Je, kupanda kwa bei ya vyakula kumezaa tabaka la wakulima na wananchi?

Je, kupanda kwa bei ya vyakula kumezaa tabaka la wakulima na wananchi?

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,019
Reaction score
6,825
Nimeona katika mijadala yetu kuhusiana na kupanda kwa bei ya vyakula kumezaa tabaka la wakulima (ambalo halitajwi wala kuonewa huruma) na la wananchi (ambalo linatajwa na kuonewa huruma).

Ningependa kuchangia kwa kusema na kumbusha kuwa, hakuna namna yoyote ya kupata chakula bila kulima kwa hiyo yeyote anayejadili chochote kuhusu chakula asimpomtaja mkulima anajilaani.

326952355_1145181609513696_3377592121893390780_n.png


Kwa mda mrefu wakulima wamekuwa wakipunjwa sana bei ya mazao yao, sasa hilo limefika mwisho baada ya serikali kupanua soko. Mkulima sasa anapata bei ya haki na sahihi ya kumuwezesha kurudisha gharama za uzalishaji na kubaki na faida. Hii inafuata misingi ya SOKO LA HAKI (FAIRTRADE).
images

Untitled%20design-37.png
 
Hilo ni tatizo la sera mbovu ya kufungua nchi wafanyabishara wakubwa walihifadhi mahindi wauze ndani ghafla wanaruhusiwa kuuza nje wanakimbilia huko nje kwe bei nzuri

USSR
 
Kuna tofauti kati ya wakulima na wafanyabiashara wa mazao.

Anyways, lawama zote ziende kwa serikali, si mkulima wala mfanyabiashara.
 
Nimeona katika mijadala yetu kuhusiana na kupanda kwa bei ya vyakula kumezaa tabaka la wakulima (ambalo halitajwi wala kuonewa huruma) na la wananchi (ambalo linatajwa na kuonewa huruma).

Ningependa kuchangia kwa kusema na kumbusha kuwa, hakuna namna yoyote ya kupata chakula bila kulima kwa hiyo yeyote anayejadili chochote kuhusu chakula asimpomtaja mkulima anajilaani.

326952355_1145181609513696_3377592121893390780_n.png


Kwa mda mrefu wakulima wamekuwa wakipunjwa sana bei ya mazao yao, sasa hilo limefika mwisho baada ya serikali kupanua soko. Mkulima sasa anapata bei ya haki na sahihi ya kumuwezesha kurudisha gharama za uzalishaji na kubaki na faida. Hii inafuata misingi ya SOKO LA HAKI (FAIRTRADE).
images

Untitled%20design-37.png
Acha porojo wewe. Wanufaika wa kupanda maradufu kwa bei za chakula, ni wafanyabiashara wa kati! Na siyo wakulima, ambao mpaka leo bado wana maisha magumu kutokana na sera zenu mbovu.

Maana hao wakulima unaojaribu kuwasemea hapa, kitambo walishauza mazao yao kwa bei ya hasara; mara tu baada ya kuvuna kutokana na ukosefu wa vifaa vya kuhifadhia, na pia kwa kurubuniwa na hao wafanyabiashara wasio waaminifu.
 
Kuna tofauti kati ya wakulima na wafanyabiashara wa mazao.

Anyways, lawama zote ziende kwa serikali, si mkulima wala mfanyabiashara.
Siku zote nilifikiri Hussein Bashe ni kijana mwerevu! Kumbe hamna kitu. Huku kupanda mara dufu kwa bei za chakula, kunawanufaisha zaidi wafanyabiashara wa hayo mazao ya chakula!

Na wala siyo wakulima waliouza hayo mazao yao kwa bei ya shambani.
 
Acha porojo wewe. Wanufaika wa kupanda maradufu kwa bei za chakula, ni wafanyabiashara wa kati! Na siyo wakulima, ambao mpaka leo bado wana maisha magumu kutokana na sera zenu mbovu.

Maana hao wakulima unaojaribu kuwasemea hapa, kitambo walishauza mazao yao kwa bei ya hasara; mara tu baada ya kuvuna kutokana na ukosefu wa vifaa vya kuhifadhia, na pia kwa kurubuniwa na hao wafanyabiashara wasio waaminifu.
Nenda na uhalisia tembelea vijijini utapata majibu ya umbumbumbu wako. Karagwe na Kyerwa ndizi zilikuwa zinaozea shambani wananunuzi wa kati wakinunua kwa malingo mkungu kati ya 3 na 5,000 as we speak mkungu sasa ni 15,000 ukitoa unakata mwenyewe mkulima akipiga mluzi. Sikiliza mkuu nyinyi wananchi kama mnataka chakula kwa gharama nafuu at the expenses ya mkulima kwa kitisho cha kukukataa kuichagua CCM sisi wakulima tuwambie kabisa tutasimama na CCM.
 
