Je, Kuna ulazima mwanamke abadili jina baada ya kuolewa?

Je, Kuna ulazima mwanamke abadili jina baada ya kuolewa?

kwanini kumepitwa na wakati?
Ila labda tuseme mwanamke na mwanaume wanaoana.

Thats exactly my point.Ukiaddress issue ya nani anabadili jina bila kuangalia structure nzima ya ndoa, utakuwa unampa dawa ya kikohozi mtu mwenye TB, unaaddress symptoms badala ya kuangalia ugonjwa wenyewe.

Kwa nini mwanamke anachukua jina la ukoo wa mwanaume? Kwa sababu mwanamke "anaolewa".S asa hata ukibadilisha asichukue jina la ukoo wa mwanaume, lakini akabaki "anaolewa" unakuwa hujabadili kitu kikubwa, ni cosmetic change tu kama CCM ilivyosema inaleta siasa ya vyama vingi kwa kubadili sentensi chache katika katiba bila kufanya institutional changes (sorry I had to inject a political example, however relevant it still has the potential explosive nature that could possibly derail us, I hope not)

But the bigger point is, ndoa tuiangalie kama partnership ya equals, tukiweza hili haya mambo ya majina yataondoka yenyewe, au hata kama yatabaki yatakuwa mainly symbolic.

Lakini kwa structure ya sasa ambapo mwanamke "anaolewa", hata kama tukifanya kila mtu abaki na jina lake, mwanamme akaendeleza mfumodume, tutakuwa hatujabadili chochote cha msingi.

Lakini wanawake nao wakae wakielewa "Noblesse Oblige".
 
Thats exactly my point.Ukiaddress issue ya nani anabadili jina bila kuangalia structure nzima ya ndoa, utakuwa unampa dawa ya kikohozi mtu mwenye TB, unaaddress symptoms badala ya kuangalia ugonjwa wenyewe.

Kwa nini mwanamke anachukua jina la ukoo wa mwanaume? Kwa sababu mwanamke "anaolewa".S asa hata ukibadilisha asichukue jina la ukoo wa mwanaume, lakini akabaki "anaolewa" unakuwa hujabadili kitu kikubwa, ni cosmetic change tu kama CCM ilivyosema inaleta siasa ya vyama vingi kwa kubadili sentensi chache katika katiba bila kufanya institutional changes (sorry I had to inject a political example, however relevant it still has the potential explosive nature that could possibly derail us, I hope not)

But the bigger point is, ndoa tuiangalie kama partnership ya equals, tukiweza hili haya mambo ya majina yataondoka yenyewe, au hata kama yatabaki yatakuwa mainly symbolic.

Lakini kwa structure ya sasa ambapo mwanamke "anaolewa", hata kama tukifanya kila mtu abaki na jina lake, mwanamme akaendeleza mfumodume, tutakuwa hatujabadili chochote cha msingi.

Nakubaliana nawe kabisa...
Miaka ya nyuma, watu walikuwa wanaona kuwa mwanamke anaolewa na mwanaume anaoa.Misemo pia iliunga mkono dhana hii ukiachilia mbali mila na desturi kama za mwanaume kumlipia mahari mwanamke na hivyo kugeuza kuwa " mali" yake kwa kila hali.Hii ilipelekea hata ugomvi mkbwa pale mwanamke alipokataa kuchukua jina la mume.
Siku hizi polepole dhana ya kuoana inakubalika zaidi, na hata wanawake wanabaki na ubini wa alikotoka..akipenda anaongeza ubini wa mume huko mwisho.
 
Huu mjadala umekuwa mrefu ila ni mzuri ningependa kuchangia......

inawezekana ni mtazamo wangu ila nilikuwa naamini kuwa kwa mwanamke kubadili jina akishaolewa ni ishara kuwa anakupenda na amekukubali wewe uwe kiongozi wa familia yake (kama ambavyo alikubali baba yake mzazi kuwa kiongozi wake kabla hajaolewa). ingawaje ni kitu cha kurithi lakini maana yake huwa inabadilika kizazi kwa kizazi.

Hivyo basi mwanamke wa leo akibadili jina na kumfuata mumewe kwangu mie nalichukulia kama ishara ya upendo na kamwe si utumwa au kujidhalilisha kama tu ilivyo kwa mke kumfulia mume underwear (si kwa kuwa ni kazi yake kama mke bali anaweza amua kufua au kuacha isipokuwa kama anampenda sana mumewe na hapendi kumwona akiteseka kufua)

Nawakilisha


MwanajamiiOne Nimekupenda kwa hii post yako....tunahitaji kufikiria zaidi ya kiboksi cha ubeijing na kuoa au kuolewa! wata wanataka kuitangua torati wakati huu na madhara yake yanaonekana!
 
