Je, kuanguka kwa utawala wa Bashar al-Assad huko Syria ni kushindwa kwa Russia na Iran?

Je, kuanguka kwa utawala wa Bashar al-Assad huko Syria ni kushindwa kwa Russia na Iran?

Kwa Afghanistan nimetolea mfano wa Taliban kuigeuka USA kwa wao kuwa na mlengwa mkali wa kiitikadi ya kidini.
Vivyo hivyo huko Syria USA huwenda akageukwa pia.
Taleban haijaigeuka Marekani. Taleban inafuata matakwa ya Marekani.

Taleban ilikuwa inafuga magaidi, Marekani ikaivamia Afghanistan kuwaondoa Taleban ili wasiendelee kufuga magaidi. Ikiwa uko Afghanistan, US ikaunda military bases kadhaa pale Middle East. Ikapambana na kina al Qaeda ikaua kina Osama bin Laden na kupigana na kina Saddam Hussein.

Ikakaa miaka 20 Taleban wakiwa mafichonj. Ugaidi umeisha, Marekani haina purpose tena ya kukaa Afghanistan ikiwalea ikaondoka. Kwenye kuondoka US haikuielekeza Afghanistan iishije, bali ilisisitiza haitaki kufugwa gaidi wala kuharibu maslahi ya Marekani. Jambo ambalo Taleban wanalishikilia hadi leo.

Kuna siku Marekani ilifanya shambulizi la kuua magaidi ikaua kijana wa Waziri mmojawapo serikali ya Taliban, walitulia.
Bado haijafahamika kama Russia itaondoa Kambi yake Tartus na haijajulikana kama kiongozi atakayeingia atakua na mlengo gani.
Russia inaondoka Tartus naval base na Hmeimin airbase. Pigia mstari hili.
Iran haina hasara yeyote kwasababu Ina uwezo wa kupifikisha silaha Lebanon pasi na kupitia ardhi ya Syria.
Iran ina hasara. Kwa miaka zaidi ya 10 Iran imewekeza na kuikopesha serikali ya Assad zaidi ya dola bilioni 50. Zote zimeyeyuka kwa kuangushwa kwa utawala wa Assad. Iran haiwezi claim deni lake wala kurudisha investments zake wala kupata faida kidiplomasia na kiusalama kwenye axis of evil yake.
Ukumbuke Houthi wanapokea silaha kutoka Iran bila ya mtu wa Kati na Yemen iko mbali sana na Iran.
Houthi wanapokea silaha kwa njia ya maji na nyingi zinakuwa intercepted. Kufuatilia shipment ya majini ni rahisi kuliko ya ardhini. Kule Syria hata underground unaweza, hata kwa kutumia Kirikuu au canter unaweza. Sasa navigation ya kutoa shehena Iran hadi Yemen inatumia chombo kikubwa kidogo ambacho kitajulikana kirahisi.

Pia Yemen haipakani na Israel. Syria inapakana na Israel na vilevile Lebanon ambayo nayo inapakana na Israel. Sasa Yemen wale Houthi mpaka warushe makombora yapite anga la nchi adui yao ndio yafike Israel.
Kwa Israel ni hasara kama Syria itageuka kuwa kama Iraq.
Hiyo Iraq yenyewe haina hasara kwa Israel kama ilivyokuwa enzi za Saddam. Syria ikiwa kama Iraq basi ni vyema kwa Israel.

Na Syria wakilazimisha vita Israel kiurahisi kabisa unajiongezea mipaka inajimegea Quneitra. Wasijaribu huo mtego.
Ufahamu kuwa ndani ya Iraq kuna makundi ambayo yameshiriki kuisaidia Hamas mkuu.
Na ndani ya Iraq USA imeshashambuliwa mara kadhaa na washika silaha.
Yote hii ni kuwa tangu utawala wa Saddam uanguke basi Iraq ikawa pro-Iran.
Ngojea tuone huyo kiongozi atayekuja atakuaje.
Hilo ndilo la kutizamwa.
Iraq ya Saddam ilikuwa na jaribio la nyuklia, ilikuwa na Scud missiles, ilikuwa na fighter jets. Iraq ilikuwa na bajeti ya kununua silaha kali za kisasa. Iraq ya Saddam ilikuwa na uwezo wa kufanya mobilization hata ya wanajeshi zaidi ya 300,000 kupigana na Israel au basi Saddam mwenyewe alikuwa na uwezo wa kutoa billions of dollars kwa wanamgambo wapigane na Israel.

