Je, kusahau ndoto uliyoota muda mfupi kabda ya kuamka huwa ni kawaida?

Je, kusahau ndoto uliyoota muda mfupi kabda ya kuamka huwa ni kawaida?

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2017
Posts
10,559
Reaction score
19,101
Habari za Jumatatu wana JF

Kwa ninavyoelewa ndoto zina maelezo tofauti kwa watu tofauti. Kuna fikra kadhaa lakini kubwa ni mbili

Fikra(school of thought) ya kwanza wanasema ndoto ni matokeo ya mawazo yako au mambo unayoyafikiria sana au marudio ya vitu ambavyo ulishawahi kuvifanya zamani

Wanachukulia ubongo wa binadamu ni kama Processing Unit ya computer ambayo hata ikizimwa inaweza kua anajipangia yenyewe ma file yake vizuri bila kua operated na mtu

Fikra ya pili ni wale wanaosema ndoto ni jambo la kiimani(spiritual) na huwa ni ujumbe unaokwambia kuhusu habari zijazo au taarifa ya kitu kilichotokea au kitakachotokea katika ulimwengu wa kiroho kiwe kizuri au kibaya na ambacho kitaweza kutokea au hata kisitokee katika ulimwengu halisi

Mimi sina ujuzi wa lolote katika hayo mawili lakini kuna mambo kadhaa yalishawahi kutokea kwangu kama ndoto na baadae yakatokea kwenye ulimwengu halisi

Mimi ni shabiki lialia wa Simba SC. Mwezi July mwaka huu niliota ndoto na immediate baada ya kuamka nikaisahau na sikuikumbuka mpaka siku mbili kabda ya Simba kucheza na wale Wabotswana ile mechi ya ugenini Lunyasi walioshinda 2-0

Niliota tumepigwa goli tatu na tumetupwa nje ya mashindano. Nilipuuza nikijua ni ndoto za Ali bin Nacha tu. Tena baada ya matokeo ya mechi ya kwanza ndio kabisaa nikapuuza. Kilichokuja kutokea baadae kinajulikana!!!!

Hoja na swali langu ni kwamba? Kwanini mtu unaweza ukaota ndoto ndeeefu kama sinema halafu mara tu ukiamka kutoka usingizini unajikuta umeisahau? Kama kuikumbuka inaweza ikawa siku nyingine kabisa

Nauliza swali hili kwa wale wote wenye fikra tofauti tofauti kuhusu kuota ndoto kwa binadamu. Huu usahaulifu wa ghafla kwa kitu kilichokutokea sekunde chache zilizopita upo kwenye sayansi ipi na nini maelezo yake?
 
Mimi nilipopata ajira yangu ya kwanza Mbeya huko mwaka 2003,siku tatu kabla ya kureport niliota mazingira ya kazi na Hadi nyumba nitakayofikia accurately kabisa siku niliyofika nikashangaa mbona kama hii sehemu nilishawahi kufika!? Nikakumbuka ni ndoto niliyoiota. Nahisi ubongo wa binadamu upo designed kufanya kazi extra mile kuliko jinsi tunavyoutumia.
 
Mimi nilipopata ajira yangu ya kwanza mbeya huko mwaka 2003,siku tatu kabla ya kureport niliota mazingira ya kazi na Hadi nyumba nitakayofikia accurately kabisa.siku niliyofika nikashangaa mbona kama hii sehemu nilishawahi kufika!?nikakumbuka ni ndoto niliyoiota.Nahisi ubongo wa binadamu upo designed kufanya kazi extra mile kuliko jinsi tunavyoutumia
Kwahiyo watu wanaosema ndoto ni spiritual wanaweza wakawa na hoja
 
Habari za Jumatatu wana JF

Kwa ninavyoelewa ndoto zina maelezo tofauti kwa watu tofauti. Kuna fikra kadhaa lakini kubwa ni mbili

Fikra(school of thought) ya kwanza wanasema ndoto ni matokeo ya mawazo yako au mambo unayoyafikiria sana au marudio ya vitu ambavyo ulishawahi kuvifanya zamani

