Je, Kuna Taasisi ya ovyo Kabisa Nchini Kuizidi TANESCO?

Je, Kuna Taasisi ya ovyo Kabisa Nchini Kuizidi TANESCO?

Bila shaka hakuna asiyejua madhara ya TANESCO, iwe mjini au kijijini, awe kiongozi au raia asiye na cheo, awe kijana au mzee, awe msomi au asiyeenda shule kabisa, awe mwenye kiwanda au mmiliki wa genge.

Ni takribani miaka 250 tangu Benjamin Franklin na Michael Faraday walipoweka kanuni jinsi umeme unavyozalishwa na unavyofanya kazi, lakini mpaka leo Tanzania haielewi chochote hata kwa vile vinavyoonekana kwa macho, kuhusiana na umeme. Uzalishaji wa umeme ni kati ya tekinolojia rahisi za kiwaida isiyohitaji elimu na tekinolojia ya pekee, lakini kwa Tanzania, hata kufunga tu wire au kuchomeka nguzo vizuri ya umeme ardhini ili isidondoke, inaonekana ni tekinolojia ngumu sana!!!

Mtanisahihisha, lakini kwa mtazamo wangu, TANESCO ni taasisi muhimu sana ambayo ubora au ubovu wake unagusa kila mahali katika maisha ya Mtanzania. Lakini kwa bahati mbaya sana, taasisi hii iliyo muhimu kabisa, bila shaka wamepewa watu wa hovyo kabisa, wenye uelewa duni kabisa, watu wazembe kabisa ambao upeo wao wa kuona mambo unaishia kwenye vidole vyao vya miguuni. Ukiwaona mitaani ya yale makoti yao unaweza kudhani wanafanya kazi, lakini kwa kiasi kikubwa wanazurura tu bila kuleta matokeo yoyote chanya.

Kuanzia Wizarani ambako kuna waziri, mpaka huko chini kwa wahandisi na mafundi, kote kumejaa watu waongo wanaotaka kuficha ubovu wao kwa kutengeneza hadithi za uwongo. Badala ya kutumia muda mwingi kufikiria namna ya kumaliza matatizo ya umeme, wao muda wote wanafikiria namna ya kutengeneza uwongo.

Miezi miwili iliyopita niitembelea vijiji 4 ambavyo vinatumia umeme kutoka kwenye mradi uliofadhiliwa na Kanisa Katoliki. Katika mwezi mzima, nilishuhudia umeme kukatika mara 2, na mara zote, haikuzidi nusu saa. Mradi huo unaendeshwa na wanakijiji wenyewe, na viongozi na watendaji wote wa mradi, hakuna mhandisi wala mfanyakazi yeyote mwenye hata degree moja. Lakini umeme ni wa uhakika.

Kwa aina ya watu waliopo wizara ya nishati mpaka hao waliopo TANESCO, nawahakikishieni, hata bwawa la Nyerere lianze kufanya kazi, hakuna kitakachobadilika. Maana tatizo kubwa halipo kwenye vyanzo vya umeme bali aina ya watu waliopo.

Muda huu ninaoandika, nimewasiliana na watu mbalimbali na kuthibitishiwa kuwa maeneo mengi ya nchi hakuna umeme.

Tujiulize, hivi watu waliyopo huko TANESCO wana uhalali gani wa kuendelea kuwatesa Watanzania kiasi hiki? Na mamlaka za juu, kwa nini zinaamua kuwatesa Watanzania kupitia TANESCO kwa kuwaweka watu ambao kwa kipimo chochote, hawafai na ni hasara kwa Taifa zima? Na sisi wananchi tutaendelea kuwavumilia hawa watu mpaka lini?

Kuna haja ya kuandaa maandamano makubwa dhidi ya TANESCO na watawala. Watawala muda huu ambao sehemu kubwa ya nchi ipo gizani, watawala wamewashiwa generators. Hawana giza.
Shirika limejaa mateja 95% unategemea tija itoke wapi
 
Mama yangu Samia Kama utapita hapa please Niko chini ya miguu yako. Ombi nalitoa kwako binafsisha TANESCO.
 
Bila shaka hakuna asiyejua madhara ya TANESCO, iwe mjini au kijijini, awe kiongozi au raia asiye na cheo, awe kijana au mzee, awe msomi au asiyeenda shule kabisa, awe mwenye kiwanda au mmiliki wa genge.