Sasa hawa njaa kali wenye viroketi vichache na wapiganaji elfu kadhaa wanakuwaje tishio kwa Israel kuliko Iraq ya Saddam?
 
Hawakushindwa bali waliona Syria army haiana mpango wa kupigana ni kama wamechoka pia .we mtu baki upambane wakati wenye nchi yao wana wakimbia waendesha boda boda
Watu walitaka Iran na Russia wapigane kwa niaba ya wasiria maana wao wenyewe walikuwa hawpigani ulitaka wafanyeje jamani
 
Mnaosema Urusi na Iran wamshindwa Syria mtakuwa hamuelewi mambo yalivyo.

Syria population ni 75% Sunni Majority. Bashar Al Asad alikuwa ni ni Shia ndo maana Iran alikuwa anam support.

Ukifanya mahesabu unaelewa kwamba hata kama Russia na Iran wangeamua ku support Assad mpaka mwisho ingekuwa ni blood war na ni likely washia wangeshindwa, alichofanya Bashar itakuwa ni ushauri wa Iran na Russia kwamba hana namna zaidi ya kungoka madarakani because the odds are not on his favor.

Kwahiyo sioni hoja ya kushangilia kwamba Iran na Russia wameshindwa. Kuanguka Assad was inevitable
Hoja kuhusu kushindwa kwa Urusi na Iran pale Syria ni hoja sahihi kabisa.

Urusi na Iran wameshindwa Syria kwa sababu wamepoteza uwanja wao wa siasa za jiografia (geopolitics) ambao ulikuwepo kutokana na uwepo wa mshirika wao madarakani (Bashar al-Assad). Ni kama tu Urusi ilivyopoteza ushawishi wake pale Ukraine baada ya Rais Viktor Yanukovych (mshirika wa Urusi) kuondolewa madarakani mwaka 2014.

Kinachoendela sasa hivi kwenye mgogoro wa Ukraine na Urusi, kwa mfano, ni matokeo ya Urusi kupoteza vita ya geopolitics mwaka 2014.

Katika karne hii, mahusiano ya kisiasa na kijeshi kati ya Urusi na nchi zingine huwa yanaishia kwenye level ya leadership iliyopo katika nchi husika. Population unayosema ama wananchi kwa ujumla huwa hawashirikishwi ipasavyo. Hakuna hiyo mechanism. Kwahiyo, sio jambo la kushangaza kukitokea civil resistance, civil war n.k.
 
Kuanguka kwa Assad ni mbaya kwa wamagharibi kuliko Russia na Iran.
Maana hao Jihadist wakishika madaraka watawageuka hadi USA na Israel waliowalisha na kuwasapoti.
Taliban iliundwa na kusapotiwa na USA at the end ikaigeuka USA kwa itikadi Kali za kidini.
Pia Itakua total chaos hapo Syria.
Israel isijitizame kuwa salama tena.
Kinyago ulichokichonga mwenyewe hakiwezi kukutisha.
 
Kuanguka kwa Assad ni mbaya kwa wamagharibi kuliko Russia na Iran.
Maana hao Jihadist wakishika madaraka watawageuka hadi USA na Israel waliowalisha na kuwasapoti.
Taliban iliundwa na kusapotiwa na USA at the end ikaigeuka USA kwa itikadi Kali za kidini.
Pia Itakua total chaos hapo Syria.
Israel isijitizame kuwa salama tena.
Kinyago ukichonge mwenyewe halafu kikutishe!
 
