Je, kuna ukweli kuwa mtu anaweza kumbadilisha mtu mzima?

Je, kuna ukweli kuwa mtu anaweza kumbadilisha mtu mzima?

Kwahiyo kubadilisha mavazi ni stupidity?
Na wakati ananiambia hayo hatukuwa hata na mwezi mmoja wa mahusiano kusema nilimpenda mpaka anibadilishe mavazi ni uwongo, Mimi tu napenda twende sawa kwenye mahusiano na ndio maana nikasema kama kitu kipo ndani ya uwezo wangu nafanya,kama hakipo sitafanya na hio ni makubaliano tu sio mapenzi.
hukubadilishwa bali ulibadilika wewe mwenyewe bcz u were in love, and u wanted to make him happy, women do a lot of stupid things when they r in love tofauti na wanaume
 
Kubadilisha addiction ni kazi ngumu sana mtu akishakuwa addicted kumtoa huko kunahitaji nguvu za ziada au aamue mwenyewe baada ya kumkuta ya kumkuta.

Sent using Jamii Forums mobile app
sure mamie uko sawa kabisa katika hili,na ndio ambacho hata mimi huwa naamini pia, maanake i was in love with an alcoholic and he was in love with me as well,ila i tried all my best to make him stop his alcohol addiction but he never stoped mpaka akafikia hatua ya kufa just because of alcoholism,from then sijawahi kukubaliana na swala la kumbadilisha tabia au aina ya Maisha ambayo mtu mzima amechagua kuishi mpaka aamue mwenyewe.
 
ha ha ha mkuu maisha umbadilisha mtu

katika NDOA ukiupita mwaka wa kwaza wa matatizo na vikwazo mkaushinda mwaka wa tatu wakuchokana na kuzoeana mkapiga mwaka wa tano mnavumilia 7bu mnalea tu watoto bila hvyo mngeachana
mkishaingia mwaka wa 7 basi hapo mnakuwa mwili mmoja ata mkigombana hauishi mwenzi mnarudiana na hata mkiachana kabisa hakuna atakatepata mbadala wa mwenzie mtatafutana tu au mawazo juu ya mwezie hataushi kichwani
hvyo mkuu ndoa sio FURAHA km wengi wanavyoamini ukioa au kuolewa wewe ni kuserebuka tuu
NDOA ni maisha km unavyoishi wewe huvi hapo sasa hvi hizo changamoto unazokumbana nazo katika maisha yako na unapigana nazo ndio NDOA ipo hivyo mkuu hvyo mengne inabidi ufumbe macho upambane nayo ukubaliane nayo
7bu huyo mwenye tabia unazotaka hakuvutii hata na humpendi
lkn huyo mwenye tabia za hovyo ndo yupo moyoni mwako na unampenda hasa
katika VITABU VITAKATIFU vinasema OENI katika mnaowapenda
na mm nakazia OA mkuu unayempenda 7bu utamvumilia

Sent using Jamii Forums mobile app
mkuu unatema madini ya hatari sana mpaka nahisi ka una uzoefu katika sekta hii

ujue mkuu sikatai kuwa kwenye ndoa sio paradiso,lakini mkuu ujue kuna vile vijimambo vidogo vidogo ambavyo kila binadamu anavyo kutokana na kutokamilika ambavyo tunapaswa kuendela kuvumiliana na wenzi wetu wa ndoa ili Maisha yasonge na haviepukiki,lakini mkuu kuna vile ambavyo ni sumu ya ndoa,hata neno uvumilivu ni vigumu sana kupenyeza kwenye ndoa inayokabiliwa na mambo hayo kama ulevi wa kupindukia,umalaya uwongo uchonganishi n.k hata umpende mtu vipi mambo kama haya ni sumu kwa ndoa na uvumilivu wa ziada unahitajika kudumu au kuendela kukaa katika ndoa yenye vitu kama hivyo
 
Mie bado sijawahi kukutana nalo hilo jambo
okay sawa mkuu @Hajto,lakini vipi mkuu umekuwa ukifikiria vipi kichwani mwako? umewahi kufikiria inawezekana kumdalisha mtu mzima aache tabia Fulani mbaya zisizopendeza?umewahi kushuhudia kwa jirani,rafiki au hata ndugu ambaye amewahi kukumbana na changamoto hii?
 
MIMI nina mtazamo tofautu kidogo naamini hakuna tabia za kurithi bari kile mtoto anachojifunza tangu anazaliwa
mfn mtoto tangu akiwa tumboni katika wiki ya 32 anaanza kusikia km nyimbo zinazoimbwa radion mnavyoongea inamaana hadi siku anazaliwa tayari kuna sauti anakuwa amezizoea baada ya sauti sasa unafatia harufu 7bu bado hajaanza ona ndo mana mtoto ukimshika wew analia lkn akipewa mamaake akisikia ile harufu ya ziwa anapoa akishaaza kuona anaanza mazoea sasa kwa wazazi na watu wa karibu kisha mazingira ya nyumbani baadae kabisa akiweza toka mwenyewe kwenda nyumba ya jirani anaanza kujifunza ya dunia sasa
hvyo binadamu kadili anavyokua anayojifunza na kukumbana nayo ndo yanambadilsha katika kila lika analopitia na jinsi mnavyomchukulia au jamii inavyomchukulia ndivyo huakisi tabia yake
mfn mtoto inafika hatua ananijua kabisa sisi kwetu hoehae au mm yatima sina wazazi naishi kwa mjomba hvyo mara nyingi tabia huendana na mazingira
ndo mana unaweza kuta tabia ya mtoto fulani nzuri sana mkalimu nk 7bu anajijua yeye yatima na km unavyojua YATIMA HADEKI
akapitia manyanyaso yakambadilisha
lkn utakuta toto wale kina JUNIOR hovyo kabisa kutokana na linavyolelewa

