Elections 2010 Je Kikwete atakubali matokeo au atakuwa kama Mugabe

Elections 2010 Je Kikwete atakubali matokeo au atakuwa kama Mugabe

Mkuu MwanaFalsafa1 naelewa sana unachojaribu kukielezea ila ningependa nikukumbushe kuwa kulingana na mwamko wa hivi sasa, dont rule anything out na naomba uzingatie haya ;

  • Kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 Chadema haikuwa tishio hata kidogo kwenye chaguzi zote mbili zilizofanyika kwenye majimbo ya Busanda na Biharamulo na iliishia kuambulia karibu asilimia 5% tu ya kura katika majimbo yote mawili.
  • Kwenye chaguzi ndogo zilizofanyika miaka minne baadaye 2009, Chadema huko Busanda iliweza kutoa ushindani mkali kwa chama cha CCM kwa kupata asilimia 42% na Biharamulo ikazoa asilimia 48% ya kura zote pamoja na mizengwe yote ya chama tawala.
Hebu fanya hesabu utuambie ongezeko kama hilo ni asilimia ngapi na ueleze ni kwa nini bado ni vigumu kwako kuamini kwamba ndani ya miaka mitano chama kilicho pata asilimia 11 au asilimia 5 kina weza kupanda ghafla bin vuu na kuvuka kura asilimia 51 za kuukwaa uraisi. Pia naomba uzingatie kuwa hadi wakati huo mgombea Uraisi kutoka Chadema bado alikuwa hajajitokeza na hivyo hivyo mwamko kama tunavyoushuhudia hivi leo ulikuwa bado.

Mazee ukishaona asilimia 48 dhidi ya chama "twawala" ujue chances kubwa sana kwamba zengwe limetembea hapo.
 
Mkuu MwanaFalsafa1 naelewa sana unachojaribu kukielezea ila ningependa nikukumbushe kuwa kulingana na mwamko wa hivi sasa, dont rule anything out na naomba uzingatie haya ;

  • Kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 Chadema haikuwa tishio hata kidogo kwenye chaguzi zote mbili zilizofanyika kwenye majimbo ya Busanda na Biharamulo na iliishia kuambulia karibu asilimia 5% tu ya kura katika majimbo yote mawili.
  • Kwenye chaguzi ndogo zilizofanyika miaka minne baadaye 2009, Chadema huko Busanda iliweza kutoa ushindani mkali kwa chama cha CCM kwa kupata asilimia 42% na Biharamulo ikazoa asilimia 48% ya kura zote pamoja na mizengwe yote ya chama tawala.
Hebu fanya hesabu utuambie ongezeko kama hilo ni asilimia ngapi na ueleze ni kwa nini bado ni vigumu kwako kuamini kwamba ndani ya miaka mitano chama kilicho pata asilimia 11 au asilimia 5 kina weza kupanda ghafla bin vuu na kuvuka kura asilimia 51 za kuukwaa uraisi. Pia naomba uzingatie kuwa hadi wakati huo mgombea Uraisi kutoka Chadema bado alikuwa hajajitokeza na hivyo hivyo mwamko kama tunavyoushuhudia hivi leo ulikuwa bado.

Mkuu nakubaliana na wewe lakini maelezo yako haipaint the whole picture bali ina isolate eneno moaj. Kwanza kwenye hayo majimbo mkuu hizo ni chaguzi za ubunge wakati tunaongelea uraisi but I will give it the benefit of the doubt. Mkuu ukisema jimbo fulani mmegain hauelezei majimbo mliyo pungua. Kwa haraka haraka naweza nika taja majiimbo ambayo yalikua ya Chadema na yaka rudi CCM mfano jimbo lililo kuwa la Marehemu Chacha Wangwe (R.I.P.). So ukigain sehemu moja uka poteza nyingine hapo chama kina baki stationary.

Pia mkuu kuhusu msisimko uliopo sasa naomba Chadema muwe very careful kwa sababu perception can be very deceiving. Kwanza lazima uangalie hao wenye msisimko ni wakina nani? Na je ni asilimia ngapi ya wapiga kura? Maana hauwezi ukaona watu wa mijini au wasomi au wana JF wana msisimko ukaichukulia kama trend ya wapiga kura wote. That's why kwenye threa moja nime suggest vyama vya upinzani viwe vina fanya poll kuangalia ni wapi wana simama.

