#COVID19 Je, kuna tofauti gani kati ya nchi zilizochanja raia wake na zile ambazo hazichanji raia wake chanjo ya covid-19?

#COVID19 Je, kuna tofauti gani kati ya nchi zilizochanja raia wake na zile ambazo hazichanji raia wake chanjo ya covid-19?

COARTEM

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2013
Posts
3,603
Reaction score
3,658
Tanzania ni nchi pekee duniani ambayo haijachanja raia wake chanjo ya covid-19 mpaka sasa.

Nchi nyingi duniani zimechanja raia wake chanjo ya covid-19.

SWALI:
Je, kimadhara na faida, kuna tofauti gani kati ya Tanzania na hizo nchi zilizochanja watu wake?
Je, Tanzania watu wamekufa sana na covid-19 kuliko India, Africa kusini, Italia e.t.c?
Je, kiuchumi Tanzania imeathirika kwa kiwango gani?

Labda tujilinganishe na Kenya au Uganda...nani ameathirika na janga la covid-19 ukilinganisha na Tanzania?

Karibuni kwa mawazo ya kuunga mkono au kupinga hii mada kwa ushahidi dhahiri.
 
Kuna wakati mwingine huwa wasomi wetu, wananishangazaga sana, sana. wanakuja na Conclusion ambayo kiukweli inashangaza sana...
 
Tanzania unakuta jitu linaitwa Professor lakini matendo yake bora yule asiyesoma hata vidudu.. Tz hakuna wasomi kuna wachumia tumbo.
 
Subiri shambulizi. Ukweli unajulikana ila watasema mwendazake aliharibu ubongo wako
Nipo tayari kupokea shambulizi lolote, ila nachohitaji ni kuambiwa ukweli tu maana tusiwe tunakurupuka tu
 
Nipo tayari kupokea shambulizi lolote, ila nachohitaji ni kuambiwa ukweli tu maana tusiwe tunakurupuka tu
Kumbe kuna mtu anashambuliwa, kwann wasikamatwe tunasubiri kushambuliwa?
 
Wameandika report vitabu kibao ili watuchanganye nina mashaka hizi scholarship na sponsorship nyingi zina agenda wanaandaa mawakala ili wakiliamsha dude kwa style ya usomi basi msomi anajiona bila kusupport atajishusha ndicho hiki kilichofanyika na huenda hiyo report wameandikiwa na wenye agenda zao
 
Tanzania ni nchi pekee duniani ambayo haijachanja raia wake chanjo ya covid-19 mpaka sasa.
Nchi nyingi duniani zimechanja raia wake chanjo ya covid-19.
SWALI:
Je kimadhara na faida, kuna tofauti gani kati ya Tanzania na hizo nchi zilizochanja watu wake?
Je Tanzania watu wamekufa sana na covid-19 kuliko India, Africa kusini, Italia e.t.c?
Je kiuchumi Tanzania imeathirika kwa kiwango gani?
Labda tujilinganishe na Kenya au Uganda...nani ameathirika na janga la covid-19 ukilinganisha na Tanzania?
Karibuni kwa mawazo ya kuunga mkono au kupinga hii mada kwa ushahidi dhahiri.
Tutamkumbuka
 
Hili mama kalifanya kwa aliji ya Mahujaji (kumbuka Saudia wametangaza kua HawaPokei Mahujaji wasio Pata chanjo) ndio maana chanjo itakua sio ya lazima.
 
Tofauti ni kubwa sana, kwanza nchi inayotoa chanjo raia wake anakuwa free on travel akiwa na kadi ya uthibitisho.

Wewe mbongo utapata tabu sana, hutoweza kutoka hapo kwenu kwenda popote, labda RUSHWA ya kadi za corona kama ipo utatoka.

KUMBUKA: Binkubwa na ile tume wamefanya hivyo makusudi ili kuwalinda watz flani watakaokuwa na route nje ya nchi.

NB: Muda si mrefu bila kadi hutoki nchini mwako, kama ilivyo yellow fever!.
 
Tofauti ni kubwa sana, kwanza nchi inayotoa chanjo raia wake anakuwa free on travel akiwa na kadi ya uthibitisho.

Wewe mbongo utapata tabu sana, hutoweza kutoka hapo kwenu kwenda popote, labda RUSHWA ya kadi za corona kama ipo utatoka.

KUMBUKA: Binkubwa na ile tume wamefanya hivyo makusudi ili kuwalinda watz flani watakaokuwa na route nje ya nchi.

NB: Muda si mrefu bila kadi hutoki nchini mwako, kama ilivyo yellow fever!.
Kwahiyo kelelezote hizo ni chanjo tu na siyo mikakati ya Jumla ya kupambana na covid-19? Basi sawa
 
Huwezi kupata jibu, sanasana naona wapinzani wanafurahia chanjo eti kwa kuwa wanamkomoa Magufuli.
 
Huwezi kupata jibu, sanasana naona wapinzani wanafurahia chanjo eti kwa kuwa wanamkomoa Magufuli.
Magufuli alishamaliza kazi yake na wala hajui nini kinaendelea Tanzania, tuliobaki hai ndiyo wa kujiuliza maswali magumu. Je ni kweli sisi Tanzania tumeathirika sana na corona ukilinganisha na nchi ambazo zimewachanja raia wake?
 
Ujinga mwingine huhitaji PhD ili kujua tofauti . Tanzania hakuna adhali full stop.
Vingine wachomane wenyewe kwa wenyewe ili roho zao zifurahi.
Kwakweli
 
Sasa tutafanyaje comparison bila kua na takwimu toka Tz?

Hizo nchi ulizozitaja kama India,South Africa na Italia wao wanatoa takwimu za idadi ya vifo,so kufanya comparison ni lazima tuwe na takwimu za nchi zote ulizozitaja,

Kuhusu madhara ya kiuchumi, hii sio issue ya mtu tu kutoa maoni yake hapa JF bali matokeo ya kujua athari za kiuchumi yatapatikana kwa kufanyiwa tafiti na mamlaka husika.
 
Sasa utajuaje kama umeathirika sana Kama ugonjwa wenyewe unakuja kwa mpito alafu unapotea na mkikaa mkajisahau mara unakuja ghafla unakomba watu kiasi na kuuguza wengine unapotea tena Sasa hapo bila kuwa na taadhali huoni unaweza kuja vibaya na kuleta madhara màkubwa? Kinga ni Bora kuliko tiba hivyo lazima tuchukue taadhali mapema na mshaambiwa kuchanjwa siyo lazima, kwani mbona kuna uzazi wa Mpango wale wasiotaka kutumia huwa hawatumii wanafyatua tu lakini dawa zipo kwa taadhali na wale watakaotaka kutumia wasikwamishwe kwa kukosa dawa.
 
Back
Top Bottom