sita Katiba imesiginwa na inaendelea kusiginwa,ukileta fyoko unamiminiwa risasi za kutosha. Hivi sasa ni undava undava tu Rais ndiye kila kitu, ukichanganya na yale mazuzu kule mjengoni ni mwendo wa kujiamulia tu akae madarakani hadi kifo.
 
Back
Top Bottom