Kinyago ulichokichonga mwenyewe hakiwezi kukutisha.
Sio kila sehemu huo msemo unatumika.
Refer USA kwa Taliban ilikuaje!?
This is politics kijana watu humbadilisha adui na rafiki kulingana na mahitaji yao.
Hao waasi wakishakamata nchi na wakafanya establishment ya economic and political policies zao hawatowahitaji hao USA wala Israel wala nani.
Ni kama Mujaheddin/Taleban walipomshinda Mrusi 1989 kwa kusaidiwa na UK na USA wali establish sera zao na kuwatema hao USA na UK.
Tena ogopa sana watu wenye mlengwa wa kijihadi.
 
Wakati utatupa jibu sahihi,
Umeangushwa utawala wa kidikteta, sawa.lakini itakuwaje kwa Marekani na Israel ikiwa utawala wa Syria utakaofuata ukiwa na uelekeo wa kiimani (Dini)zaidi!?
Si jambo lakushangaza kwa Marekani na Wamagharibi kuvuruga amani na hata kuwezesha kufanywa mapinduzi kwenye mataifa mengine lakini kinachoshangaza na kustaajabisha ni matokeo yake!
Ikiwa utawala wa Syria utakaofuata utaleta usumbufu na kusababisha matatizo zaidi kwa Marekani na washirika wake kuliko utawala walioung'oa basi ushindi wao utakuwa wa goli la kujifunga hautakuwa na maana kwao,watakuwa wamefunga lakini hawakushinda!
Cha msingi Assad aliyekuwa anasaidiwa na kubwa na la Magaidi ( Iran) na Hezbollah kaondoka basi. Magaidi uchwara ya Korogwe na Urambo na Kilosa yamebaki midomo wazi
 
Honestly, kuanguka kwa huyu mwamba kiboko ya mataifa ya magharibi kumenihuzunisha sana. Was it coincidence or planned. Mbona imekuwa haraka sana wakati jana tu nimeskia Hezbollah wametuma maelfu ya wapiganaji kumsaidia ASSAD.

Wasiwasi wangu ni hii nchi kuangukia kwenye machafuko ya kila mara maana hawa wanamapinduzi wanataka nchi itawaliwe KIISLAM kwa itikadi kali, je itakuwaj hapo baadae.

All in all, nchi za magharibi ni chanzo cha machafuko na mapinduzi mengi Duniani ikiwemo Africa na hakika kwa hili wamefanikiwa. Yani wametegea RUSSIA na IRAN wako kwenye tension kubwa ya vita ndo wakawaambia waasi waanze safari ya kuelekea Damascus.

Je kuna uwezekano wa Russia na Iran ku-heat back ili kumrejesha kipenzi chao? Au ndo basi tena.

NB.
Kuna nchi nyingi sana Africa zimejificha kwenye kichaka kinachoitwa demokrasia, but in reality it's just propaganda or romantised democracy. Nchi km hizi pia mapinduzi ndo size yao.

Pole sana Russia, pole sana Iran, mimi nimeumia lakini nyie mmeumizwa zaidi.
mkuu tumia akil usiwe kama nyumb wa ccmu , hv kama shia na sunni wakianza pendana , nan atawagombanisha ? sababu ya yote ni wao , tusipende kujadili mambo kana kwamba wazungu tu ndo wana utimamu wa akili
 
Taleban haijaigeuka Marekani. Taleban inafuata matakwa ya Marekani.

Taleban ilikuwa inafuga magaidi, Marekani ikaivamia Afghanistan kuwaondoa Taleban ili wasiendelee kufuga magaidi. Ikiwa uko Afghanistan, US ikaunda military bases kadhaa pale Middle East. Ikapambana na kina al Qaeda ikaua kina Osama bin Laden na kupigana na kina Saddam Hussein.

Ikakaa miaka 20 Taleban wakiwa mafichonj. Ugaidi umeisha, Marekani haina purpose tena ya kukaa Afghanistan ikiwalea ikaondoka. Kwenye kuondoka US haikuielekeza Afghanistan iishije, bali ilisisitiza haitaki kufugwa gaidi wala kuharibu maslahi ya Marekani. Jambo ambalo Taleban wanalishikilia hadi leo.

Kuna siku Marekani ilifanya shambulizi la kuua magaidi ikaua kijana wa Waziri mmojawapo serikali ya Taliban, walitulia.