Kwa hiyo mkuu kwa sababu tunaangalia uachguzi wa uraisi lazima tuangalie nchi nzima na si majimbo mawili tu. Sawa Busanda na Biharamulo Chadema ili panda na kufikia asilimia 42 but hauja onyesha proof kwamba hii ni trend nchi zima bali ni sawa na kuassume kwa sababu ume faulu mtihani wa biologia basi na geographia nayo lazima utafaulu kutokana na matokeo ya biologia.

Kwa hiyo mkuu the opportunist in me wants to believe that Watanzania wapo smart enough na watamchagua mgombea aliye bora (i.e.Slaa) but the realist in me does not see that happening. Ni wakati tuna bidi tutambue kwamba mvuto wa mgombea pekee siyo unaoshinda uchaguzi. Party mechanism na planning plays a big part. Siwezi sema chochote kuhusu strategy ya Chadema because I'm not an insider but if they have a well placed game plan na wamejiandaa tokea mwanzo(meaning hata kabla ya sasa) then chances ipo. It's up to Chadema.
 
Je vyama vya upinzani navyo vitakubali matokeo kama Kikwete akishinda kwa kishindoo?

Hilo nalo neno mkuu. Miaka kadhaa iliyo pita kuna mtu fulani influencial kutoka Afrika ali hojiwa na CNN au BBC. Aka sema Afrika kwa mtazamo wa vyama vya upinzani ni kwamba uchaguzi si huru na haki mpaka upinzani ushinde. Kwa maana chama tawala kikishinda tu basi uchaguzi haukuwa wa huru na haki. Africa bado demokrasia ni barabara yenye njia moja.
 
Of course Kikwete kashapitishwa na CCM na sasa hivi ndiye mgombea pekee wa CCM, kwa hiyo namuongelea Kikwete mgombea wa CCM. Kikwete si mgombea wa CHADEMA kwa hiyo huwezi kusema kwamba naongelea Kikwete mgombea wa CHADEMA. Tanzania hairuhusu ugombea binafsi, kwa hiyo huwezi kusema namuongelea Kikwete mtu binafsi.

Maswali yako yanaibua maswali ya kufikirika, vipi kama Kikwete angekataliwa na CCM, halafu CCM wakamuweka mgombea mwingine, Kikwete angekuwa na confidence aliyonayo sasa? Angekuwa na nafasi aliyonayo sasa? Of course asingekuwa navyo, kwani CCM ina party machinery na name recognition nchi nzima.

Wakati Benjamin William Mkapa anateuliwa kuwa rais wala hata hakuwa anajulikana. In fact hata katika kutangaza nia alikuwa ni mtu wa mwisho nafikiri. Na watu wengine walisema wanamjua zaidi Ken Mkapa (Mchezaji mpira wa Yanga) kuliko Benjamin Mkapa. Lakini kwa sababu alikuwa mgombea wa CCM alipita.

Vivyo hivyo Ally Hassan Mwinyi, mtu ambaye alishajiuzulu uwaziri kwa scandal la mauaji ya vibibi. Lakini CCM ikamshika mkono miezi michache tu baada ya kutangazwa kama "rais wa muda Zanzibar" baada ya kipindi cha "machafuko ya hali ya hewa ya kisiasa" huko Zanzibar yaliyomfanya Sheikh Aboud Jumbe Mwinyi kujiuzulu, lakini watu wakaimba "Ally Mwinyi Ally Mwinyi, NDIYO, NDIYO, NDIYO, mwenye busara na hekima,NDIYO NDIYO NDIYO" watoto wa kihuni katika kubeza collectivism miaka ya baadaye (miaka ile hata Mzee Maharage aliogopa kumkataa) wakaja ku parody wimbo kwa kuongeza "aliku--ra migombani, NDIYO, NDIYO,NDIYO".

Kwa nini nasema haya yote ? Naonyesha umuhimu wa chama katika kampeni, chama kinaweza kumchukua mtu aliyekaa kama jiwe na kumfanya rais. Tanzania CCM ndiyo inachagua rais, si watanzania per se.

