Je, kiusalama, kuvaa vest ya kuzuia risasi, na kuacha kichwa, ambayo ni sehemu hatari zaidi, ikiwa wazi, mtu anakuwa amejilinda?

Una macho lakini huoni.
Anapunguza eneo la kulengwa na kuongeza uwezekano wa kukoswa.
 
Dunia hii ina wagonjwa wengi wa akili kuliko watu wazima.

Swsli lako ni zuri sana na lina logic. Unavaaje bulet amour kukinga kifua ukiamini moyo uneulinda huku ukiacha fuvu wazi....

Mkuu elewa tunaishi na wagonjwa
 
wachana na movies na games mzee ...headshot sio poa, NGUMU! hata hivyo nitakupa sababu, iko hivi siku zote sehemu zinazoboreshwa ni zile ambazo katika uhalisia ndizo mara nyingi huonekana kuathirika, mfano walio pigwa risasi wengi duniani walipigwa sehemu za kifua na tumbo na sio kichwa,ingawa ukila ya kichwa ni AKHERA MOJA KWA MOJA,lakini pia hata ndege,vifaru ama meli zikienda battlefield zikirudi/ama zikiharibika basi huangaliwa wapi zimepigwa sana/kuathirika na hapo ndipo wanapo dili napo kupawekea kinga sana, same as human 😅 bai ze wei jana nimeona video ya KOMANDO WA KIZAYUNI AKIJARIBU KUFANYIA KAZI MAZOEZI HALISI YA HEADSHOT AKIUA MTOTO WA KIPALESTINA....na akimkosa mwingine WAZI KABISA...! 🙂

NB:-masilaha ya kizazi hiki hata ukae ndani ya suti ya chuma UNAKUFA TU
 
Rejea shambulio la Lissu la 2017 kule Dodoma, hakuna hata risasi moja iliyolenga kichwa. Ukichunguza mostly wale professional snipers ndiyo huwa wanalenga kichwa, kichwa si easy target hivyo bulletproof vest ni kupunguza tu kwa asilimia fulani madhara ya shambulio la risasi.
Wale vilaza wa TISS walivyomshambulia Lissu ingelikuwa ni 'real professional assassins' risasi moja tu ya kichwa ingetosha kumaliza uhai na kukamilisha unyama wao.
 
 
Kwenye mapigano ya kawaida yaani random kupiga kichwa ni nadra kiwiliwili ndio kinapigwa kwa urahisi. In case wakijua kuna sniper wanavaa helmet ya chuma kupunguza target.
 
...Helmet haizuii Risasi !
 
Kumbe JF bado kuna watu wajinga kiasi hiki?
 
Mtu aliyepigwa risasi ya kichwa mara kadhaa wengi uwa hawafi mfano mzuri ni wale watu wenye jicho moja(chongo) wengine uwa ni majeraha ya risasi,si sehemu zote za kichwa zaweza kupelekea mtu kufa ila kifuani kuna moyo,maini,mapafu na yote yana upana mkubwa(mnofu)mlengaji hawezi kosa kimojawapo na vyote husababisa kifo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…