Je, kutoa takwimu za watu waliokufa kwa matatizo ya kupumua wakati wewe siyo Waziri wa afya inaruhusiwa kisheria?

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Nauliza tu maana naona kasi ya watu na taasisi za kidini kutoa takwimu za marehemu wa magonjwa ya kupumua imeongezeka.

Waziri wa Katiba na sheria Prof Mwigullu Nchemba alisema wanaoruhusiwa kutoa takwimu ni Rais, Makamu wa Rais, Waziri mkuu na waziri wa afya pekee.

Sasa najiuliza hawa wengine akina Padri hawavunji sheria?

Maendeleo hayana vyama!
 
... kwamba imefika mahali haturuhusiwi kusema nyumbani kwetu tumepatwa na misiba? Na waliofariki ni idadi fulani? Kanisa limetoa taarifa jinsi lilivyoathirika; tena kwa heshima kubwa kwa kutokutaja majina ya waathirika; lingeamua wala sio dhambi kuwataja kwa majina. Kuzaliwa na kufa haijawahi na haipaswi kuwa siri!
 
Mtoa hoja hii acha kuwa na uchoyo wa ukweli,huyo waziri wa katiba kutumia kifungu gani cha kisheria kwenye katiba yetu eti ni wateule hao tu ndio wanaruhusiwa kutoa takwimu za covid 19?

Na mtoa hoja acha uoga hakuna ugonjwa wa kushindwa kupumua muda huu Tanzania imekumbwa na first wave ya covid 19 means tulia nyumbani,epuka mikusanyiko isiyo muhimu,nawa mikono kwa sabuni na running water,VAA Mask!
 
Unaijua bwa shee acha utani!! Hii kauli ni nzito mno..kanisa sasa limeamua kusimama na kuchukua hatamu!! Ni message kubwa mno kwa watawala...kuna jambo halipo sawa!!
... message mojawapo ni onyo kwa yule jamaa asirudie ujinga wake kung'ang'ania mike madhabahuni kuhubiri ujinga wake.
 
Unaijua bwa shee acha utani!! Hii kauli ni nzito mno..kanisa sasa limeamua kusimama na kuchukua hatamu!! Ni message kubwa mno kwa watawala...kuna jambo halipo sawa!!
Kuna watu humu nchini ni wapumbavu kidogo.
Kwamba ukiwa kiongozi unaweza kuamua na kusema lolote bila kufuata sheria yoyote ili mtu yoyote alazimike kuitii hii amuri bila shuruti.

Mwigulu anaonekana hayuko sawa kichwani.
Watu wanakufa bila kelele na hakuna ruhusa ya kusema sababu ya kifo???

Kweli huyu mutu ni mzima kichwani?

Ugonjwa unaua kwa kasi, unazuiaje taharuki kwa kunyamaza kimya?
 
Nauliza tu maana naona kasi ya watu na taasisi za kidini kutoa takwimu za marehemu wa magonjwa ya kupumua imeongezeka..

Maendeleo hayana vyama!
Kusema ni mtu fulani tu ndiye anaweza kitoa takwimu za ugonjwa au vifo, ni upumbavu.

Mtu yeyote mkuu wa taasisi yeyote ana haki ya kutoa takwimu ya wagonkwa, vifo, ajali. Kwa watu wanaojua uongozi, wanafajamu kiwa jukumu la la kwanza ni kiongozi yeyote ni usalama wa wqtu wake.

Kupiga marufuku ovyo ovyo ni ushamba na ulimbukeni wa madaraka. Marufuku za namna hiyo, watu wazipuuze, na wanaozitoa, wawadharau kama tunavyowadharau wendawazimu. Kuwa waziri au kiongozi mwingine yeyote haina maana umepewa haki kuwaondolea watu wengine itashi na akili.
 
Inaruhusiwa kwa sababu hakuna sheria inayokataza.

Yale yalikuwa matamko ya kisiasa.
Halafu Padri Kitime hajasema mapadri wamekufa kwa Corona kasema changamoto ya kupumua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…