Ni takribani miaka 250 tangu Benjamin Franklin na Michael Faraday walipoweka kanuni jinsi umeme unavyozalishwa na unavyofanya kazi, lakini mpaka leo Tanzania haielewi chochote hata kwa vile vinavyoonekana kwa macho, kuhusiana na umeme. Uzalishaji wa umeme ni kati ya tekinolojia rahisi za kiwaida isiyohitaji elimu na tekinolojia ya pekee, lakini kwa Tanzania, hata kufunga tu wire au kuchomeka nguzo vizuri ya umeme ardhini ili isidondoke, inaonekana ni tekinolojia ngumu sana!!!

Mtanisahihisha, lakini kwa mtazamo wangu, TANESCO ni taasisi muhimu sana ambayo ubora au ubovu wake unagusa kila mahali katika maisha ya Mtanzania. Lakini kwa bahati mbaya sana, taasisi hii iliyo muhimu kabisa, bila shaka wamepewa watu wa hovyo kabisa, wenye uelewa duni kabisa, watu wazembe kabisa ambao upeo wao wa kuona mambo unaishia kwenye vidole vyao vya miguuni. Ukiwaona mitaani ya yale makoti yao unaweza kudhani wanafanya kazi, lakini kwa kiasi kikubwa wanazurura tu bila kuleta matokeo yoyote chanya.

Kuanzia Wizarani ambako kuna waziri, mpaka huko chini kwa wahandisi na mafundi, kote kumejaa watu waongo wanaotaka kuficha ubovu wao kwa kutengeneza hadithi za uwongo. Badala ya kutumia muda mwingi kufikiria namna ya kumaliza matatizo ya umeme, wao muda wote wanafikiria namna ya kutengeneza uwongo.

Miezi miwili iliyopita niitembelea vijiji 4 ambavyo vinatumia umeme kutoka kwenye mradi uliofadhiliwa na Kanisa Katoliki. Katika mwezi mzima, nilishuhudia umeme kukatika mara 2, na mara zote, haikuzidi nusu saa. Mradi huo unaendeshwa na wanakijiji wenyewe, na viongozi na watendaji wote wa mradi, hakuna mhandisi wala mfanyakazi yeyote mwenye hata degree moja. Lakini umeme ni wa uhakika.

Kwa aina ya watu waliopo wizara ya nishati mpaka hao waliopo TANESCO, nawahakikishieni, hata bwawa la Nyerere lianze kufanya kazi, hakuna kitakachobadilika. Maana tatizo kubwa halipo kwenye vyanzo vya umeme bali aina ya watu waliopo.

Muda huu ninaoandika, nimewasiliana na watu mbalimbali na kuthibitishiwa kuwa maeneo mengi ya nchi hakuna umeme.

Tujiulize, hivi watu waliyopo huko TANESCO wana uhalali gani wa kuendelea kuwatesa Watanzania kiasi hiki? Na mamlaka za juu, kwa nini zinaamua kuwatesa Watanzania kupitia TANESCO kwa kuwaweka watu ambao kwa kipimo chochote, hawafai na ni hasara kwa Taifa zima? Na sisi wananchi tutaendelea kuwavumilia hawa watu mpaka lini?

Kuna haja ya kuandaa maandamano makubwa dhidi ya TANESCO na watawala. Watawala muda huu ambao sehemu kubwa ya nchi ipo gizani, watawala wamewashiwa generators. Hawana giza.
Huwa nazikwepa Sana thread za Tanesco maana hawa ni mapepo pasee, ukianza kuwataja hapohapo ulipo wanawakatia umeme uwaseme vizuri.

Ndio sababu hakuna thread sitakagi kabisa kuchangia kama hizi hasa Leo jumapili nimepumzika home hawakawii kukuharibia siku.
 
CCM, baba kazaliwa kakua kasoma kamaliza katafuta mchumba kaoa wamezaa mtoto anatembea, bado mama, baba na mtoto wao wanakwenda mbugani kuchota maji kwenye gema ambalo tembo alichimba kwa ajili ya matumizi yake na mwae, eti mama ameupiga mwingi.

Na ndiyo maana kipindupindu kina mkataba wa kudumu na Serikali ya CCM.
 