Russia inaondoka Tartus naval base na Hmeimin airbase. Pigia mstari hili.

Iran ina hasara. Kwa miaka zaidi ya 10 Iran imewekeza na kuikopesha serikali ya Assad zaidi ya dola bilioni 50. Zote zimeyeyuka kwa kuangushwa kwa utawala wa Assad. Iran haiwezi claim deni lake wala kurudisha investments zake wala kupata faida kidiplomasia na kiusalama kwenye axis of evil yake.

Houthi wanapokea silaha kwa njia ya maji na nyingi zinakuwa intercepted. Kufuatilia shipment ya majini ni rahisi kuliko ya ardhini. Kule Syria hata underground unaweza, hata kwa kutumia Kirikuu au canter unaweza. Sasa navigation ya kutoa shehena Iran hadi Yemen inatumia chombo kikubwa kidogo ambacho kitajulikana kirahisi.

Pia Yemen haipakani na Israel. Syria inapakana na Israel na vilevile Lebanon ambayo nayo inapakana na Israel. Sasa Yemen wale Houthi mpaka warushe makombora yapite anga la nchi adui yao ndio yafike Israel.

Hiyo Iraq yenyewe haina hasara kwa Israel kama ilivyokuwa enzi za Saddam. Syria ikiwa kama Iraq basi ni vyema kwa Israel.

Na Syria wakilazimisha vita Israel kiurahisi kabisa unajiongezea mipaka inajimegea Quneitra. Wasijaribu huo mtego.

Iraq ya Saddam ilikuwa na jaribio la nyuklia, ilikuwa na Scud missiles, ilikuwa na fighter jets. Iraq ilikuwa na bajeti ya kununua silaha kali za kisasa. Iraq ya Saddam ilikuwa na uwezo wa kufanya mobilization hata ya wanajeshi zaidi ya 300,000 kupigana na Israel au basi Saddam mwenyewe alikuwa na uwezo wa kutoa billions of dollars kwa wanamgambo wapigane na Israel.

Sasa hawa njaa kali wenye viroketi vichache na wapiganaji elfu kadhaa wanakuwaje tishio kwa Israel kuliko Iraq ya Saddam?
Kuhusu deni la Iran nadhani lipo kiserikali na sio kwamba alikuwa anakopeshwa Asad kama mtu binafisi.
Kwani Tz CCM ikipinduliwa basi madeni inayo daiwa Tz yatakuwa yamekufa?
 
Taleban haijaigeuka Marekani. Taleban inafuata matakwa ya Marekani.

Taleban ilikuwa inafuga magaidi, Marekani ikaivamia Afghanistan kuwaondoa Taleban ili wasiendelee kufuga magaidi. Ikiwa uko Afghanistan, US ikaunda military bases kadhaa pale Middle East. Ikapambana na kina al Qaeda ikaua kina Osama bin Laden na kupigana na kina Saddam Hussein.

Ikakaa miaka 20 Taleban wakiwa mafichonj. Ugaidi umeisha, Marekani haina purpose tena ya kukaa Afghanistan ikiwalea ikaondoka. Kwenye kuondoka US haikuielekeza Afghanistan iishije, bali ilisisitiza haitaki kufugwa gaidi wala kuharibu maslahi ya Marekani. Jambo ambalo Taleban wanalishikilia hadi leo.

