Je kifo cha 'Jasusi mbobezi' kimeondoka na kichwa leo?

Je kifo cha 'Jasusi mbobezi' kimeondoka na kichwa leo?

Basi bwana, baada ya kifo cha Jasusi mbobezi zilipenya za chini ya kapeti kuwa Jasusi karestishwa.

Watu wakachimba zaidi kutaka kujua kulikoni Jasusi kujasusiwa?.

Wanyetishaji wa kijiweni wakadai kuwa Jasusi kapigwa faulo moja matata kama Salum Kabunda au Roy Kean ndiyo maana kavuta

Mnyetishaji akadai hana ushahidi kama "aliyeomba kupumzika" alihusika lakini homeboy wake mmoja aliyekuwa mnene kwenye kilindi cha wavaa suti nyeusi alicheza faulo. Lengo ni kusaidia homeboy wake aendelee kuwa mshika mikasi wa kuzindua shughuli. Maana inasemekana Jasusi mbobezi angeweza kuchukua nafasi yake Twente Twente Five

Sasa Malkia wa nyuki alipopewa inshu akafumua fumua kilindi cha wavaa suti na yule aliyedhaniwa kuhusika akawekwa pembeni. (Mnakumbuka zile panguapangua kwenye ofisi za kilindi cha wavaa suti kwenye nchi ya wadanganyika hadi mnene wao kutoka mji wa wala migebuka kuweka pembeni au vipi)?.

Sasa leo mla migebuka kawekwa pembeni ili in the future asiwe mbeba mikasi ya kuzindua miradi tena. Kiufupi anaenda kula pensheni yake. Hii si kawaida maana kakaa pele kwenye kula haluwa na kiti cha kunesanesa kwa miaka minne tu.

Hii ndo kijiweni watu wananong'ona kuwa Inshu ya Jasusi mbobezi kudanja imemuweka pembeni?
Yote haya ni kwasababu ya kulinda
1737353145220.png
 
Penis-we angalau ajifunze kwa bwana migebuka ni bora kuachia ngazi legacy ikabaki daima, vile vile kama alichofanya mdogo wake "heavy" kuachia uenyekiti wa zambarau party waendeleze wengine gurudumu
Penis-we = Sultan AL ASSAD
 
Hizi code mnazotembeza humu wazee mbona nyeupe kabisa kila mtu anaelewa. Jaribuni kuficha zaidi
 
Wanaukataa ukweli kuwa hakuna binadamu atakayeishi milele hata kama atalindwa kwa nukes..
Na ajabu ni kwamba imeshathibitika kwamba alikuwa anaumwa ugonjwa wa moyo tangu akiwa UDSM halafu bado watu wanaamini kifo chake lazima kimesababishwa na mtu/watu.
 
Huu mchezo hautaki haraka, ndani ya siku tisini zijazo tutaelewa picha nzima na mchezo ulivyo. Wakuda wanasema, hii ngoma bado mbichi mnoo.

Hali ni tete kila angle, lolote linaweza kutokea kwa yoyote yule.
Duh 🙄 !
Mnatutisha bhana !
Hamna kitu !
 
Hivi ikitokea Samia ame rest in peace kesho au keshokutwa, Dr Philip Mpango si ndiye atakuwa Rais..?

Huyu Nchimbi atakuwa nani..?

Mbona CCM na Samia wanafanya maamuzi ambayo ni very premature..?

Kama anaendelea kuwa VP mpaka baada ya uchaguzi, kulikuwa na sababu gani ya kimantiki kutangaza barua yake ya kujiuzuru wakati wameshajadiliana naye akakukubali kuendelea kuhitimisha awamu hii..?
Ingeeleweka vipi wamtangaze mtu atakaye shikilia nafasi yake wakati yeye yupo?
Ilikuwa kutafuta uhalali kwa wanachama wao.
 
Back
Top Bottom