Katika serikali iliyoongozwa na JPM walikuwepo baadhi ya mawaziri waliozitendea haki wizara ngumu walizopewa dhamana ya kuziongoza. Mojawapo alikuwa ni Mh. Lukuvi ambaye kwa kiasi kikubwa aliitendea haki Wizara ya Ardhi na kuweza kufanikiwa kutafuta ufumbuzi wa migogoro mingi ya ardhi nchini.

Sijui hata ni kwa nini mkongwe kama huyu hakuweza kuaminika na kisha kupewa unaibu waziri mkuu na uwaziri wa nishati ili aweze kuuadabisha uongozi na wafanyakazi wa TANESCO!?

Hivi katiba inamruhusu ex-CAG Mussa Assad kuteulwa kuwa mwenyekiti wa bodi katika shirika hili!? Mtu kama huyu kwa hakika angaliweza kufanya mageuzi makubwa katika shirika lenye utata mwingi kama hili.
 
Tatizo nchi yetu, Raia tunalalamika, utakuta kiongozi mkubwa naye analalamika. Tanesco kinachowasumbua wanatumika sana kisiasa, ilibidi watolewe kwenye monopoly waruhusu ushindani kutoka makampuni binafsi.

Linawezekana ila wanajua wakiwekwa kwenye ushindani watapotea kama ttcl
 
Na Watanzania kwa kuzoea matatizo imekuwa jadi yetu tunaona sawa tu kukaa siku nzima bila umeme.

Hii mentality ndio inapelekea baadhi ya viongoz kutuchkulia poa , they dont care kwa sababu hata waki underperform hamna lolote mtawafanya, mtavumilia as usual
 
Hiyo mitambo ni ya kisasa, ikihisi hatari inajizima, na haiwaki mpaka hatari iishe, watu wanataka iendelee kuwaka wamulike vitambi vyao walivyoshiba magimbi at the risk ya mitambo kuungua
Mitambo hiyo hiyo ndio imefungwa ujerumani, uingereza na china. Mbona huko haijuzimi?
Tafuta sababu nyingine.
 
Upuuzi mtupu!

Niambie ni wapi kwenye uhakika wa maji? Maeneo mengi wananchi wanategemea maji ya mvuana mito, au unataka kusema mvua zinazonyesha ni matunda ya serikali ya awamu ya 6?

Subiri mvua ziishe halafu uje utoe taarifa jinsi Serikali ya awamu ya 6 ilivyomaliza tatizo la maji.
Relax na jitahid atleast uwe normal,

wanadamu tumeumbwa kusahau na zadi sana kujipa umuhimu nkubwa na wa taofauti sana na binadamu wengine...

bila mihemko na ghadhabu ndipo unaweza kuelewa na kujifunza jambo..
vinginevyo ntasema mfano huu juu ya hoja ile, utaacha hoja utadandia mfano kwa maswali yasio muhimu na matokeo yake ni kupoteza wakati bila sababu...

mwenye maskio aliskia mikakati ya serikali kuhusu tataizo la umeme na wenye uelewa waneketi tuli wakisubiri ilichoahidi serikali juu ya jambo hili...

nyie wengine wa negativity hakuna namna tunaweza wasaidia katika muondokane na hiyo negativity....
 
Bila shaka hakuna asiyejua madhara ya TANESCO, iwe mjini au kijijini, awe kiongozi au raia asiye na cheo, awe kijana au mzee, awe msomi au asiyeenda shule kabisa, awe mwenye kiwanda au mmiliki wa genge.

Ni takribani miaka 250 tangu Benjamin Franklin na Michael Faraday walipoweka kanuni jinsi umeme unavyozalishwa na unavyofanya kazi, lakini mpaka leo Tanzania haielewi chochote hata kwa vile vinavyoonekana kwa macho, kuhusiana na umeme. Uzalishaji wa umeme ni kati ya tekinolojia rahisi za kiwaida isiyohitaji elimu na tekinolojia ya pekee, lakini kwa Tanzania, hata kufunga tu wire au kuchomeka nguzo vizuri ya umeme ardhini ili isidondoke, inaonekana ni tekinolojia ngumu sana!!!