Nadhani zamani wanawake ilikuwa ni rahisi kubadilisha jina kwasababu walikuwa wanaolewa mapema (early twenties or still in college). Siku hizi wengi wanaolewa in their mid twenties and above na unakuta they are already known professionally by their sir names. Hivyo wanaona ni process ndefu ya kuanza kutumia jina lingine.

Either way, I think its a personal choice. What I dont understand are the 'Jolie-Pitts' of this world. I always wonder what will happen when their daughters get married by say a Mr John. Will their names be Jolie-Pitt-John?
 
Nikawaida mwanamke kubadili jina baada ya kuolewa,lakini pia wapo wanawake walioolewa ambao hadi leo wanatumia majina ya wazazi wao. Niliongea na baadhi ya watu,walisema yafuatayo:
1. ASHA WA MAGALA KIMBANGULILE ALISEMA.' Mr Tall unasemaje? eti nini? nibadili jina,mmmmh,mzazi wangu kanilea,kanipeleka shule, nafanya kazi,mshahara wangu mkubwa kuliko wa mume wangu,halafu ooooooh sijui badili jina,labda abadili yeye atumie jina la baba yangu,KWA TAARIFA YAKO HAKUNA WA KUBADILI JINA HAPA,TENA UISHIE USINICHEFUE.
2.JOHN WA MBEZI KWA MSUGURI ALISEMA: Nikinunua gari nabadili jina na kutumia jina langu.Nikinunua shamba naandika jina langu,mimi ni msukuma,nimelipa ng'ombe nyingi sana wakati naoa kama mahari,halafu mjinga mmoja aseme nisibadili jina,loooh hapo nimeoa sijaoa?JINA LAZIMA LIBADILISHWE.
3.JANE WA TANDIKA YOMBO KWA MAGURUWE ALISEMA: 'kubadili jina ni heshima,imeandikwa.....atamwacha mama yake na baba yake nao watakuwa mwili mmoja. kubadili jina inaonyesha umoja, mimi ni wake.
4.HEMEDI WA GONGO LA MBOTO MONGO LANDEGE ALISEMA:'Mimi sijaoa,nikioa si lazima mke abadili jina kwa sababu:
a)Ninacho jali ni upendo,heshima,amani na ushirikiano, jina nini bwana.
b)Kuna watu wana majina ya ajabuajabu na mabaya,mfano mtu anaitwa kibaka.Akioa, mke anaacha jina zuri la kwao,anaitwa mrs kibaka loooh.Si uonevu huu?
c)Halafu ngoja nikunong'oneza bwana Tall,jina mkeo asibadili maana mkiachana mali zote ni zako, zina jina lako.
d)Leo nimeoa,mke ataitwa mrs Hemedi,bahati mbaya nimekufa baadae mke wangu akiolewa itabidi abadili jina mara ya pili,halafu huyo jamaa akimpiga chini,akaolewa tena,pia abadili jina mara ya tatu? atakuwa na majina mangapi? ni upuuzi tu.MKE ASIBADILI JINA FULLSTOP.
NB: MAJINA YALIYOTUMIKA SIYO YA WAHUSIKA HALISI
mwana JF wewe unasemaje?jina libadilishwe lisibadilishwe?
 
kubadili jina ni mapendekezo ya mtu binafsi sio lazima. kwani ukishabadili kutoka kwenye hilo jina ni ngumu sana
 
Binafsi sioni sababu kubwa na ya msingi ya mama kubadili jina baada ya kuolewa rasmi. Nadhani hii ilizoeleka zamani enzi hizo when a man was everything and anything. Bahati mbaya sioi ila kama ningeoa nisingekubali my wife abadili jina eti kwakuwa amekuwa mrs mimi. Ni mfumo dume tu!
 
Nadhani kwa akina dada kutoka familia zenye majina ambayo yamekuwa attached kwenye mambo ya ufisadi na kuongelewa sana hapa Tanzania pale watakapo olewa lengo na nia ya kubadilisha majina yao na kuchukua ya upande wa mwanaume inaongezeka.
 
Mie naona ni maajabu mtu kuukwepa uko wawazazi wake kisa? Saa nyingine maukoo ya watu yana milaana nawewe unaenda kujipachika huko kwangu mimi nimegoma nahakuna ubaya wowote najivunia sir name yangu nasiwezi kuuacha ng'ooooo
 
Back
Top Bottom