Je, Marekani inaogopa nini kwa kuhujumu mara kwa mara hadhi ya China kama nchi inayoendelea?

Je, Marekani inaogopa nini kwa kuhujumu mara kwa mara hadhi ya China kama nchi inayoendelea?

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG41N1198668373.jpg

Baraza la Wawakilishi la Marekani hapo awali lilipitisha mswada wa sheria iliyolenga kuivua China hadhi yake ya "nchi inayoendelea". Hivi karibuni, Bunge la Marekani lilipendekeza azimio lingine la kupinga hadhi ya nchi inayoendelea ya China katika Shirika la Biashara Duniani WTO. Kwa kujibu hilo, Wizara ya Mambo ya Nje ya China ilisema kuwa China haiwezi kuvaa kofia ya "nchi iliyoendelea" ambayo Marekani inataka kuipa China.

Kwanza kabisa, iwe nchi iliyoendelea au nchi inayoendelea, mashirika ya kimataifa yana vigezo, na Marekani haina uamuzi wa mwisho. Kulingana na vigezo vipya vya Benki ya Dunia, nchi yenye pato la taifa kwa mtu mmoja mmoja la zaidi ya dola za Kimarekani elfu 13 inaorodheshwa kama nchi yenye kipato cha juu. Mwaka 2022, Pato la Taifa la China kwa mtu mmoja mmoja lilikuwa dola 12,700, ni juu kidogo ya wastani wa kiwango hicho duniani, moja ya tano ya kiwango hicho cha nchi zilizoendelea, na moja ya sita ya kile cha Marekani. Uchumi mkubwa lakini pato dogo la taifa kwa mtu mmoja mmoja daima ni sifa kuu ya China kama nchi yenye idadi kubwa ya watu. Kama alivyosema Keith Rockwell, aliyekuwa msemaji wa WTO kwa karibu miaka 30, kwamba "China sio tu ina miji ya kisasa kama vile Beijing, Shanghai, na Guangzhou, lakini pia kuna maeneo ya magharibi ambayo yamejikwamua kwenye lindi la umaskini uliokithiri hivi majuzi tu ."

Hii si mara ya kwanza kwa Marekani kujaribu kudhoofisha hadhi ya China ya "nchi inayoendelea". Ili kuhalalisha kushindwa kwa "vita vya kibiashara dhidi ya China", serikali iliyopita ya Marekani iliyoongozwa na Donald Trump iliiomba mara kwa mara WTO kufuta hadhi ya China ya "nchi inayoendelea". Kwa maneno ya Trump mwenyewe: Kama nchi inayoendelea, China imepata manufaa mengi ambayo Marekani haina. Lakini hali halisi ni kuwa, China haijawahi kutumia hadhi hiyo kama sababu yake ya kukwepa majukumu ya kimataifa. Kinyume chake, katika suala la kukuza amani na maendeleo ya dunia, mchango wa China unazidi kwa mbali ule unaostahiki kwa nchi zinazoendelea, na hata kuzidi nchi zilizoendelea.

Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, kuanzia mwaka 2013 hadi 2021, wastani wa kiwango cha mchango wa China katika ukuaji wa uchumi wa dunia ulikuwa 38.6%, juu ya jumla ya mchango uliotolewa na kundi la G7. Tangu sera ya mageuzi na ufunguaji mlango ianze kutekelezwa, watu milioni 770 nchini China wameondokana na umaskini, na kuchangia katika kupunguza umaskini duniani kwa zaidi ya 70%, na kufikia lengo la Umoja wa Mataifa la kupunguza umaskini mwaka 2030 miaka 10 kabla ya muda uliopangwa. China pia ni nchi ya pili kwa mchango mkubwa katika Umoja wa Mataifa, na ya pili kwa mchango mkubwa katika shughuli za kulinda amani. Aidha, pendekezo la "Ukanda Mmoja, Njia Moja" na "Mipango Mitatu Duniani" iliyotolewa na China yote inalenga kukuza ushirikiano wa kimataifa na kujenga jumuiya ya binadamu yenye mustakabali wa pamoja. Hii kimsingi ni tofauti na Marekani, nchi iliyoendelea ambayo inachukulia maslahi ya nchi nyingine kuwa si kitu na kutoa vitisho na vikwazo.