Mtanisahihisha, lakini kwa mtazamo wangu, TANESCO ni taasisi muhimu sana ambayo ubora au ubovu wake unagusa kila mahali katika maisha ya Mtanzania. Lakini kwa bahati mbaya sana, taasisi hii iliyo muhimu kabisa, bila shaka wamepewa watu wa hovyo kabisa, wenye uelewa duni kabisa, watu wazembe kabisa ambao upeo wao wa kuona mambo unaishia kwenye vidole vyao vya miguuni. Ukiwaona mitaani ya yale makoti yao unaweza kudhani wanafanya kazi, lakini kwa kiasi kikubwa wanazurura tu bila kuleta matokeo yoyote chanya.

Kuanzia Wizarani ambako kuna waziri, mpaka huko chini kwa wahandisi na mafundi, kote kumejaa watu waongo wanaotaka kuficha ubovu wao kwa kutengeneza hadithi za uwongo. Badala ya kutumia muda mwingi kufikiria namna ya kumaliza matatizo ya umeme, wao muda wote wanafikiria namna ya kutengeneza uwongo.

Miezi miwili iliyopita niitembelea vijiji 4 ambavyo vinatumia umeme kutoka kwenye mradi uliofadhiliwa na Kanisa Katoliki. Katika mwezi mzima, nilishuhudia umeme kukatika mara 2, na mara zote, haikuzidi nusu saa. Mradi huo unaendeshwa na wanakijiji wenyewe, na viongozi na watendaji wote wa mradi, hakuna mhandisi wala mfanyakazi yeyote mwenye hata degree moja. Lakini umeme ni wa uhakika.

Kwa aina ya watu waliopo wizara ya nishati mpaka hao waliopo TANESCO, nawahakikishieni, hata bwawa la Nyerere lianze kufanya kazi, hakuna kitakachobadilika. Maana tatizo kubwa halipo kwenye vyanzo vya umeme bali aina ya watu waliopo.

Muda huu ninaoandika, nimewasiliana na watu mbalimbali na kuthibitishiwa kuwa maeneo mengi ya nchi hakuna umeme.

Tujiulize, hivi watu waliyopo huko TANESCO wana uhalali gani wa kuendelea kuwatesa Watanzania kiasi hiki? Na mamlaka za juu, kwa nini zinaamua kuwatesa Watanzania kupitia TANESCO kwa kuwaweka watu ambao kwa kipimo chochote, hawafai na ni hasara kwa Taifa zima? Na sisi wananchi tutaendelea kuwavumilia hawa watu mpaka lini?

Kuna haja ya kuandaa maandamano makubwa dhidi ya TANESCO na watawala. Watawala muda huu ambao sehemu kubwa ya nchi ipo gizani, watawala wamewashiwa generators. Hawana giza.
Tanesko na Dada yake Nida wanaoboa mno Ila Tanesko hapa mpinzani, Tanesko ni kijana/mzee wa Hovyo.
 
Tanesko na Dada yake Nida wanaoboa mno Ila Tanesko hapa mpinzani, Tanesko ni kijana/mzee wa Hovyo.
Kama wazee wanawaacha wake zao nyumbani na kwenda kufanyiwa massage Sinza na kuacha laki huko.
 
Na wanalipwa mishahara na posho! Za kazi Gani sasa. Tanesco ifutiliwe mbali tuanze upya
 
Hiyo mitambo ni ya kisasa, ikihisi hatari inajizima, na haiwaki mpaka hatari iishe, watu wanataka iendelee kuwaka wamulike vitambi vyao walivyoshiba magimbi at the risk ya mitambo kuungua
Utakuwa mmoja wao bosi.
Hatar ya aaje kwamfano jombaa
 

Huwa nazikwepa Sana thread za Tanesco maana hawa ni mapepo pasee, ukianza kuwataja hapohapo ulipo wanawakatia umeme uwaseme vizuri.

Ndio sababu hakuna thread sitakagi kabisa kuchangia kama hizi hasa Leo jumapili nimepumzika home hawakawii kukuharibia siku.
Acha kuzuga wewe ni mfanyakazi wa Tanesco na uko kitengo cha imejensi, nani asiyekujua.
 