Lakini miaka hii ya karibuni, ambapo tunaona hata CCM inagawanyika katika makundi, mtu anaweza kusema hii automaton inaanza kwisha na kila mtu anaanza kujipalilia mwenyewe ndani ya chama na katika makundi haya.

Ndiyo ukauliza, huyu Kikwete ana confience yeye mwenyewe au kwa tiketi ya CCM ? Narudia, of course kwa tiketi ya CCM, kwani yeye hajaona kilichompata Mrema ?

Ila kwa sababu sasa hivi CCM hawana utamaduni wa kumkataa rais kumalizia muhula wa pili, na kwa sababu Kikwete tayari ndiye de facto / de jure mgombea wa CCM pekee (baada ya Shibuda kugwaya) as far as the campaign is concerned hakuna tofauti kati ya Jakaya Kikwete the person and the CCM candidate.

After all Tanzania hatuna utamaduni wa kufuatisha institutions kama vyama, bado tuna utamaduni wa kufuatisha strongmen.

Na Kikwete ndiye strongman wa CCM, kama si Tanzania.

Asante kwa maelezo yako ambayo kwa namna fulani yanapingana na dai lako la awali kwani kwanza. Uzito wa dai la kushinda kihalali unapungua kwani unasisitiza jinsi ilivyo vigumu kuiondoa CCM madarakani kwa sababu wao ndio wanaamua nani awe Raisi wa nchi hii na siyo wananchi per se ! Hapa ni kama vile unakubaliana na mleta mada kuwa pamoja na wananchi kuamua tofauti, utamaduni wetu wa kufuatisha strongmen unaweza kumpa kiburi Kikwete (CCM) asikubali matokeo tofauti na akawa kama Mugabe. Hivyo kutoafiki na dai lako la awali liko pale kwamba je, kwa mtu (chama) kama huyo, hiyo confidence ya kushinda kihalali inatoka wapi kama si ukweli kuwa wananchi hata wafanye nini watalazimika kumchagua tu yeye kuwa Raisi ?
 
Mkuu nakubaliana na wewe lakini maelezo yako haipaint the whole picture bali ina isolate eneno moaj. Kwanza kwenye hayo majimbo mkuu hizo ni chaguzi za ubunge wakati tunaongelea uraisi but I will give it the benefit of the doubt. Mkuu ukisema jimbo fulani mmegain hauelezei majimbo mliyo pungua. Kwa haraka haraka naweza nika taja majiimbo ambayo yalikua ya Chadema na yaka rudi CCM mfano jimbo lililo kuwa la Marehemu Chacha Wangwe (R.I.P.). So ukigain sehemu moja uka poteza nyingine hapo chama kina baki stationary.
Siyo kweli Mkuu, Chadema walilitetea jimbo la Tarime. Labda unasahau alivyotimka Makamba usiku wa manane bila kuaga akiikimbia Tarime.
Pia mkuu kuhusu msisimko uliopo sasa naomba Chadema muwe very careful kwa sababu perception can be very deceiving. Kwanza lazima uangalie hao wenye msisimko ni wakina nani? Na je ni asilimia ngapi ya wapiga kura? Maana hauwezi ukaona watu wa mijini au wasomi au wana JF wana msisimko ukaichukulia kama trend ya wapiga kura wote. That's why kwenye threa moja nime suggest vyama vya upinzani viwe vina fanya poll kuangalia ni wapi wana simama.
Kama kuna sehemu zinaponipa tumaini ni hizo unazoziita za vijijini kuliko mijini na mifano mpaka sasa ipo. Laiti ungejua uvumi wa ukombozi unavyosambaa kwa kasi ya kutisha huko vijijini kwani ukimya wa vyombo kama TBC ni baraka kubwa kwa Dr. Slaa.
Kwa hiyo mkuu kwa sababu tunaangalia uachguzi wa uraisi lazima tuangalie nchi nzima na si majimbo mawili tu. Sawa Busanda na Biharamulo Chadema ili panda na kufikia asilimia 42 but hauja onyesha proof kwamba hii ni trend nchi zima bali ni sawa na kuassume kwa sababu ume faulu mtihani wa biologia basi na geographia nayo lazima utafaulu kutokana na matokeo ya biologia.
Mkuu MwanaFalsafa1, mbegu safari hii imepandwa kwenye udongo wenye rutuba. Kuna watu wameanza kuhaha kikwelikweli na kulingana na ripoti tunayoipata wengine huko makwetu hakuna mteremko tena kwa CCM labda wafanye faulo.
Kwa hiyo mkuu the opportunist in me wants to believe that Watanzania wapo smart enough na watamchagua mgombea aliye bora (i.e.Slaa) but the realist in me does not see that happening. Ni wakati tuna bidi tutambue kwamba mvuto wa mgombea pekee siyo unaoshinda uchaguzi. Party mechanism na planning plays a big part. Siwezi sema chochote kuhusu strategy ya Chadema because I'm not an insider but if they have a well placed game plan na wamejiandaa tokea mwanzo(meaning hata kabla ya sasa) then chances ipo. It's up to Chadema.
MwanaFalsafa1, subiri kampeni rasmi zianze na nakuhakikishia CCM hawajawahi kupata upinzani kama watakaoupata safari hii. Mimi hata sina wasi wasi zaidi ya lile la kukataa matokeo kwa CCM. Tuombe Mungu atupe uzima, wale akinaThomasi itabidi wasubiri hadi waone majeraha na kugusa makovu ndio watakubali, October 31 si mbali.
 