Mara kwa mara Marekani imeunda mtego wa kauli ya "China si nchi inayoendelea". Kwanza, kuiondoa China kwenye kundi la nchi zinazoendelea kutaongeza gharama za kujitafutia maendeleo za China na kuifanya nchi hiyo kubeba majukumu zaidi ya uwezo wake. Pili, inaweza pia kuharibu uhusiano kati ya China na nchi zinazoendelea, na kuifanya China kuwa "ya kipekee", na tatu, pia itakandamiza kasi ya ongezeko la ushawishi wa jumla wa nchi zinazoendelea, na kudumisha utawala wa Marekani. China haikubaliani na njama kama hiyo, na hata nchi nyingine zinazoendelea pia hazitakubali.
 
China inaitwa nchi inayoendelea licha ya ukuaji wake mkubwa wa kiuchumi kutokana na sababu zifuatazo:
  1. Pato la Taifa kwa Kila Mtu (GDP per Capita): Ingawa China ina uchumi wa pili kwa ukubwa duniani, GDP per capita yake bado ni ya kati ikilinganishwa na nchi zilizoendelea. Kwa mfano, mwaka 2022, GDP per capita ya China ilikuwa takriban dola za Marekani 12,992, wakati nchi kama Marekani ilikuwa na GDP per capita ya zaidi ya dola 70,000 katika kipindi hicho.
  2. Viashiria vya Maendeleo ya Jamii: China imepiga hatua katika kuboresha huduma za afya na elimu, lakini bado kuna tofauti kubwa kati ya maeneo ya mijini na vijijini. Maeneo ya vijijini mara nyingi yanakabiliwa na upungufu wa miundombinu na huduma muhimu, hali inayoashiria changamoto katika maendeleo ya kijamii.
  3. Ukosefu wa Usawa wa Kiuchumi: Kuna tofauti kubwa za kipato kati ya wakazi wa mijini na vijijini nchini China. Ingawa miji mikubwa kama Beijing na Shanghai ina viwango vya juu vya maisha, maeneo ya ndani bado yanakabiliwa na umaskini. Kwa mfano, mwaka 2016, asilimia 5.7 ya watu wa China waliishi chini ya mstari wa umaskini wa kitaifa.
  4. Mfumo wa Siasa na Uchumi: China ina mfumo wa kipekee unaochanganya soko huria na udhibiti wa serikali. Ingawa imepiga hatua kubwa katika mageuzi ya kiuchumi, bado kuna maeneo yanayohitaji maboresho, kama uwazi katika masoko na uhuru wa kisheria, ili kufikia viwango vya nchi zilizoendelea.
  5. Utegemezi wa Sekta za Kiwanda na Kilimo: China bado inategemea sana sekta za viwanda na kilimo. Ingawa kuna ukuaji katika sekta ya huduma na teknolojia, mchango wa sekta hizi bado haujafikia viwango vya nchi zilizoendelea, ambazo zinategemea zaidi uchumi wa huduma na teknolojia ya hali ya juu.
  6. Viashiria vya Mazingira na Maendeleo Endelevu: Ukuaji wa haraka wa viwanda nchini China umeleta changamoto za kimazingira kama uchafuzi wa hewa na maji. Ingawa serikali imeanzisha hatua za kukabiliana na matatizo haya, bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kufikia viwango vya uendelevu vinavyoonekana katika nchi zilizoendelea.
Kwa sababu hizi, licha ya mafanikio yake makubwa ya kiuchumi, China bado inachukuliwa kama nchi inayoendelea kulingana na viwango vya kimataifa.
 
Back
Top Bottom