Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
Alibadili katiba(Kihuni) na kutoa ukomo ili ajipe haki ya kuwa mwenyekiti bila ukomo. So unaposema haki ya kikatiba elewa vyema kuwa alijipa haki hiyo kihuni.Masharti kabla ya makubaliano? Una maana CDM waliweka masharti ambayo walitaka yatekelezwe kabla ya kuingia kwenye majaliano. Tatizo lenu wafuasi wa Lissu ni kuwa mnaamini kuwa watu huwa wanaanza majadiliano kabla ya masharti yote kutimizwa. Ndivyo ilivyo Gaza. Au kinacho wauma ni kuwa sharti mojawapo lilikuwa Lissu alipwe stahili zake lakini wakina Mbowe wakaanza majadiliano kabla hajalipwa? Au hamkutaka mazungumzo kabla wakina Halima kuondolewa Bungeni?
Mnadhani hayo machache mnayobeza yaèx̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌x̌
Amandla...
Kama mnamuona mhuni basi fanyeni kampeni asipigiwe kura lakini sio kutaka kumnyang'anya haki yake ya kikatiba. Mkifanikiwa kwake si ndio mtaweza kuwakataza wengine kugombea kwa sababu watu wa dini yao wameongoza kwa muda mrefu ( kwa nini ni muislamu mmoja tu ndio amewahi kuwa Mwenyekiti) au watu wa jinsia yao ( kwa nini wanaume tu ndio wamekuwa wenyekiti) au watu wa kutoka eneo fulani ( ni zamu sasa ya wachaga kukaa pembeni ili wamakonde nao waonje uenyekiti) au sasa ni zamu ya mzanzibari kuwa Mwenyekiti au watu wafupi n.k.
Mnafungua boksi la Pandora kwa hili mnalofanya.
Amandla..
Na demokrasia isikufanye uende kama roboti, kama mnaona kupokezana Wakristo na Waislamu, au Wamakonde na Wachagga kunajenga zaidi basi fanyeni hivyo. Huko ni kukomaa na kuondoa Tyranny of the majority, wala si kufungua pandora box.