Mwanafalsafa!
I hate to burst your bubble. Umesema hakujawahi kutokea wizi wa kura Tz bara. You are wrong. 1995 Mrema alishinda kwa 60% ushindi ukabadilishwa kwa shinikizo ya usalama wa taifa. It has happened on the mainland, it could happen again.
 
Mwanafalsafa!
I hate to burst your bubble. Umesema hakujawahi kutokea wizi wa kura Tz bara. You are wrong. 1995 Mrema alishinda kwa 60% ushindi ukabadilishwa kwa shinikizo ya usalama wa taifa. It has happened on the mainland, it could happen again.

Hmmm Jasusi acha kamba bana. Siamini hata kidogo kuwa Mrema alishinda let alone kushinda kwa asilimia 60.

Una ushahidi gani kuthibitisha hayo unayosema?

Ukiniambia Seif Sharriff Hamad alishinda Zanzibar nitakubali maana tume ya uchaguzi ilichelewesha matokeo na baadaye kuja kutoa matokeo ya kupikwa ambapo Komandoo ndio akatangazwa mshindi kwa asilimia chini ya moja kama sikosei. Katika mazingira yetu haya ushindi mwembamba kama wa Salmin Amour ni ushahidi tosha kuwa matokeo yalipikwa.

Lakini hiyo ya Mrema.....
 
Hilo nalo neno mkuu. Miaka kadhaa iliyo pita kuna mtu fulani influencial kutoka Afrika ali hojiwa na CNN au BBC. Aka sema Afrika kwa mtazamo wa vyama vya upinzani ni kwamba uchaguzi si huru na haki mpaka upinzani ushinde. Kwa maana chama tawala kikishinda tu basi uchaguzi haukuwa wa huru na haki. Africa bado demokrasia ni barabara yenye njia moja.
Mkuu unajuwa kuwa hamasa na msisiko wa kisiasa hapa JF kwa kiwango fulani ni mkubwa, lakini je vipi wale wengi ambao wanaishi vijijini kusiko na mitandao au websites je wanafikiwa na hizi hamasa!?
 
Nadhani zamani ilikuwa ni rahisi kuiba kura au kung'ang'ania madaraka ila kadri siku zilivyokwenda, Kikwete atakuwa anatembea juu ya kamba kujaribu kung'ang'ania madarakani iwapo kura zitaonyesha kuwa alishindwa. Atajijengea nafasi kama ya Nyerere katika historia ya Tanzania iwapo atakubali kukabidhi madaraka kwa mshindi kwa njia ya amani bila kusubiri watu wakwaruzane kama ilivyotokea huko Kenya na Zimbabwe.
 
