Je, kinadharia inawezekana kila mtu duniani akawa tajiri?

Je, kinadharia inawezekana kila mtu duniani akawa tajiri?

Kutosha nini? Maana kinachokutosha wewe mwengine hakimtoshi

mAHITAJI YAKO YANAYO KUZUNGUKAA

NB:KWA RENKI YA KIDUNIA UKIWA NA TRILLIONI MBILI UNAWEZA UKAISHI MAISHA YAKO YOOOTE (HIGH STANDARD LIFE)BILA KUFANYA CHOCHOTE MPAKA UKAFA.HUO NDO UTAJIRI NAO UZUNGUMZIA MKUU
 
Wanajamvi, Kwanza napenda kumshukuru Mungu kwa nafasi hii aliyonipa ya uhai na afya tele kuweza kuleta swali hili kwenu.
Swali langu haliongelei kama inawezekana kila mtu akawa tajiri 'kiutendaji', la hasha. Bali je, logic inakubali kwa watu wote duniani kuwa matajiri bila kuacha masikini hata mmoja? au kwa wengine kuwa matajiri ni lazima kuwe na wahanga? (masikini)?
Nawasilisha.

Hii ni ngumu kwasababu binadamu tunatofautiana namna ya kufikiri na hata kufanya mambo...

Kama hali ya kutafakari na kufikiri ingekuwa sawa hili lingewezekana lakini nadhani ingesumbua kwasababu tungekuwa na mambo yanayofanana,tusichokijua ni kuwa huu utofauti uliopo ndio unafanya maisha yawe matam kwa asili yake...
 
Mi nadhan wengine ni lazima wawe maskini ! Hata nikirefer Bibble Mathayo kuna sehemu alisema Heri wale masikini duniani maana mbinguni wataiona raha ya milele. Pia ukiangalia mfano wa Tajiri na Lazaro! so gepu la maskini na tajili halikwepeki.
 
Kama utajiri unao uzungumzia ni kuwa na mali nyingi, kwa hali ya kawaida haiwezekani watu wote kuwa matajiri. Sababu kila binadamu ameumbwa tofauti kuanzia kiakili hadi kiutendaji. Kuna wengine ni vichaa, walemavu, wavivu, waoga, n.k. Hata kama kinadharia ingekua hela zinaokotwa alfajiri ya saa 11.00, bado kuna wengine wangechelewa na hivyo wangekosa kuwa na pesa nyingi. Pia, kumbuka binadamu tunategemeana ili maisha yaende, hivyo kuna wengine hawataki kuwaona wenzao wamefanikiwa, wanavinyongo! Kwani definition ya utajiri ni ipi unayoizungumzia kwa muktadha huu?
 
Umasikini upi unazumgumzia❔➖WA roho au mwili❔
 
Mkuu i think inategemea unamaanisha nini unavozungumzia neno "umaskini" kama umaskini unamaanisha mtu kukosa basic needs kama msosi na nguo na sehemu ya kuishi basi inawezekana kila mtu kuwa tajiri.

Kuna report ilikua published kwa worldbank inasema 95% ya watu wamejazana katika 10% ya ardhi yote iliyopo duniani, hii inamaanisha hiyo 90% ya ardhi imejaa vitu ka wanyama, misitu, barabara, na sehemu chache pia jangwa, so kama ni sehemu ya kujenga nyumba hilo hata usiulize, zipo kibao zimejaa, kama ni sehemu za kulima zimejaa vilevile, malighafi nazo same thing.

Vitu ka mafuta wanayotoa baharini, bahari inachukua zaidi ya 70% ya dunia na sehemu yote hiyo binadamu tushawahi kuona 5% ya bahari peke yake, so malighafi tunazotoa baharini jua tumetoa kwenye hiyo 5%, je 95% ambayo hatujawahi tembelea itakua na nini? Lazima kuna viumbe na malighafi kibao tu ambazo tunaweza tumia.

Vitu kama umeme, ni uvivu tu wa binadamu na kukosa ushirikiano, theoretically kujaza solar panels jangwa la sahara zinaweza kutupa umeme wa kutosha dunia nzima kwa miaka sio chini ya 20 kabla ya kubadilisha panels.

Sema sasa tukija in reality, capitalism, kitu pesa kila mtu anakomaa kuzivuta kwake kadri awezavyo, hata kama ni kubomoa nyumba za watu, kufunga watu, people don't care, kufanya watu wawe slaves etc, na ni moja ya vitu vinavyochangia vitu kama weapons manufacturing, sababu kama weapons zingekua hazilipi vya kutosha makampuni yasingejitokeza kutengeneza very advanced weapons, kwa style hii lazima baadhi ya watu waumie tu, haitotokea siku hata moja kuwe na balance sababu system nzima inaoperate kwa principle ya moja ata-gain profit moja ata-lose hamna swala la kusema nchi zote zitashirikiana kutengeneza kitu flani ku-end world hunger, coz kila mtu yuko busy kujaribu kuvuta pesa kwake hamna muda wa kufikiria kuhandle matatizo ya binadamu wengine.

bro umetema madini tupuu,,yani ubinafsi ndo tatizo kubwa ila kila mtu hapa dunian anaweza kuwa tajiri,,ila karma nayo inachangia kuwepo kwa madaraja mana haya maisha ni cycling process
 
Habari Mwanzilishi wa Mada. Nashukuru kwa aliyenitag katika mada hii kwani naamini anapenda kuona mchango wa watu mbalimbali na mimi nikiwemo katika kuelezea hii mada.