Wanachukulia ubongo wa binadamu ni kama Processing Unit ya computer ambayo hata ikizimwa inaweza kua anajipangia yenyewe ma file yake vizuri bila kua operated na mtu

Fikra ya pili ni wale wanaosema ndoto ni jambo la kiimani(spiritual) na huwa ni ujumbe unaokwambia kuhusu habari zijazo au taarifa ya kitu kilichotokea au kitakachotokea katika ulimwengu wa kiroho kiwe kizuri au kibaya na ambacho kitaweza kutokea au hata kisitokee katika ulimwengu halisi

Mimi sina ujuzi wa lolote katika hayo mawili lakini kuna mambo kadhaa yalishawahi kutokea kwangu kama ndoto na baadae yakatokea kwenye ulimwengu halisi

Mimi ni shabiki lialia wa Simba SC. Mwezi July mwaka huu niliota ndoto na immediate baada ya kuamka nikaisahau na sikuikumbuka mpaka siku mbili kabda ya Simba kucheza na wale Wabotswana ile mechi ya ugenini Lunyasi walioshinda 2-0

Niliota tumepigwa goli tatu na tumetupwa nje ya mashindano. Nilipuuza nikijua ni ndoto za Ali bin Nacha tu. Tena baada ya matokeo ya mechi ya kwanza ndio kabisaa nikapuuza. Kilichokuja kutokea baadae kinajulikana!!!!

Hoja na swali langu ni kwamba? Kwanini mtu unaweza ukaota ndoto ndeeefu kama sinema halafu mara tu ukiamka kutoka usingizini unajikuta umeisahau? Kama kuikumbuka inaweza ikawa siku nyingine kabisa

Nauliza swali hili kwa wale wote wenye fikra tofauti tofauti kuhusu kuota ndoto kwa binadamu. Huu usahaulifu wa ghafla kwa kitu kilichokutokea sekunde chache zilizopita upo kwenye sayansi ipi na nini maelezo yake?
Kifupi sana;
Ukiota ndoto, then ikasahaulika immediately unapotoka ucngzini, ujue Kuna Jambo la kwel na hakika linstukia very soon, kwa hyo ujumbe huo unakua hacked spiritually ili usijue kinachoendelea!!

Kwama hutojal, imekupasa kumwomba Mungu akurudishie ndoto hyo!!

Zaidi soma kitabu cha Daniel, utakutana na scenario ya namna hyo ambapo mfalme nebkadneza aliipata, akalazika kuwashurutisha wachawi na manabii wa kichawi wamweleze aliota ndoto gani na tafsir yake ni nini, na waliposhindwa aliwaangamiza , akawaamuru akina Daniel kwa namna hyohyo, ambao wao walifunga na kuomba na Kisha Mungu akawapa ndoto na tafsir yake.
 
Naamini ndoto ziko kiimani zaidi,Mambo mengi niyafanyayo bila ndoto huwa Sina uhakika wa kufaulu kwa Mambo hayo!!!

Ndoto hutuletea taarifa ya mambo yajayo na hivyo kutupa onyo ama tahadhari,na Kama mtu anaota ndoto baadae anazisahau au Haiti kabisa huyo ni sawa na marehemu yampasa kujichunguza mienendo yake,kuna siku nililala na kuota mke wangu anachati na mtu ambaye alikuwa hawala yake wa zamani,na Hadi namba ya simu ya bwana yake nilioneshwa,nilipoamka asubuhi nilimwambia mke wangu akakataa,baada ya siku mbili nilimfuma na namba ilikuwa Ni Ile Ile niliyoota.

Nilipokuwa shule nikiota nakimbia mbio ,na katika mbio hizo tuko watatu na nikawa eidha wa kwanza au wa pili na hata wa tatu Basi lazima nishike namba hizo katika matokeo ya mitihani yangu.

My brother mwaka 2010 aliniambia kuwa ameota kuwa Tanzania Kuna siku moja itatawaliwa na mwanamke ,nilimkatalia na nilimwambia labda miaka 100 ijayo ,Leo hii tuko katika utawala wa mwanamke.