hvyo athari za kitabia au hizo hulka zinatokana hatua za ukuaji anazopitia mtoto sio kusema kurithi au yeye alivyo bali ni vile tu maisha anayokumbana nayo
mfn mama malaya abaushi na mtoto wa kike na kila siku mauncle wapya hata yeye akikua anaona kawaida kubadili wanaume
au baba mlevi anapiga mama mtoto anaona naye akikua nae anaona kawaida
lkn baba mlevi anapiga mama lkn mtoto anaishi kwa bibi na babu ambao watu wa dini maadili mema sasa ataanzaje kuwa mlevi eti amrithi babayake na hakuna mazingira ya ushawushi hivyo
wakurya ni majasili kutokana na makuzi yao lkn mtoto mkurya akazaliwa nzanzibar akajulia nzanzibar lazima atakuwa na tabia za wanzanzibari hata lafudhi itabadilika pia

mm bwana kulikuwa na rafiki ingawa si wa karibu tulisoma wote msingi kwa kweli alikuwa mpole mkarimu na alikuwa yuko vizuri kichwani kupita viwango kiasi hadi walimu walikuwa wanampenda tulipoteana miaka mingi siku nakuja kutana nae mkoani ni deleva malori aisee kwa mademu sijapata ona na anapenda kubet kinoma yaan hvyo ni mambo tu ambayo maisha yanaambadilisha mtu
hvyo hakuna kinachoshindikana ikiwa huyo mtu mwenyewe mpo katika mazingira gani kwa sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu naomba kwanza niadmit uko vizuri,

lakini mkuu hivi umewahi kujiuliza kwamba ni kwa nini kwenye hizi taasisi mbalimbali za elimu say jeshini,taasisi za uongozi,taasisi za sharia madaktari,mnakuwa wengi mnasoma kitu kile kile lakini huwa wanakuwepo the best? kwa nini kumekuwa na viongozi ambao wameumiza vichwa watu wengi kwa miaka na wamewekwa kwenye rekodi kama viongozi bora kuwa hi kutokea? mfano akina Nelson Mandela,Kina Nkwamhe Nkurumah akina Nyerere?

binafsi huwa naamini kuna zile tabia ambazo mtoto anakuwa nazo ndani yake,yaani make up yake,mtu anakuwa kiongozi by nature,au mtetea haki by nature from akiwa mtoto na unakuta wazazi wake hawako hivyo ila hata wao wakimuona mtoto na Maisha yake ya kila siku wanajikuta wanajisema katakuwa kakiongozi haka,katakuwa kanasheria sikumoja haka na mambo kama hayo

lakini pia mkuu hujawahi kuona familia say ya kitajiri full madharau ubaguzi lakini wanatokea watoto wawili au mmoja ambao wako tofauti kabisa na tabia ya familia nzima?

au kijana ambaye anachukizwa na tabia ya baba yake mlevi anayepiga mke,lakini yeye akikua mambo yanakuwa tofauti na anakuwa mtu anayempenda mke wake na kuitunza familia yake?

kikukweli haya mambo yanachanganya sana mkuu.
 
okay sawa mkuu @Hajto,lakini vipi mkuu umekuwa ukifikiria vipi kichwani mwako? umewahi kufikiria inawezekana kumdalisha mtu mzima aache tabia Fulani mbaya zisizopendeza?umewahi kushuhudia kwa jirani,rafiki au hata ndugu ambaye amewahi kukumbana na changamoto hii?
Kuwezekana inawezekana ila itakuchukua muda sana,kwenye hilo nimewahi kuona
 
Kuwezekana inawezekana ila itakuchukua muda sana,kwenye hilo nimewahi kuona
unaweza kutusimulia ulichokion mkuu? ili tujue kama inawezekana ni kwa kutumia mbinu zipi na kwa tabia zipi na kwa muda gani? na je huko mbeleni mtu huwa harudii matapishi yake?
 
unaweza kutusimulia ulichokion mkuu? ili tujue kama inawezekana ni kwa kutumia mbinu zipi na kwa tabia zipi na kwa muda gani? na je huko mbeleni mtu huwa harudii matapishi yake?
Unajua kubadilika kwa mtu kunategemeana vitu vingi kwa uyo mwenye kumbadilisha mtu,Nakumbuka kuna kijana mmoja alikuwa ni msela sana tena alikuwa anauza bangi,basi akampata bint mmoja basi alimbadirisha alibadirika hadi mwishoni wakafunga ndoa,yule jamaa leo hii ukijakutana nae huwezi dhania kabisa
 
Back
Top Bottom