Kuna siku Marekani ilifanya shambulizi la kuua magaidi ikaua kijana wa Waziri mmojawapo serikali ya Taliban, walitulia.
Hapa usitudanganye, Taliban ni kundi la mlengo mkali wa kijihadi ndio maana ilikaribisha hata makundi mengine kama Alqaeda.
Pia usitudanganye kuwa Taliban walikaa tu mafichoni ilhali Kambi za USA zilikuwa zikishambuliwa kwa hit and run na kujeruhi na kuua wanajeshi wengi tu Wa USA.
Trump kipindi anaingia madarakani Taliban walikua wameshaanza kuteka miji kama waasi wa HTS wanavyofanya Syria,kuona viongozi wa Afghan wanakimbia na wanajeshi wa Afghan wanasarenda wenyewe Trump alisema hakuna tena sababu ya wanajeshi wa US kufa kisa hao waafghan ambao wao wenyewe hawawezi jitetea.
Na aliongezea na kusema hakuna tena haja ya majeshi kuwepo kule.
Utasema hapa Afghanistan inafuata anachosema USA!?
Kwanini ilikua iki ambush Kambi zake kama inafuata anachosema USA!?
Russia inaondoka Tartus naval base na Hmeimin airbase. Pigia mstari hili.
Hili halijulikani muda ndio utaongea kama Russia itaondoa ama laa,inategemea na atayekuja.
Iran ina hasara. Kwa miaka zaidi ya 10 Iran imewekeza na kuikopesha serikali ya Assad zaidi ya dola bilioni 50. Zote zimeyeyuka kwa kuangushwa kwa utawala wa Assad. Iran haiwezi claim deni lake wala kurudisha investments zake wala kupata faida kidiplomasia na kiusalama kwenye axis of evil yake.
Kuhusu hasara ya deni hilo liko wazi.
Ila kuhusu uwepo wa axis of resistance bado itakuwepo pasi na ugumu wowote.
Houthi wanapokea silaha kwa njia ya maji na nyingi zinakuwa intercepted. Kufuatilia shipment ya majini ni rahisi kuliko ya ardhini. Kule Syria hata underground unaweza, hata kwa kutumia Kirikuu au canter unaweza. Sasa navigation ya kutoa shehena Iran hadi Yemen inatumia chombo kikubwa kidogo ambacho kitajulikana kirahisi.
Silaha zilizokuwa intercepted ni zile za kipindi cha 2023-2024 baada ya USA kuwa anafanya patrol red sea kuzuia mashambulizi ya Houthi pale Baan Al mandib,tofauti na hapo miaka ya nyuma yote Iran imekua inapeleka silaha Yemen pasi na shida.
Pia Yemen haipakani na Israel. Syria inapakana na Israel na vilevile Lebanon ambayo nayo inapakana na Israel. Sasa Yemen wale Houthi mpaka warushe makombora yapite anga la nchi adui yao ndio yafike Israel.

Hiyo Iraq yenyewe haina hasara kwa Israel kama ilivyokuwa enzi za Saddam. Syria ikiwa kama Iraq basi ni vyema kwa Israel.

Na Syria wakilazimisha vita Israel kiurahisi kabisa unajiongezea mipaka inajimegea Quneitra. Wasijaribu huo mtego.

Iraq ya Saddam ilikuwa na jaribio la nyuklia, ilikuwa na Scud missiles, ilikuwa na fighter jets. Iraq ilikuwa na bajeti ya kununua silaha kali za kisasa. Iraq ya Saddam ilikuwa na uwezo wa kufanya mobilization hata ya wanajeshi zaidi ya 300,000 kupigana na Israel au basi Saddam mwenyewe alikuwa na uwezo wa kutoa billions of dollars kwa wanamgambo wapigane na Israel.

Sasa hawa njaa kali wenye viroketi vichache na wapiganaji elfu kadhaa wanakuwaje tishio kwa Israel kuliko Iraq ya Saddam?
Iraq ya Saddam ilikua under USA influence kwa miaka mingi.
Ila Iraq ya sasa haiko under US influence.
Nadhani umejisahaulisha kuwa Palestin Islamic Jihad wapo Iraq na wanajiimarisha Iraq pia.
Na hao PIJ walishiriki katika shambulio la Oktoba 7 na pia wako mstari wa mbele kuisaidia Hamas.
Au kwa wewe unaona hilo ni jambo dogo!?
Kama Ingekua Iraq ya Saddam Hussein basi Saddam asingeruhusu hayo makundi yajiimarishe kwake tena under Iran influence.
Leo hii Iran inaingia na kufanya coordination ya kuishambulia Israel kupitia proxy wake hapo hapo Iraq na Iraq inakubali.
Usijisahaulishe pia kuanzia December kuja January makundi ya jihadi ya Iraq yalishiriki kuishambulia Israel na kuishambulia Kambi za USA zilizopo Iraq.
Unajisahaulisha pia kuwa silaha zingine kuelekea Syria kwenda Lebanon zinapitia Iraq.
Je angekuwepo Saddam hili lingetokea!?