Siku zote nilifikiri Hussein Bashe ni kijana mwerevu! Kumbe hamna kitu. Huku kupanda mara dufu kwa bei za chakula, kunawanufaisha zaidi wafanyabiashara wa hayo mazao ya chakula!

Na wala siyo wakulima waliouza hayo mazao yao kwa bei ya shambani.
Unajidanganya bei ya mahindi ya mkulima imepanda na wakulima wanafurahia. CCM OYEEEE
 
Wakulima tumefikiwa, tuacheni jamani na sisi tuna watoto wanatuangalia na kilimo ndio biashara yetu. Wakati wa kupata faida umefika...kwenye hasara hamkutupigia makelele ya kutuonea huruma
 
Huwezi tenganisha wakulima na wananchi. Nchi ambayo watu wengi ni wakulima, wananchi=wakulima.
 
Acha porojo wewe. Wanufaika wa kupanda maradufu kwa bei za chakula, ni wafanyabiashara wa kati! Na siyo wakulima, ambao mpaka leo bado wana maisha magumu kutokana na sera zenu mbovu.

Maana hao wakulima unaojaribu kuwasemea hapa, kitambo walishauza mazao yao kwa bei ya hasara; mara tu baada ya kuvuna kutokana na ukosefu wa vifaa vya kuhifadhia, na pia kwa kurubuniwa na hao wafanyabiashara wasio waaminifu.
Mimi mkulima,ndiyo nauza mpunga wangu muda huu kwa Bei ya laki unusu,hizo habari za wafanyabiashara wa kati mmekaririshana tu,mkulima wa Leo siyo wa 70,80,90s huko,wake ya,wanyaruanda tunawapimia kwa kilo Kisha fedha zinabadili mikono,hakuna mtu wa kati labda mbele kwa mbele huko
 
Hilo ni tatizo la sera mbovu ya kufungua nchi wafanyabishara wakubwa walihifadhi mahindi wauze ndani ghafla wanaruhusiwa kuuza nje wanakimbilia huko nje kwe bei nzuri

USSR
Tusipokuwa makini wafanyabiashara wanaweza hata kufyonza kwenye maghala ya umma wakapeleka nje ya nchi ilhali walipakodi wanataabika kwa njaa.
 
Huwezi tenganisha wakulima na wananchi. Nchi ambayo watu wengi ni wakulima, wananchi=wakulima.
Kwangu mie wakulima siyo sawa na wala haimaanishi wananchi hasa kwenye hili la kupanda kwa bei ya vyakula
 
Kwangu mie wakulima siyo sawa na wala haimaanishi wananchi hasa kwenye hili la kupanda kwa bei ya vyakula
Hilo haliondoa ukweli kuwa unapoongelea wananchi TZ, unaongelea wakulima .
 
Nadhani sasa tunaelekea katika njia sahihi kabisa ispokuwa tu, kuna mipaka fulani fulani ambayo ni lazima iwe na rungu lake, alerts zake mbalimbali za kuijulisha mfano, ni lazima tufahamu nje na akiba ya taifa, je ni tani ngapi zinatakiwa ziwepo katika mzunguko ndani ya nchi,
Kwenye akiba tuna ngapi?, zinazozunguka ndani ya nchi zinatakiwa ziwe tani ngapi, na za kutoka nje kwa masoko ziwe tani ngapi, we must have a limitations for our citizens.
 
Nadhani sasa tunaelekea katika njia sahihi kabisa ispokuwa tu, kuna mipaka fulani fulani ambayo ni lazima iwe na rungu lake, alerts zake mbalimbali za kuijulisha mfano, ni lazima tufahamu nje na akiba ya taifa, je ni tani ngapi zinatakiwa ziwepo katika mzunguko ndani ya nchi,
Kwenye akiba tuna ngapi?, zinazozunguka ndani ya nchi zinatakiwa ziwe tani ngapi, na za kutoka nje kwa masoko ziwe tani ngapi, we must have a limitations for our citizens.
Naunga mkono hoja
 
Back
Top Bottom