Je, kukosa kwetu ajira na ugumu wa kupata pesa, lawama tumtwishe nani?

Je, kukosa kwetu ajira na ugumu wa kupata pesa, lawama tumtwishe nani?

Okwaaa

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2020
Posts
1,332
Reaction score
2,963
Wasalaam wakuu,

Kwanza poleni na kazi kwa ambao michongo imegoma mpaka sasa, na pia hongereni na kazi kwa ambao michongo imeenda sawa.

Wakuu, mm ni mhanga wa kukosa ajira, zaidi mhanga wa maisha magumu. Siku hizi nimeshaanza kuzoea mlo mmoja😁, sijisifii ila ukweli upande wangu hali ni ngumu. Nahofia vidonda vya tumbo.

Binafsi nishamove home saizi najitegemea kigeto zaidi. Ila geto langu ukiona utacheka, hali imekuwa ngumu hadi natamani kuuza vitu hivyo hivyo vichache vya geto kama ndoo za maji na kimeza ili nipate mlo😆

Sitanii jamani hali ni ngumu, nimejaribu kuwaomba watu waliopo humu connection but imekuwa ngumu, nimetangaza kuuza simu yangu hii nayotumia ili nibalance maisha na mtaji, bado sipati mteja, wengi tunashindwana kwa sababu ya umbali. Nimejaribu kuparangana kutafta hela lakini naambulia patupu.

Siku yote naparangana kupata 2000 na yenyewe inanipiga chenga. Hii inanikumbusha kipindi nipo chuo niliwahi shuhudia wabeba mizigo wakichomana bisibisi stend kuu kisa sh mia (100) nikastaajabu sana, ila saizi naona inawezekana kabisa 86%.

Sasa niwaulize wajuzi wa mambo, huu ugumu wa maisha ulikuwepo tangu enzi na enzi au? (tusije mlaumu mtu bure). Au huu utawala wa JPM ndo umezidisha huu ugumu wa maisha?

Mlioanza kujitegemea tangia utawala wa JK tupeni mrejesho basi wakuu?

Mwisho. Sijachoka kutafta kazi halali ya kunipatia kipato kidogo, maana ndoto yangu kubwa nimsaidie bi mkubwa wangu maana umri unaenda na mimi sina kitu (ni aibu).

Pia nauza simu ili nijiajiri, unaweza kunipa msaada tu hata kwa kununua simu yangu Samsung A10 kwa 215,000/=, hiyo hela cash ina maana kubwa sana.

0746866631.
 
Maisha magumu pande zote mjomba, bado kidogo tutaanza kufurahi, ukimwelekeza bi mkubwa atakuelewa, hata kwa jk maisha yalikua magumu kama huna ajira, kilichoongezeka miaka hii ni matarajio. Tumekua tukitarajia mambo mazuri, hasa baada ya kumaliza kusoma. Tafuta jimama ujiweke mwanangu, maisha haya mafupi, unateseka miaka 10 ya maisha yako wakati kuna mjane mwenye hela za urithi anatafuta wa kumtibu upweke.
 
Serikali ilaumiwe kwa sababu imeshindwa kutoa mazingira rafiki ya watu kujiajiri na kuongeza mzunguko wa pesa. Kodi zinapanda kila siku, Biashara zinafungwa, Sekta Binafsi ambayo ikiwezeshwa inaweza kutoa ajira kwa wengi nayo inafifishwa kwa mambo ya ajabu, wawekezaji wanapewa mazingira magum ya kuwekeza nchini sababu ikiwa eti ni uzalendo
Yote hayo yasipowezekana serikali ndo inakua imeshikilia pesa haitaingia kwa raia yoyote kwa namna yoyote.

Kwa staili hii uchumi wa mtu mmoja mmoja lazima udorore tu.
 
Hapo ni wewe na kichwa chako ukikosa jibu geukia family yako ww Sasa yaani baba na mamaako.kisha tafakari kwanini jirani yako ana ajira
 
Asante mkuu kwa ushauri🙏
maisha magumu pande zote mjomba, bado kidogo tutaanza kufurahi, ukimwelekeza bi mkubwa atakuelewa, hata kwa jk maisha yalikua magumu kama huna ajira, kilichoongezeka miaka hii ni matarajio. Tumekua tukitarajia mambo mazuri, hasa baada ya kumaliza kusoma. Tafuta jimama ujiweke mwanangu, maisha haya mafupi, unateseka miaka 10 ya maisha yako wakati kuna mjane mwenye hela za urithi anatafuta wa kumtibu upweke.
 
Wasalaam wakuu,

Kwanza poleni na kazi kwa ambao michongo imegoma mpaka sasa, na pia hongereni na kazi kwa ambao michongo imeenda sawa.

Wakuu, mm ni mhanga wa kukosa ajira, zaidi mhanga wa maisha magumu. Siku hizi nimeshaanza kuzoea mlo mmoja😁, sijisifii ila ukweli upande wangu hali ni ngumu. Nahofia vidonda vya tumbo.

Binafsi nishamove home saizi najitegemea kigeto zaidi. Ila geto langu ukiona utacheka, hali imekuwa ngumu hadi natamani kuuza vitu hivyo hivyo vichache vya geto kama ndoo za maji na kimeza ili nipate mlo😆

Sitanii jamani hali ni ngumu, nimejaribu kuwaomba watu waliopo humu connection but imekuwa ngumu, nimetangaza kuuza simu yangu hii nayotumia ili nibalance maisha na mtaji, bado sipati mteja, wengi tunashindwana kwa sababu ya umbali. Nimejaribu kuparangana kutafta hela lakini naambulia patupu.

Siku yote naparangana kupata 2000 na yenyewe inanipiga chenga. Hii inanikumbusha kipindi nipo chuo niliwahi shuhudia wabeba mizigo wakichomana bisibisi stend kuu kisa sh mia (100) nikastaajabu sana, ila saizi naona inawezekana kabisa 86%.

Sasa niwaulize wajuzi wa mambo, huu ugumu wa maisha ulikuwepo tangu enzi na enzi au? (tusije mlaumu mtu bure). Au huu utawala wa JPM ndo umezidisha huu ugumu wa maisha?

Mlioanza kujitegemea tangia utawala wa JK tupeni mrejesho basi wakuu?

Mwisho. Sijachoka kutafta kazi halali ya kunipatia kipato kidogo, maana ndoto yangu kubwa nimsaidie bi mkubwa wangu maana umri unaenda na mimi sina kitu (ni aibu).

Pia nauza simu ili nijiajiri, unaweza kunipa msaada tu hata kwa kununua simu yangu Samsung A10 kwa 215,000/=, hiyo hela cash ina maana kubwa sana.

0746866631.
The inner circle
IMG_20210211_163253.jpg
 
Usimfuatilie Bujibuji, mpuuzie, ni mwehu kabisa hana akili hata moja. Respect your limited time and use it effectively
Mhhh! Mkuu heshima yako ni kubwa sanaaa within jf na may be outside jf. So bado nitakupa heshima yako sana mkuu. 🙏🙏
 
Back
Top Bottom