Kwa uelewa wangu na kwa jinsi nilivyosoma mada yako Naamini umezungumzia hasa utajiri wa Mali (Physical Things). Je ni kweli kwamba kila mwanadamu anaweza kuwa tajiri?

Kuna dhana mbalimbali watu wanazo juu ya utajiri lakini ninaweza kuelezea kwa kina kuhusiana na hilo.

Kwanza kabisa ni vyema kufahamu nini lengo la Maisha, Lengo la maisha ni kuwa na furaha. Kila mwanadamu anapenda kuwa na furaha. Kila kitendo tunachokifanya, shughuli tunayofanya na nia tunayoweka katika shughuli zetu ni kutafuta furaha. Unaweza ukawa hujaona kuwa furaha ndio mzizi lakini ni kweli, furaha ni mzizi mkuu na ni tegemei la mwisho kwa kila hatua. Unafanya kazi ili familia yako, marafiki, watu wako wa muhimu na wewe mwenyewe upate furaha na amani. Unaweza ukawa unasoma kwa lengo la maisha mazuri hapo baadaye, lakini bado maisha yayo mazuri ni kwa lengo la furaha hapo baadaye, unajituma na kuhakikisha unapata kipato ili kutimiza mahitaji yako, na mahitaji hayo ni chanzo au chemichemi ya furaha kwako. Hivyo kila hatua ya mwisho ni kuwa na furaha.

Je furaha inapatikanaje? Je furaha inapatikana tu kwa kuwa na mali, umaarufu, na vitu vingi? Je ukipewa kila kitu unachokitaka kama ni mke mzuri, mali za kununua utakacho, na umaarufu je utapata furaha? Je kila mwenye vyote ana furaha? Utagundua pia kwa upande mwingine hata mwenye kila mali, umaarufu, na utajiri hana furaha yote asilimia mia. Bado atajitahidi kulinda anaowapenda kama ni mke na watoto, bado atajitahidi kumaintain utajiri wake, bado atahitaji kujilisha na wanyang'anyi, bado anakufa, atazeeka na bado hawezi kudhibiti kufa na kuzeeka kwa anaowapenda. Pia bado akifa anaacha vyote hivyo alivyojitahidi kuvikusanya, je lengo la maisha ni nini hasa? Lengo la maisha ni kuitafuta furaha ya kweli, isiyoisha, isiyoibwa na wanyang'anyi na furaha ambayo haishikiliwi na vitu vya muda. Maisha ukiyachunguza yanatupa mafunzo kuwa vingi tunavyoviona ni vya muhimu havina umuhimu milele na pia kila mwanadamu anateseka (kutoridhika na hali).

Nature ya mwanadamu ni kutoridhika, utapenda kuwa ni hichi utakipata lakini bado utapenda kuwa na kingine utakipata lakini bado utapenda kuwa na kile, hakuna unachokipata kama mali na umaarufu na kuridhika daima. Pia mbali na kutoridhika nature ya akili ni kutamani. Akili ni kama samaki anayetapatapa, inatamani hiki na kile na kile na kile na kukujengea hamu. Hamu haikamiliki kwa nje bali inakamilika moyoni na sio akilini.

Hata kila mwanadamu akiwa na mali na kila kitu bado hatutaweza kuishi kwa amani. Bado tutahitaji mfano upendo, kujitambua, hekima, adabu na busara.

Mafanikio yanakuja pale unapokamilisha safari ya nafsi, Mfano mzuri ni speech ya Steve Jobs, alisema kila mwanadamu anapaswa kufahamu ni kwanini yupo leo hii ulimwenguni, na ukifahamu lengo la maisha yako na kulifuata utasaidia nafsi za wanadamu wengine ambazo zinahitaji kujitambua na utakuwa mwanga kwao wenye giza. Badala ya kufikiria nitakuwa na mali kiasi gani nifurahi fikiria nitafanya nini katika maisha yangu kuangaza wanadamu wengine. Leo tunafahamu kuna aliyeanzisha umeme, aliyegundua computer, aliyebuni kitu fulani, aliyetumia maisha yake kutoa huduma yake kwa wanadamu, na kadhalika wote hawa hawasahauliki. Kwa kutenda lengo lako la maisha, rehema na baraka hukujia na mafanikio yako huongezeka.