Juzi kaniambia kuwa kaota makamu wa rais Dr. mpango amechukua madaraka,lakini ni katika namna ambayo si nzuri ,

Ndoto Mimi huziamini Sana,kikubwa ukilala na kuota ndoto ambayo Ni mbaya,pale pale amka na uikemee ili kuzui Mambo hayo kutokea.
 
Kifupi sana;
Ukiota ndoto, then ikasahaulika immediately unapotoka ucngzini, ujue Kuna Jambo la kwel na hakika linstukia very soon, kwa hyo ujumbe huo unakua hacked spiritually ili usijue kinachoendelea!!

Kwama hutojal, imekupasa kumwomba Mungu akurudishie ndoto hyo!!

Zaidi soma kitabu cha Daniel, utakutana na scenario ya namna hyo ambapo mfalme nebkadneza aliipata, akalazika kuwashurutisha wachawi na manabii wa kichawi wamweleze aliota ndoto gani na tafsir yake ni nini, na waliposhindwa aliwaangamiza , akawaamuru akina Daniel kwa namna hyohyo, ambao wao walifunga na kuomba na Kisha Mungu akawapa ndoto na tafsir yake.
Aisee! Kwahiyo ni vitu vinavyohusiana kiroho zaidi? Maana sio kawaida unaota then unashtuka usingizini halafu kama kuna pazia la kuzuia kumbukumbu linawekwa katikati ya ubongo wako na wewe mwenyewe!

Unajiuliza nimeota ndoto ndefu ya kutisha au ya kufurahisha lakini nimeota nini? Mbona sikumbuki? Then unaweza kuja kuikumbuka baadae ama yote au kipande au sehemu ya ndoto
 
Naamini ndoto ziko kiimani zaidi,Mambo mengi niyafanyayo bila ndoto huwa Sina uhakika wa kufaulu kwa Mambo hayo!!!

Ndoto hutuletea taarifa ya mambo yajayo na hivyo kutupa onyo ama tahadhari,na Kama mtu anaota ndoto baadae anazisahau au Haiti kabisa huyo ni sawa na marehemu yampasa kujichunguza mienendo yake,kuna siku nililala na kuota mke wangu anachati na mtu ambaye alikuwa hawala yake wa zamani,na Hadi namba ya simu ya bwana yake nilioneshwa,nilipoamka asubuhi nilimwambia mke wangu akakataa,baada ya siku mbili nilimfuma na namba ilikuwa Ni Ile Ile niliyoota.

Nilipokuwa shule nikiota nakimbia mbio ,na katika mbio hizo tuko watatu na nikawa eidha wa kwanza au wa pili na hata wa tatu Basi lazima nishike namba hizo katika matokeo ya mitihani yangu.

My brother mwaka 2010 aliniambia kuwa ameota kuwa Tanzania Kuna siku moja itatawaliwa na mwanamke ,nilimkatalia na nilimwambia labda miaka 100 ijayo ,Leo hii tuko katika utawala wa mwanamke.

Juzi kaniambia kuwa kaota makamu wa rais Dr. mpango amechukua madaraka,lakini ni katika namna ambayo si nzuri ,

Ndoto Mimi huziamini Sana,kikubwa ukilala na kuota ndoto ambayo Ni mbaya,pale pale amka na uikemee ili kuzui Mambo hayo kutokea.
Dah! Hilo la change of regime linatisha.

Na nimeshasikia sana kuna watu wakiota jambo ni lazima litokee!
 
Kwa mujibu wa maandiko matakatifu ya Paulo (mtume), kuna ndoto za aina mbili; aina ya kwanza ni matukio uliyoyafanya muda uliopita (muda mfupi au mrefu uliopita), na aina ya pili ya ndoto ni maono. Hii aina ya kwanza mtume Paulo anasema ni ya kupuuzia maana ni kumbukumbu tu iliyohifahidhiwa ubongoni (au akilini). Lakini aina ya pili, hii sio ya kupuuzia kwani ni ujumbe wenye lengo maalumu.