Hmmm Jasusi acha kamba bana. Siamini hata kidogo kuwa Mrema alishinda let alone kushinda kwa asilimia 60.

Una ushahidi gani kuthibitisha hayo unayosema?

Ukiniambia Seif Sharriff Hamad alishinda Zanzibar nitakubali maana tume ya uchaguzi ilichelewesha matokeo na baadaye kuja kutoa matokeo ya kupikwa ambapo Komandoo ndio akatangazwa mshindi kwa asilimia chini ya moja kama sikosei. Katika mazingira yetu haya ushindi mwembamba kama wa Salmin Amour ni ushahidi tosha kuwa matokeo yalipikwa.

Lakini hiyo ya Mrema.....
Nyani,
I am willing to put my reputation on the line. I cannot reveal my sources but ni kweli.
 
Nyani,
I am willing to put my reputation on the line. I cannot reveal my sources but ni kweli.
Eeh! Mbona hakushika nafasi hata ya pili kwenye huo uchaguzi, kulikoni?
 
Nyani,
I am willing to put my reputation on the line. I cannot reveal my sources but ni kweli.

You are contradicting yourself! If you are "willing to put" your "reputation on the line" then you should reveal your sources. Otherwise, you are not willing to put it on the line.
 
There are those who lose before they even start. CHADEMA can win. CCM can be beaten. This is not naiveté. The conditions are ripe for a change of rulers in Tanzania. Many thought that KANU and UNIP could not be beaten but they were.

Tanzanians are not as stupid as Kiranga wishes to believe. They know that we have had only one group of rulers for 50 years and that this has led to abject poverty. They know that it would be disastrous to celebrate our Golden Jubilee under the leadership of the same group of failed leaders.

There is also the influence of neighbours. These have had a second phase of government, and the results are good. We in Tanzania have had only one phase, the CCM phase. We want a second phase. A better phase.

Do not underestimate Tanzanians. They know that they cannot elect the same people over and over again and expect a different result.

The only thing that is constant in today's world is change. Tanzanians cannot be expected to constantly re-elect CCM.
 
Asante kwa maelezo yako ambayo kwa namna fulani yanapingana na dai lako la awali

Kitu cha kwanza kabisa nilichotaka kuweka wazi ni kwamba maelezo yangu hayapingani. Ndiyo maana nikaanza kusema kwamba Kikwete kashapitishwa na CCM, na Tanzania hairuhusu mgombea binafsi, kwa hiyo unless unaongelea hyperbolics za dunia ya kufikirika zilizo nje ya context ya uchaguzi wetu huu, mtu akimuongelea mgombea Kikwete anamuongelea Kikwete mgombea wa CCM na wala si wa CHADEMA, au mgombea binafsi Kikwete. Mimi siko interested na hypothetical hyperbolics za alternate universe na alternate futures, nikitaka kuburudishwa na hyperbolics hizi natafuta tungo za Arthuc C. Clarke, Isac Asimov, Carl Sagan, Herbert G. Wells au hata Douglass Adams katika tamthiliya zao za "Science Fiction". Kwenye ku deal na ukweli unaoendelea nadeal na ukweli.


kwani kwanza.
?
Uzito wa dai la kushinda kihalali unapungua kwani unasisitiza jinsi ilivyo vigumu kuiondoa CCM madarakani kwa sababu wao ndio wanaamua nani awe Raisi wa nchi hii na siyo wananchi per se !

CCM washampitisha Kikwete, what's your point ? Mimi sikusema Kikwete ana ujanja uchawi wa kuwaroga Watanzania wampigie kura yeye bila kujali chama.Sielewi unapata wapi hisia kwamba ninavyomuongelea Kikwete namuongelea nje ya siasa za vyama. Tanzania hamna elective politics bila vyama, sasa sijui hii notion ya Kikwete anayeelea hewani bila ya kuwa na chama unaitoa wapi.