Unachukulia mambo kiwepesi sana.
 
Si unaona sasa!?kwa hiyo juhudi nguvu,maarifa na rasilimali zao zote walizotumia kuuangusha utawala wa rais Saadam hussein, matokeo yake ni kuinufaisha Iran. Adui wao mkuu.
Iraq unayoiona sasa ina coordinate silaha kupita kuelekea Syria na kupokelewa na Lebanon Hizbollah.
Iraq hiyo hiyo Ina vikundi viwili vya axis of resistance ambavyo vilishiriki kuishambulia Israel wakati wa Oktoba 7 hadi sasa.
Iraq sasa hivi imejinasibu kuitaka USA iondoe kambi zake hapo Baghdad.
 
Sio kila sehemu huo msamiati unafanya kazi.
Muulize USA imekuaje kinyago chake Taliban kilimtisha.
Mmeanza tena ulongo wenu,... Marekani alishaanza siku nyingi ku withdraw vikosi vyake Afghanistan akabakiza wanajeshi kidogo sana kwa ajili ya training ya askari wa Afghanistan... Kwa hiyo askari wa Afghanistan wenyewe ndo walishindwa kulinda nchi Yao dhidi ya Taleban. Hamchelew kusema humu Marekani anawaogopa wale wapumbavu wa Taleban,kama jinsi wapuuzi wengine
wanavyosema Marekani kiboko Yao ni Houthi.... HATUTAKI UONGO UONGO HUMU TUAMBIENI NI LINI IRAN ANALIPA KISASI KWA ISRAEL MBONA ALISHAMBULIWA HALAFU KAAMUA KUKAA KIMYA
 
Honestly, kuanguka kwa huyu mwamba kiboko ya mataifa ya magharibi kumenihuzunisha sana. Was it coincidence or planned. Mbona imekuwa haraka sana wakati jana tu nimeskia Hezbollah wametuma maelfu ya wapiganaji kumsaidia ASSAD.

Wasiwasi wangu ni hii nchi kuangukia kwenye machafuko ya kila mara maana hawa wanamapinduzi wanataka nchi itawaliwe KIISLAM kwa itikadi kali, je itakuwaj hapo baadae.

All in all, nchi za magharibi ni chanzo cha machafuko na mapinduzi mengi Duniani ikiwemo Africa na hakika kwa hili wamefanikiwa. Yani wametegea RUSSIA na IRAN wako kwenye tension kubwa ya vita ndo wakawaambia waasi waanze safari ya kuelekea Damascus.

Je kuna uwezekano wa Russia na Iran ku-heat back ili kumrejesha kipenzi chao? Au ndo basi tena.

NB.
Kuna nchi nyingi sana Africa zimejificha kwenye kichaka kinachoitwa demokrasia, but in reality it's just propaganda or romantised democracy. Nchi km hizi pia mapinduzi ndo size yao.

Pole sana Russia, pole sana Iran, mimi nimeumia lakini nyie mmeumizwa zaidi.
Jibu ni ndio,Russia na Iran zinapumulia mashine,na hasa Iran baada ya viongozi wengi wa ugaidi kuuawa na Israel,hivyo wamapoteza muelekeo...
 
Mmeanza tena ulongo wenu,... Marekani alishaanza siku nyingi ku withdraw vikosi vyake Afghanistan akabakiza wanajeshi kidogo sana kwa ajili ya training ya askari wa Afghanistan... Kwa hiyo askari wa Afghanistan wenyewe ndo walishindwa kulinda nchi Yao dhidi ya Taleban. Hamchelew kusema humu Marekani anawaogopa wale wapumbavu wa Taleban,kama jinsi wapuuzi wengine
wanavyosema Marekani kiboko Yao ni Houthi.... HATUTAKI UONGO UONGO HUMU TUAMBIENI NI LINI IRAN ANALIPA KISASI KWA ISRAEL MBONA ALISHAMBULIWA HALAFU KAAMUA KUKAA KIMYA
Hata Syria wanajeshi wa Asad ndo wameshindwa kupigana maana Urusi na Iran walimsaidia kukomboa ardhi kubwa kutoka kwa waasi lakini yeye akashindwa kuunda jeshi imara kwa ajili ya kuilinda.