Tatizo linakuja kwenye hii ndoto ya pili (maono) ni kutafsiri, kama ambavyo mchangiaji aliyepita alivyofafanua ndoto ya mfalme Kardibuneza. Yawezekana wengi tunapewa maono kupitia ndoto, lakini kwa kuwa hatuwezi kuzitafsiri tunaachana nazo na kusema ni ndoto za kawaida na kwamba hazina maana.

Utakumbuka mfalme Farao wa Misri, aliota ndoto (maono) lakini hakujuwa maana yake, ndipo alipoletwa Yusufu toka gerezani ili atafsiri. Mfalme alioteshwa kuna ng'ombe saba walionawiri na wengine saba wamekonda sana. Tafsiri ya Yusufu kwa mfalme ilikuwa kutakuwa na miaka saba ya neema na miaka saba ya njaa. Ndipo mfalme alipompa jukumu Yusufu la kuwa waziri mkuu na kumtaka asimamie ukusanywaji wa chakula na kukihifadhi katika kipindi cha neema ili kipindi cha dhiki wasitaabike.

Na kweli, baada ya miaka saba, ilipiga njaa kali sana katika ukanda huo kwa kipindi cha miaka saba. Na hicho ndicho kilikuwa chanzo cha wana wa Israel kuhamia utumwani Misri. Walienda Misri kufuata chakula, lakini hili pia lilikuwa kusudio la Mwenyezi Mungu. Unaweza kuona kama huu ulikuwa ni mpango wa Mungu, ukiangalia tangu Yusufu anauzwa na ndugu zake. Kwa hiyo tuwe making na baadhi ya ndoto tunazoota, kwani mengine ni maono.
 
Kwa mujibu wa maandiko matakatifu ya Paulo (mtume), kuna ndoto za aina mbili; aina ya kwanza ni matukio uliyoyafanya muda uliopita (muda mfupi au mrefu uliopita), na aina ya pili ya ndoto ni maono. Hii aina ya kwanza mtume Paulo anasema ni ya kupuuzia maana ni kumbukumbu tu iliyohifahidhiwa ubongoni (au akilini). Lakini aina ya pili, hii sio ya kupuuzia kwani ni ujumbe wenye lengo maalumu.

Tatizo linakuja kwenye hii ndoto ya pili (maono) ni kutafsiri, kama ambavyo mchangiaji aliyepita alivyofafanua ndoto ya mfalme Kardibuneza. Yawezekana wengi tunapewa maono kupitia ndoto, lakini kwa kuwa hatuwezi kuzitafsiri tunaachana nazo na kusema ni ndoto za kawaida na kwamba hazina maana.

Utakumbuka mfalme Farao wa Misri, aliota ndoto (maono) lakini hakujuwa maana yake, ndipo alipoletwa Yusufu toka gerezani ili atafsiri. Mfalme alioteshwa kuna ng'ombe saba walionawiri na wengine saba wamekonda sana. Tafsiri ya Yusufu kwa mfalme ilikuwa kutakuwa na miaka saba ya neema na miaka saba ya njaa. Ndipo mfalme alipompa jukumu Yusufu la kuwa waziri mkuu na kumtaka asimamie ukusanywaji wa chakula na kukihifadhi katika kipindi cha neema ili kipindi cha dhiki wasitaabike.

Na kweli, baada ya miaka saba, ilipiga njaa kali sana katika ukanda huo kwa kipindi cha miaka saba. Na hicho ndicho kilikuwa chanzo cha wana wa Israel kuhamia utumwani Misri. Walienda Misri kufuata chakula, lakini hili pia lilikuwa kusudio la Mwenyezi Mungu. Unaweza kuona kama huu ulikuwa ni mpango wa Mungu, ukiangalia tangu Yusufu anauzwa na ndugu zake. Kwa hiyo tuwe making na baadhi ya ndoto tunazoota, kwani mengine ni maono.
Hoja yako ina mashiko mkuu. Inavyoonekana ndoto ni kama njia mojawapo ya mawasiliano kati Mungu na wateule wake
 
Dah! Hilo la change of regime linatisha.