Hapa ni kama vile unakubaliana na mleta mada kuwa pamoja na wananchi kuamua tofauti,

Wananchi wetu hawana utamaduni wa kuamua tofauti, ni 1985 tu wametoka kuimbishwa "Ally Mwinyi, Ally Mwinyi, NDIYO NDIYO NDIYO". Mpaka leo Nyerere ni kama mungumtu pamoja na maovu yote aliyoyafanya (not that hakutenda mema). Mpaka leo badala ya watu kuangalia tutaleta uongozi bor, bado wanalila lia na "hero worship", wanamlilia Nyerere afufuke aje atuongoze, wasomi hao.Worse still hata upinzani wenyewe bado upo katika "hero worship" hiyo hiyo. Watu pekee mwenye uwezo wa kumsema Nyerere bila haya ni Mtikila na Wazanzibari fulani. Mpaka mara nyingine mtu unaona huyu Nyerere sasa anatumika kama mtaji wa kisiasa.Huyu Nyerere si ndiye yule yule alikuwa anakandya vyama vya upinzani huyu? Huyu Nyerere si ndiye aliyefanikisha wizi wa kura wa kumnyang'anya Seif Sharif urais wa Zanzibar huyu? Mbona wapinzani wanamuogopa hata baada ya kufa? Au ndiyo nidhamu ya woga isiyotaka kuwasema vibaya wafu, hata kama ni kina Iddi Amini ?

Kwa hiyo usijidanganye kwamba wananchi watafanya tofauti, kuna sehemu huko watu hawajui kwamba Nyerer amefariki si rais. Wengine washamsikia Nyerere miaka kibao wanafikiri kile cheo cha urais ndiyo Unyerere, ukiongea nao ukiwaambia Nyerere alifariki wanakuuliza Nyerere wetu sasa hivi nani ?

Wananchi kuamua tofauti, tofauti my foot, tofauti yenyewe iko wapi? Hivi vimikoa viwili vitatu urbanite ?

[UOTE]utamaduni wetu wa kufuatisha strongmen unaweza kumpa kiburi Kikwete (CCM) asikubali matokeo tofauti na akawa kama Mugabe. [/QUOTE]

No, you got it backwards. Ukiwa strongman Africa mara nyingine unakuwa so powerful kiasi hata huhitaji kuiba kura.Kwa sababu una control communication, una control education, una control largesse.Kila kazi muhimu inatokana na uteuzi wa rais.Kuanzia majaji (judiciary) mpaka wabunge wa kuteuliwa (legislature, in fact rais mwenyewe ni sehemu ya bunge) cabinet (executive) wakuu wa mashirika ya umma (technocrats, administrators, aristocrats) huyo huyo rais ndiye mwenyekiti wa chama (party politics) na amiri jeshi mkuu (armed forces) anateua gavana wa benki kuu na hata mabalozi (diplomatic corps). Anachagua mpaka mwenyekiti wa tume ya uchaguzi (electoral process).Sasa unategemea mtu kama huyo atashindwa vipi kuwa na unfair influence kiasi cha kutohitaji kuiba kura ?

Hivyo kutoafiki na dai lako la awali liko pale kwamba je, kwa mtu (chama) kama huyo, hiyo confidence ya kushinda kihalali inatoka wapi kama si ukweli kuwa wananchi hata wafanye nini watalazimika kumchagua tu yeye kuwa Raisi ?

Inategemea na maana yako ya neno "halali" ni nini. Kama unamaanisha uhalali wa kutoiba kura (ambao ndio tuliokuwa tunauzungumzia hapa originally) then utaona kwamba Kikwete atashinda kihalali kwa sababu ana kila nguvu ya kufanya hivyo. Ni kama umpiganishe Tyson alipokuwa katika prime yake na kijana mchanga.

Lakini kama unasema kumpiganisha Tyson in his prime na kijana mchanga, asiye wa uzito wa Tyson wala uzoefu wake, ambaye sio professional boxer na wala hana access ya chakula na mazoezi ya Tyson, ukasema kuwapambanisha si halali, then utakuwa sawa.

Kama una object playing field haiko level, team ya Kikwete iko kilimani inasaidiwa na gravity na timu za upinzani ziko chini zina fight an uphill battle, then naweza kukubaliana na wewe, kwamba tumpunguzie rais madaraka yake ya kuteua kila mtu, tubadili katiba etc etc.Lakini hili si swali tulilokuwa tunahjadili hapa.