Kuhusu Iran kujibu kwani Israel alipo shambuliwa na Iran alijibu siku hiyo hiyo?
 
Iraq unayoiona sasa ina coordinate silaha kupita kuelekea Syria na kupokelewa na Lebanon Hizbollah.
Iraq hiyo hiyo Ina vikundi viwili vya axis of resistance ambavyo vilishiriki kuishambulia Israel wakati wa Oktoba 7 hadi sasa.
Iraq sasa hivi imejinasibu kuitaka USA iondoe kambi zake hapo Baghdad.
Naam, hayo ndiyo malipo wanayoyapata Warekani na washirika wake wa magharibi baada ya kuuangusha utawala wa Saadam Hussein, huku Iran ikichukuliwa kama ndugu na rafiki kipenzi kwa utawala mpya wa Iraq uliopo madarakani.
Bila shaka na malipo watakayolipwa wadhamin wa mapinduzi ya Syria yatafanana na hayo.
 
Kuhusu deni la Iran nadhani lipo kiserikali na sio kwamba alikuwa anakopeshwa Asad kama mtu binafisi.
Kwani Tz CCM ikipinduliwa basi madeni inayo daiwa Tz yatakuwa yamekufa?
Hawalipi hilo deni Iran itawafanya nini sasa.
Hao jamaa wanajua habari za kuheshimu mikataba kwani. North Korea ilikopa magari ya Volvo kama elfu moja hivi, haijawahi lipa hadi leo miaka zaidi ya 30.

Au wewe ni lini umesikia Houthi wameanza kulipa deni ambalo Saudi Arabia ilikopesha serikali ya Ali Abdullah Saleh (R.I.P) au ya Rais Mansur Hadi.

Mpaka Syria ije kulipa labda ije serikali tofauti na hawa vibaka waliokuwa wanashambuliwa na Iran. Wana hasira nayo sana.
 
Hapa usitudanganye, Taliban ni kundi la mlengo mkali wa kijihadi ndio maana ilikaribisha hata makundi mengine kama Alqaeda.
Pia usitudanganye kuwa Taliban walikaa tu mafichoni ilhali Kambi za USA zilikuwa zikishambuliwa kwa hit and run na kujeruhi na kuua wanajeshi wengi tu Wa USA.
Trump kipindi anaingia madarakani Taliban walikua wameshaanza kuteka miji kama waasi wa HTS wanavyofanya Syria,kuona viongozi wa Afghan wanakimbia na wanajeshi wa Afghan wanasarenda wenyewe Trump alisema hakuna tena sababu ya wanajeshi wa US kufa kisa hao waafghan ambao wao wenyewe hawawezi jitetea.
Na aliongezea na kusema hakuna tena haja ya majeshi kuwepo kule.
Utasema hapa Afghanistan inafuata anachosema USA!?
Kwanini ilikua iki ambush Kambi zake kama inafuata anachosema USA!?
US iliifukuza Taliban madarakani kwa miaka 20, as long as US ingebaki Afghanistan ndoto za Taliban kuteka utawala wa Afghanistan sahau.
Rais wa Taliban alikuwa mapangoni uko.

Kama Taliban haijanywea kwa masharti ya Marekani kwenye mazungumzo waliyofanya basi tuambie tangu Marekani itoke Taliban imefanya shambulizi gani dhidi ya US au Israel?
Taliban inafuata ilichopangiwa na Marekani baada ya mkataba, sio before. Ndio maana Marekani imeacha silaha na kila kitu pale ikijua Taliban atazitumia hizi silaha kulinda amani na kuthibiti ugaidi.

