Je, Marais wote duniani wakiwa wanawaambia 'Wateule' wao kuwa wasiwe kama Misikiti / Makanisa 'wanapoongoza' Watu humaanisha nini kati ya yafuatayo?

Je, Marais wote duniani wakiwa wanawaambia 'Wateule' wao kuwa wasiwe kama Misikiti / Makanisa 'wanapoongoza' Watu humaanisha nini kati ya yafuatayo?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Je,

1. Wasiwe Wapole sana?
2. Wawe na Roho mbaya mno?
3. Wawamalize Maadui zao mapema ili wasiwasumbue mbeleni?
4. Wawe wanamfurahisha yeye zaidi na siyo anaowaongoza?
5. Wahakikishe Maslahi ya Vyama vyao hao Marais ndiyo yanazingatiwa?
6. Wafanye Tukio Kubwa na Baya kwa Jamii ila ambalo litafurahiwa na kupongezwa na hao Marais?
7. Wakazane katika Miradi mbalimbali ili Chenji zinazobaki basi wawe wanawapelekea haraka Ikulu hawa Marais?

Karibuni katika Kuchangia japo nitapenda kupata Michango yenu Kamili yenye 'Uzoefu' zaidi katika hili ili nami GENTAMYCINE nijifunze mengi pia.
 
Mleta mada naona umemvalia njuga Magufuli anyway uchaguzi ukiisha tutajuana mbele kwa mbele wewe endelea tu na chokochoko zako
 
Wasiwe TISS
WAWE JW
WAWE na roho ngumu wasiwe wababaishaji
 
Ni Mtu anae amini ktk kutumia Nguvu kama option yake ya kwanza ili kulimaliza/kuondoa tatizo ambalo pengine halikuhitaji nguvu.Na haya ndio matumizi mabaya ya Akili ,wengine husema kuwa huyu Mtu hana Akili sawa sawa.
 
Mleta mada naona umemvalia njuga Magufuli anyway uchaguzi ukiisha tutajuana mbele kwa mbele wewe endelea tu na chokochoko zako

Matisho ni ya nini sasa Mkuu ,kwani sio kweli haya yana zungumzwa kwa Sababu yamekuwa yakijirudia kutoka kwa Bwana mkubwa ?
 
Mleta mada naona umemvalia njuga Magufuli anyway uchaguzi ukiisha tutajuana mbele kwa mbele wewe endelea tu na chokochoko zako
Anaongea ukweli au amemvalia njuga. Kwa wenye akili magufuli hafai kuwa hata kiongozi wa mtaa. Na Ndo mana mwaka huu tunamshtaafisha na kumrudisha Chato
 
Bashite angepiga marufuku Lisu kufanya shopping kariakoo, thus huyu kaambiwa asiwe shehe au mchungaji.
Ipo tofauti Kati ya zero brain na aliyepita darassni
 
Huyu the Genius tumeshamjua. Tumejua kuwa hakufanyiwa vetting ya uhakika 2015 kwa iyo alipita kimakosa tu.

Mwaka huu tunaenda kumuweka pembeni maana tumegundua hafai kwa mustakabali wa nchi hii. Ni mtu mbaguzi, mwenye chuki na roho mbaya kupindukia. Ni mdini mkubwa nayejificha udini wake kwenye kuwahonga viongozi wa dini.

Anaingia Lissu kuwa Raisi ili tuweke mfumo imara wa katiba, sheria na taasisi imara za kuwekeza kuisimamia nchi vizuri na kuzibiti madaraka ya Raisi.

Tulikosea sana 2015. Hatutakosea tena 2020
 
Kuna uzi kwa nini watu wenye roho nzuri/watenda wema utendewa mabaya.
Siku zote ukitaka kufanya jambo usipelekeshwe na watu uwezi kufika hata kidogo.ukiende nchi yoyote haya mambo yapo sema kwa vile sisi wakina asha mwajuma kwa midomo tunaona kama tunaonewa kuliko nchi yoyote
 
No.3 na 4 zinaweza kuwa ndiyo msingi wa maneno hayo.
Maana ya usiwe mpole kama Msikiti/Kanisa;

1.Kanisani/Msikitini huwa hatuhoji mahubiri/mawaidha ya kiongozi wetu, hivyo kauli hii inawataka wateule wasihoji au kuomba ufafanuzi wa maamuzi au maelekezo yenye ukakasi toka kwa Mteuzi.

2.Kanisani/Msikitini kiongozi ni mteule wa Mungu hivyo sisi wengine tunatafuta na kupeleka kwa ajili ya kazi ya Mungu. Hapa ukiwakuta viongozi walafi ndo unaona wanatembelea Vogue/Rolls Royce ya m300 huku muumini hana hata bike ya 90k.

Kwa maana hiyo anawasihi wasiwaonee muhali waumini wao, wawakamue hasa na vinavyopatikana vipelekwe kwa "malaika".
 
[emoji469][emoji626][emoji134][emoji134]
 
Back
Top Bottom