Na nimeshasikia sana kuna watu wakiota jambo ni lazima litokee!
Wapo wa hivyo, nina rafiki yangu yeye mara nyingi akiota ndoto basi itatokea kweli hadi hua anaogopa kulala mchana maana ndoto zake za mchana ndio hua kweli karibia zote.

Mimi mara nyingi hua nikiota nikashtuka muda huo basi na ndoto nakua nishaisahau. Ni vile tu hua sifatilii sana ila nimegundua ndoto nyingi hua ni matokeo ya mawazo/matukio yaliyonitokea au nikiwa na hofu sana juu ya jambo flani nikilala usiku naota.
 
Wapo wa hivyo, nina rafiki yangu yeye mara nyingi akiota ndoto basi itatokea kweli hadi hua anaogopa kulala mchana maana ndoto zake za mchana ndio hua kweli karibia zote.

Mimi mara nyingi hua nikiota nikashtuka muda huo basi na ndoto nakua nishaisahau. Ni vile tu hua sifatilii sana ila nimegundua ndoto nyingi hua ni matokeo ya mawazo/matukio yaliyonitokea au nikiwa na hofu sana juu ya jambo flani nikilala usiku naota.
Haijawahi kukutokea ukamuota mtu ambaye haupo naye karibu au uliyepotezana nae miaka mingi na ulishamsahau? Maana mtu anaota mambo anayoyafikiria sana pengine huyo uliyemuota wala hakua mawazoni mwako hata kidogo
 
Haijawahi kukutokea ukamuota mtu ambaye haupo naye karibu au uliyepotezana nae miaka mingi na ulishamsahau? Maana mtu anaota mambo anayoyafikiria sana pengine huyo uliyemuota wala hakua mawazoni mwako hata kidogo
Nakumbuka hyo moja nilimuota mtu tulisoma nae kitambo and after few days nilikutana naye kituoni Mwenge na mazingira ni yale yale ya kwenye ndoto yalijirudia. Niliogopa! Ila badae nikapotezea nikasahau
Haijawah nitokea tena nadhani.

Sipendi sana kufatilia mambo ya ndoto maana ndoto zingine hua sio nzuri zinaweza fanya uishi kwa hofu
 
Kuna jamaa nilisoma nao advance

Jamaa 1: Huwa haoti kabisa, ila akiota basi jambo linatokea, alituhadithia mwenyewe

Jamaa 2:Aliwahi kuzingua sana home kwao, basi akaota mzee wake (marehemu) anamuadabisha kwa kumchapa bakora, alipoamka akakutana na maumivu na michirizi ya bakora
 
Kuna jamaa nilisoma nao advance

Jamaa 1: Huwa haoti kabisa, ila akiota basi jambo linatokea, alituhadithia mwenyewe

Jamaa 2:Aliwahi kuzingua sana home kwao, basi akaota mzee wake (marehemu) anamuadabisha kwa kumchapa bakora, alipoamka akakutana na maumivu na michirizi ya bakora
Huyo wa 2 duuh
 
Nakumbuka hyo moja nilimuota mtu tulisoma nae kitambo and after few days nilikutana naye kituoni Mwenge na mazingira ni yale yale ya kwenye ndoto yalijirudia. Niliogopa! Ila badae nikapotezea nikasahau
Haijawah nitokea tena nadhani.

Sipendi sana kufatilia mambo ya ndoto maana ndoto zingine hua sio nzuri zinaweza fanya uishi kwa hofu
Basi hiyo ni some kind of revelation(ufunuo) mkuu
 
Ndoto ina maana kubwa katika maisha ya binadamu.Wachawi hufanya ndoto zikupotee ili usiweze kufanya maelekezo ya kwenye ndoto.Ndoto ni utabiri wa kitu fulani unakuwa unaletewa kama picha ujipange,kujichunguza au kujitafakari.Unapoota nan ndoto kupotea wachawi wanakuwa wameihack hiyo ndoto!
 
Back
Top Bottom