Trump ni sera yake kwenye kampeni, sio reaction kuondoa majeshi yake.
Hili halijulikani muda ndio utaongea kama Russia itaondoa ama laa,inategemea na atayekuja.
Russia ameishaondoa meli na ndege na troops hizo bases. Kabakiza vitu kidogo, waasi hawamtaki hapo, Uturuki haipendelei kumuona pale.
Iraq ya Saddam ilikua under USA influence kwa miaka mingi.
Ila Iraq ya sasa haiko under US influence.
Nadhani umejisahaulisha kuwa Palestin Islamic Jihad wapo Iraq na wanajiimarisha Iraq pia.
Na hao PIJ walishiriki katika shambulio la Oktoba 7 na pia wako mstari wa mbele kuisaidia Hamas.
Au kwa wewe unaona hilo ni jambo dogo!?
Kama Ingekua Iraq ya Saddam Hussein basi Saddam asingeruhusu hayo makundi yajiimarishe kwake tena under Iran influence.
Leo hii Iran inaingia na kufanya coordination ya kuishambulia Israel kupitia proxy wake hapo hapo Iraq na Iraq inakubali.
Usijisahaulishe pia kuanzia December kuja January makundi ya jihadi ya Iraq yalishiriki kuishambulia Israel na kuishambulia Kambi za USA zilizopo Iraq.
Unajisahaulisha pia kuwa silaha zingine kuelekea Syria kwenda Lebanon zinapitia Iraq.
Je angekuwepo Saddam hili lingetokea!?

Unachukulia mambo kiwepesi sana.
Iraq ya Saddam ilikuwa tishio kwa Israe. Syria ya Hafez al Assas ilikuwa tishio dhidi ya Israel.

Hawa wanamgambo wa Iraq hawafiki hata nusu ya uwezo wa Hezbollah, sasa Israel inawapiga Hezbollah kama watoto ndio ije ishindwe PIJ?
Yaani unalinganisha tishio la PIJ na uwezo wa kijeshi wa Saddam Hussein mbona unalinganisha chandimu na ligi kuu.

Syria ilipozidiwa Yom Kippur war ikatishiwa kupigwa Damascus ikaomba msaada kwa Waarabu, Iraq ilitoa wanajeshi 30,000 vifaru 400 na APC kama 600. Yani huo ni msaada wa kufumba na kufumbua. Sasa PIJ hata 15,000 wa kwenda Israel wapo? Vifaru hata 10 wanavyo wale?

Saddam karusha modified Scud missiles 42 kwenye Gulf war kwenda Israel na kuua watu 13. Wanamgambo wa Iraq hawana uwezo huo wa kutishia amani Israel kama mwaka ule 1991.

Au tuje kwa hawa Syria. Enzi za Hafez al Assad anavamia Israel na ndege 100, mamia ya vifaru na maelfu ya wanajeshi. Akapiga Golan heights akaingia Valley of tears wakapigana vikali na IDF ndio akatolewa. Ndio Syria hiyohiyo unaiona sasa, hii ya mabodaboda wanarukaruka ndio unadai itaitishia Israel kuliko stable Syria ya Hafez ambayo at any moment ilikuwa inaweza kusanya wapiganaji 200,000 na ina bajeti ya kutosha?

Israel kwa sasa ina jeuri mno. Kipindi yupo Assad senior na Saddam usingeona Israel inaingia hata Gaza. Ilikuwa inaishi mashakani
 
Hawalipi hilo deni Iran itawafanya nini sasa.
Hao jamaa wanajua habari za kuheshimu mikataba kwani. North Korea ilikopa magari ya Volvo kama elfu moja hivi, haijawahi lipa hadi leo miaka zaidi ya 30.

Au wewe ni lini umesikia Houthi wameanza kulipa deni ambalo Saudi Arabia ilikopesha serikali ya Ali Abdullah Saleh (R.I.P) au ya Rais Mansur Hadi.

Mpaka Syria ije kulipa labda ije serikali tofauti na hawa vibaka waliokuwa wanashambuliwa na Iran. Wana hasira nayo sana.
Wahuthi hawawezi kulipa kwa sababu mpaka sasa hawatambuliki kama serikali bali inayo ni serikali iliyo mjini Aden.
 
Back
Top Bottom