Tunaongelea mtu ambaye ameshindwa katika kura, na sasa anaamua kung'ang'ania Ikulu na kutaka kubadilisha matokeo.Ndiyo mimi nikasema Kikwete hawezi hata kufikia point ya kutaka kubadili matokeo, atatakaje kubadili matokeo wakati kiwanja chenyewe hakiko level na yeye yuko juu wakati wapinzani wako chini? Ni obvious ukitumia kiwanja hiki atashinda mechi.
 
Nadhani zamani ilikuwa ni rahisi kuiba kura au kung'ang'ania madaraka ila kadri siku zilivyokwenda, Kikwete atakuwa anatembea juu ya kamba kujaribu kung'ang'ania madarakani iwapo kura zitaonyesha kuwa alishindwa. Atajijengea nafasi kama ya Nyerere katika historia ya Tanzania iwapo atakubali kukabidhi madaraka kwa mshindi kwa njia ya amani bila kusubiri watu wakwaruzane kama ilivyotokea huko Kenya na Zimbabwe.

Kichuguu you nailed it.Watu wanafikiri kuiba mmatokeo ni rahisi tu.

Wewe unafikiri kwa nini CCM wamekubali muafaka Zanzibar, CCM na uchu wao wote wa kuhodhi madaraka na uhasama wote uliokuwa Zanzibar.

Wameona kila siku zinavyozidi, kila wanavyoiba, ndiyo mbinu zao zinavyojulikana. Wakaona sasa hapa siku CUF watashinda, tutashindwa kuiba, tutakuwa nje ya serikali kabisa. Bora tuingie muafaka ni insurance policy, wakishinda CUF at least tutakuwamo katika serikali ya mseto.

Kuiba kura si rahisi hivyo.
 
There are those who lose before they even start. CHADEMA can win. CCM can be beaten. This is not naiveté. The conditions are ripe for a change of rulers in Tanzania. Many thought that KANU and UNIP could not be beaten but they were.

Tanzanians are not as stupid as Kiranga wishes to believe. They know that we have had only one group of rulers for 50 years and that this has led to abject poverty. They know that it would be disastrous to celebrate our Golden Jubilee under the leadership of the same group of failed leaders.

There is also the influence of neighbours. These have had a second phase of government, and the results are good. We in Tanzania have had only one phase, the CCM phase. We want a second phase. A better phase.

Do not underestimate Tanzanians. They know that they cannot elect the same people over and over again and expect a different result.

The only thing that is constant in today's world is change. Tanzanians cannot be expected to constantly re-elect CCM.

I say this will be a gradual process and it will take time.The opposition has to narrow the margin first. Ni vigumu sana katika mazingira ya Tanzania ya sasa Kikwete kupoteza urais, amepata asilimia ngapi last time 80? kwa maana hiyo hata akipoteza asilimia 30 za uongozi wake katika kura bado atakuwa na 50%. Na Tanzania politics zetu all you have to do to maintain support is not shoot somebody in broad daylight like Ditto, and even then some people may still excuse you (seeing how some people are excusing Shyrose Bhanji) .Na Kikwete akiweka kismile chake kile basi watu hawana hiyana naye, half the population don't know what went down with EPA and the biggest scandals.

Kwa hiyo urais mwaka huu sahau mwalimu, kampeni hizi ni za kuelekea 2015 (ambako kuna chances kubwa kwa sababu rais mpya atakuja as far as we know).

Otherwise you can put your money where your mouth is, hapa hapa JF. I hate to sound like I am rooting for JK, I am not.Lakini ukweli wenyewe ni kwamba atashinda, ninachoangalia ni kwa asilimia ngapi.

Kama vipi let's revisit this thread after the election.

And of course I guarantee you there are going to be some "foul play" cries.
 
You lack HOPE, Dear Kiranga. Kama kila mtu akikata tamaa hivyo itakuwaje? You argue that he won by a huge margin last time and therefore he will win agin. Non sequitur. I does not follow. Hakuna wabunge walioshinda kwa asilimia kubwa hapo nyuma na sasa hawapiti hata kwenye primaries?