Hebu jiulize kwanini watu matajiri wa dunia bado wanajituma, wanajitahidi kuendeleza shughuli zao badala ya kukaa na kutumia mali zao tu? Kwa sababu lengo lao la maisha sio kujilimbikizia mali, wanafahamu kuwa furaha haiji kwa mali bali kwa kuridhika na hali na kuishi katika unachokipenda na ambacho ni lengo lako la maisha. Na kupitia wao wengine huona mwanga na kuamka.

Weka mali ambayo haina mwisho, ambayo hakuna mtu anayeweza kukuibia wala kukudhulumu. Kumbuka sisi ni sehemu ya Aliye Mkubwa, mali haiwezi kukununua wala hakuna dhamani inayoweza kulingana na wewe. Fahamu lengo lako la maisha na maisha yatajipanga kutimiza lengo lako. Tangu mamilioni ya miaka na miaka dunia imetumia muda kutokea kama ilivyo leo, kwanini wewe upo leo hii, ni bahati kubwa kuzaliwa mwanadamu, ni bahati kubwa kuwa Ufahamu unaoishi. Unautajiri mkubwa ndani kuliko utajiri wa nje.

Mali na umaarufu sio chanzo cha furaha na ndio maana haiwezekani duniani kila mtu akawa tajiri. Maisha yamefanya hivyo kutufunza kuwa kuna utajiri mkubwa zaidi ya mali.

nakuelewa sana kaka,,i salute u
 
Utajiri unaouzungumzia ni kiasi gani?
Kuna waoona wakiwa na mil 100 ni matajiri na wengine wakiwa na bil 10 wanajiona middle class.
Utajiri unausemea ni upi? Kwa kiwango gani?
 
Madaraja katika jamii hayawezi kupotea kwa namna yeyote
Hivyo haiwezi kutokea dunia nzima wote tukawa matajiri, hata katika kufikilia tu!
Kinachoweza kutokea ni watu katika dunia kukua kimaendeleo katika ujumla wao.
 
Wanajamvi, Kwanza napenda kumshukuru Mungu kwa nafasi hii aliyonipa ya uhai na afya tele kuweza kuleta swali hili kwenu.
Swali langu haliongelei kama inawezekana kila mtu akawa tajiri 'kiutendaji', la hasha. Bali je, logic inakubali kwa watu wote duniani kuwa matajiri bila kuacha masikini hata mmoja? au kwa wengine kuwa matajiri ni lazima kuwe na wahanga? (masikini)?
Nawasilisha.

At one point, everybody was rich.
 
Watu mnazunguka sana na kulikuza swali.
Kumbe na wewe umeona mkuu...Mtoa mada ni hv,hilo haliwezekani na kama lingewezkana wewe usingeweza kuzama humu jf kwasbb mzungu asingehangaika akutengnezee simu/computer uliongilia jf wakt tayar ana mihela kibao..Hili swala la kila mtu awe tajiri hata mungu hakuthubutu litokee na hata serikali yoyte dunian haiwez kuthubutu kila raia wake awe bilionea...yan kuna madhara makubwa sn na huenda hata kula yako ingekuwa shida tupu na ungetembea uchi japo bilionea..nani akutngnezee nguo? Nani akulimie chakula...hujaelewa bado?
 
kwa uelewa wangu ni vigumu kwa kila mtu kua tajiri kwa kila kitu, ili kue na balance nzuri katika maisha ni lazima kuwe na pande mbili, yaani upande wa wasio na utajiri na upande wa wenye utajiri, ili huo utajiri uonekane ni wa maana ni lazima kuwepo na watu walioukosa, hivyo watalazimika kuutafuta kutoka kwa wale walionao, ili maisha yaendelee lazima kuwe na kutegemeana. mfano ni lazima kuwe na wabeba mizigo, wakulima, wanunuzi wa mazao ya wakulima n.k. kila kitu kikipatikana kwa wingi na kila mtu akiwa nacho, dhamani ya kitu hicho hushuka(paradox of value) ndio maana maji ni ya muhimu sana kuliko dhahabu lakini bado maji yanauzwa bei ya chini na dhahabu inauzwa bei kubwa kwa sababu inapatikana kwa shida. hivyo kama kila mtu angekua na fedha au kila kitu anachohitaji, maisha yangekua magumu, nani angefanya kazi ngumu? nani angekubali kuishi kijijini? nani angemuheshimu mwingine?
 
Umasikini ni state of mind.
Kuwa watu muda wote wanawaza kuuza walivyonavyo au kutumia hadi viishe
Wengine wanawaza kuzalisha na kuongeza vipato.

Utafiti usio rasmi unaonyesha, Leo kama utachukua pesa zote dunia nzima ukawagawia watu wote sawasawa.
Mwisho Wa siku zitarudi kwa walewale walikuwa nazo mwanzo.
 
Watu wote hawawezi kuwa tajiri lazma kuwe na balance .imagine kila mtu angekuw tajir nani angefny kaz kw mwenzie?!nani angekaa shamban alime?!mifano ipo mingi ila wote tungekuw matajir dunia isingeendelea
 
Back
Top Bottom