Sasa kama akili zinawaza ngono 24/7 Unafikiri akili ya kuwaza maendeleo na nia ya dhati ya kuyapigania itatoka wapi?
 
ni kweli kuna changamoto ya umeme nchini na mara kadha wahusika wameshalielezea kwa kina jambo hili na mikakati inayotekelezwa kulikabili .

ni vizuri kuwa na subra na wastahimilivu. Ni vizuri zaidi kuwapa muda wa kitosha zaidi ili walishughulikie kwa uhakika zaidi ili kuondokana na kadhia hii ya kukatikatika kwa nishati hiyo muhimu nchini..

hayo mengine yabaki tu kama maoni na mtazamo utatuzi unakuja.🐒
Umeme usingekuwa tatizo mpaka leo kama wasingevuruga uchaguzi, wanaficha lkn ukweli ndio huo.
 
Shida kubwa sio shirika,bali nidhamu katika mtiririko wa kimajukumu.
Nchi hii mwanasiasa ana maamuzi kuliko mtaalamu.
Nchi hii pia,hata uwe na PhD ya kitu flani
Lakini amini usiamini std 7,4m4 mwenye cheti Cha veta aliyepenya kwenye siasa na kumpata cheo ndo huyo huyo atakaetaka mawazo yake yafanyiwe kazi na sio utaalamu.

Mpangilio huo hakuna wa kulaumiwa zaidi ya Ccm inayokataa mchakato wa Katiba mpya.

Kama democrasia inafana,mbona Marekani yenye wananchi zaidi ya 200m wana vyama viwili na pia Katiba Yao ni kwamba,haijalishi unatokea malengo gani.ila ukifika White House. Unakutana na sela za Nchi,na sio sela za chama Wala za kwako binafsi.

Kwetu tumejaza vyama mfu rukuki ambavyo havina tija Kwa taifa ambavyo mnufaika ni huyu jinamizi CCM.

Viongozi wa kisiasa wamekuwa ndo wenye sauti kuliko wataalamu.

Hivyo,usikute tatizo la Tanesco linaanzia Kwa wanasiasa.

Watumishi mtawasurubisha bule,ila tatizo lipo kemwenye vyeo vya KISIASA.Na sio kwenye vyeo vya kiutendaji.
 
Relax na jitahid atleast uwe normal,

wanadamu tumeumbwa kusahau na zadi sana kujipa umuhimu nkubwa na wa taofauti sana na binadamu wengine...

bila mihemko na ghadhabu ndipo unaweza kuelewa na kujifunza jambo..
vinginevyo ntasema mfano huu juu ya hoja ile, utaacha hoja utadandia mfano kwa maswali yasio muhimu na matokeo yake ni kupoteza wakati bila sababu...

mwenye maskio aliskia mikakati ya serikali kuhusu tataizo la umeme na wenye uelewa waneketi tuli wakisubiri ilichoahidi serikali juu ya jambo hili...

nyie wengine wa negativity hakuna namna tunaweza wasaidia katika muondokane na hiyo negativity....
Sisi wengine tinaangalia zaidi vitendo kuliko hadithi.

1) Makamba alisema kuwa umeme umekuwa wa shida kwa sababu wakati wa kipindi cha awamu ya 5, hakukuwa na service ya mitambo, hivyo mitambo sasa hivi inafanyiwa matengenezo, baada ya matengenezo, mgao utakuwa historia. Je, tatizo la umeme lilikuwa historia au ni maisha ya kila siku?

2) Baadaye Makamba alisema kuwa, kuna upungufu wa maji. Tatizo la mgao litaisha mabwawa yakijaa maji. Je, tatizo la mgao wa umeme limeisha?

3) Mvua zilipoanza kunyesha, hadithi ikabadilika, ikawa tatizo la umeme linasababishwa na miundombinu, hasa nguzo kuoza. Wakasema tatizo litaisha baada ya kukamilisha ubadilishaji wa nguzo kutoka za miti na kuwa za zege. Baada ya hilo zoezi kukamilika maeneo mengi, kumekuwa na utofauti wowote?

4) Sahizi hadithi imebadilika na kuwa linasubiriwa bwawa la Nyerere, kuanzia mwezi wa pili tatizo la umeme litakwisha, tena hiyo ni kauli ya Rais. Mwezi wa pili ni wiki tu hii ijayo, wewe unaona kuna hata dalili?

Matatizo humalizwa kwa kutenda siyo kwa ngonjera za mdomoni. Kuna watu Serikalini na huko TANESCO wanataka kumaliza tatizo la umeme kwa hadithi za mdomoni!!
 
Back
Top Bottom