Kuhusu wizi wa kura, nikukumbushe kesi dhidi ya ushindi wa Ubunge wa Slaa. Unaikumbuka? Ulitolewa ushahidi mahakamani kwamba viongozi wa CCM walipita wakibadilisha matokeo ya kura zilizohesabiwa. Yaani idadi kama ya kura 170 kwenye kituo inabadilshwa kuwa 1700. Ndio maana kwenye vituo vingine idadi ya kura za CCM huzidi hata idadi ya waliojiandikisha.

CCM haikuiba kura Zanzibar? Inafanya hivyo karibu chaguzi zote. Uliza mitaani, utaambiwa watu walivyoona wenyewe masanduku yakitoroshwa na kujazwa kura za mgombea.
 
Mkuu unajuwa kuwa hamasa na msisiko wa kisiasa hapa JF kwa kiwango fulani ni mkubwa, lakini je vipi wale wengi ambao wanaishi vijijini kusiko na mitandao au websites je wanafikiwa na hizi hamasa!?

Huu ni ukweli ndio maana kuna mheshimiwa mmoja alisema wanashukuru sana mtandao wa internet umewafikia wachache, alitamba kuwa ja JF hayawafikii wapiga kura wao kwa hiyo wataendelea kupeta.
 
Imani yangu ni kwamba Dr.Slaa ataleta ushindani mkubwa sana ambao haujawahi kutokea. Sidhani kama anaweza kumshinda Kikwete kirahisi isipokuwa uwezekano upo japo mdogo kulingana na siasa za Bongo. Kura kuibiwa wala hilo halina Ubishi, CCM will do anything possible hata ikibidi kutumia nguvu ya dola kuhakikisha Ushindi wao lakini mwaka huu ndio mwaka wa mageuzi na sio 2015.

Kuingia kwa DR. Slaa kutakiwezesha Chadema kupata viti vingi Bungeni hilo ni wazi labda tu Chadema washindwe kujiuza wakitumia CHUKI ya wananchi kwa CCM ili kuhamasisha nguvu ya ushindi. Na hakika Dr. Slaa ataweza tu kumshinda Kikwete kama atatumia vizuri muda wake kuonyesha kwamba yeye ndiye tumaini ambalo wananchi walilokuwa wakisubiri, kama alivyoweza Morgan Tsvangirai kuwashawishi dunia nzima mabaya ya Mugabe. Hivyo basi sioni sababu Dr.Slaa ashindwe ikiwa sababu anayo, nia anayo na uwezo anao!..
Yatakayo ajili baada ya Uchaguzi - Mungu pekee ndio anajua! Lakini I think, This is it (Michael Jacksoin)
 
Kichuguu you nailed it.Watu wanafikiri kuiba mmatokeo ni rahisi tu.

Wewe unafikiri kwa nini CCM wamekubali muafaka Zanzibar, CCM na uchu wao wote wa kuhodhi madaraka na uhasama wote uliokuwa Zanzibar.

Wameona kila siku zinavyozidi, kila wanavyoiba, ndiyo mbinu zao zinavyojulikana. Wakaona sasa hapa siku CUF watashinda, tutashindwa kuiba, tutakuwa nje ya serikali kabisa. Bora tuingie muafaka ni insurance policy, wakishinda CUF at least tutakuwamo katika serikali ya mseto.

Kuiba kura si rahisi hivyo.

Mkuu kwa Tanzania hata sasa bado mambo ni easy tu. Simu moja inaweza kubadilisha matokeo na wananchi wakakaa kimya, bado wengi wetu tumelala. Mfano mzuri ni EPA, wezi wapo wanajulikana lakini mpaka leo wanapeta tena hao hao tumewachagua kwenye kura za maoni kuwa wagombea ubunge kwa chama chetu. It is so easy kuwadanganya watanzania waliowengi kwa kuwa wengi bado hawana uelewa wa nini kinachoendelea. This time CUF walikuwa wamefikia braking point, wanajua kuwa wakiibiwa mara ya tatu ni lazima pachimbike, ndio maana wameogopa kuiba kura.

Huku bara it happens every now and then, and it will keep on happning until wote tukiwa kama watu wa tarime au Zanzibar.
 
Back
Top Bottom