Je, mfumo wa ulinzi wa anga lsrael "Iron Dome" hauaminiki tena?

Je, mfumo wa ulinzi wa anga lsrael "Iron Dome" hauaminiki tena?

Hamas walirusha makombora zaidi ya elfu tano je ni mangapi yalitua kwenye ardhi ya Israel?
 
Waisrael hawana lolote. Jeshi la nchi linapigana na kikundi Cha wahuni wachache Leo Ni wiki ya tatu, Sana Sana wanaua raia wasio na hatia.
Imagine Israel ingepigana na jeshi la nchi Kama iran au hata Somalia ambao Wana maji, mafuta na chakula, si Israel ingechakazwa ndani ya wikimoja, au imagine Israel isingesaidiwa na marekani si wangekosa sehemu ya kuzikia!
Israel ilikuwa haina nia ya kupigana na hamas bali inachofanya ni kujilinda dhidi ya mashambulizi ya kuvizia ya hamas kwa kuwaondolea uwezo wa kijeshi
 
Mfumo huu ambao unaaminika kuwa bora na wenye ufanisi mkubwa katika siku za hivi karibuni umeonyesha shaka. Mfumo huu ulibuniwa na kampuni ya kizawa Rafael advanced system

1: Hamas waliporusha makobora Tel aviv mengi kwa mkupuo battery za Iron dome zilichoka na ikabidi wafanye recharging.

2: Ilibidi waomb4 msaada US wa makombora ya kwa ajili ya kujazia kwenye Iron dome maana waliokuwa nayo waliona yanaisha.

3: Kitendo cha marekani juzi kupeleka mifumo yake ya ulinzi kuongezea nguvu Iron dome huko Israel.

4: Je siku zote wamejiandaa kupambana na taasisi dhaifu kama Hamas ambao viatarishi vyao ni hafifu ukilinganisha na Iran na Vibaraka wake Hesbullah wenye uwezo mkubwa kuliko hamas.

Je ni kweli Israeli hii ni toafuti na ile ya miaka ya Sabini ambayo ilikuwa na uwezo wa kuwapa vichapo waarabu wote kwa siku moja tu. Au wanafanya makusudi kwa njama na US ili wapate kisingizio cha kuifuta Iran maana ndio adui mkuu mwenye watoto maadui wa Israel.


Ni hayo tu.
Ni kweli Israel hii ni dhaif ndiyo maana mpaka sasa waisrael waliokufa ni wengi kuliko wapalestina, na israel imegeuzwa magofu na hamas wakati gaza iko vilevile hakuna hata kombora moja la israel lililofanikuwa kutua au kulipuka gaza maana yote mifumo ya anga ya hamas imeyadaka na kuyarudisha israel. Mpaka sasa Israel inalialia tu wakati Palestine incheeka kwa dhereu! Mpaka sasa kutokana na kichapo ilichopewa Israel imeomba Hamas wasitishe vita.
allah akbar...tumswalie mtume....
 
Mfumo huu ambao unaaminika kuwa bora na wenye ufanisi mkubwa katika siku za hivi karibuni umeonyesha shaka. Mfumo huu ulibuniwa na kampuni ya kizawa Rafael advanced system

1: Hamas waliporusha makobora Tel aviv mengi kwa mkupuo battery za Iron dome zilichoka na ikabidi wafanye recharging.
Kwamba Iron Dome ilichoka ikabidi ifanyiwe 'recharging' (unamaanisha reloading). Ni mfumo gani duniani hauna reloading?

Hiyo S-400 unayosifia si inabeba four missile canisters kwenye launcher moja. Zikiisha nne wanafanyaje kama sio reloading? Au wanatupa launching vehicle?
Reloading ya S-400 hii hapa, na Russia wana tabia ya kurusha interceptors zaidi ya moja (salvo launching) sababu ya wasiwasi wa accuracy na makombora yao sio hit to kill bali air blast.
5b19a13edda4c8491d8b4585.jpg

2: Ilibidi waomb4 msaada US wa makombora ya kwa ajili ya kujazia kwenye Iron dome maana waliokuwa nayo waliona yanaisha.
Sasa mfumo unaodai hauna uwezo inakuwaje tena wanauombea makombora ya kujazia (interceptors). Hayo makombora yatarushwa na mfumo gani?

Kwa taarifa yako Iron Dome haijaishiwa bali Israel inajipanga kupigana na yeyote atakayejitokeza. Badala watumie kila walichonacho wanajiandaa for the worst. Na kilichofanyika hapo ni mkataba wao na Marekani wa muda mrefu. Hata South Korea wana mkataba huohuo ndio maana mwaka huu imetoa mamilioni ya artillery shells kwenda Marekani.
Kuna makombora na maroketi zaidi ya 200,000 yametengenezwa dhidi ya Israel. Taja ni mfumo gani duniani unaweza zuia makombora zaidi ya 200,000 ukiwa wenyewe.
3: Kitendo cha marekani juzi kupeleka mifumo yake ya ulinzi kuongezea nguvu Iron dome huko Israel.
Hiyo ni deterrence. Hujaona kambi za Marekani pale Iraq zinashambuliwa na suicide drones?
Kuna mtu anadekezwa azoee, ili ushahidi ukijaa abamizwe.
4: Je siku zote wamejiandaa kupambana na taasisi dhaifu kama Hamas ambao viatarishi vyao ni hafifu ukilinganisha na Iran na Vibaraka wake Hesbullah wenye uwezo mkubwa kuliko hamas.
Iran haina uwezo wa kupigana na Israel ikiwa yenyewe. Walikuwepo Jordan, Syria na Egypt kwa pamoja wakashindwa. Iran analazimika kutumia magaidi wasiotofautishwa na raia. Ndio maana Hamas wana command center yao chini ya hospitali kubwa zaidi Gaza, ili ikipigwa na Israel wajilize
20231027_183028.jpg

Iran ikisimama yenyewe na Israel inapoteana. Kama unadhani ina jeshi, mwaka 1967 Egypt ilikuwa na jeshi Iran ni takataka. Zaidi ya ndege 400 ya kisasa kabisa wakati huo na ikapigwa vibaya na hapo sijataja mamia ya Jordan na Syria. Iran haina hata nusu ya ndege kama hizo na bado ni za kizamani sana kina F-4, F-14 za Marekani.
Je ni kweli Israeli hii ni toafuti na ile ya miaka ya Sabini ambayo ilikuwa na uwezo wa kuwapa vichapo waarabu wote kwa siku moja tu. Au wanafanya makusudi kwa njama na US ili wapate kisingizio cha kuifuta Iran maana ndio adui mkuu mwenye watoto maadui wa Israel.


Ni hayo tu.
Kuna mtu anavimbishwa kichwa ila naye sio mjinga. Huu ushabiki upo mtandaoni tu, Ayatollah anajua fika akianzisha vita na Israel ndio mwisho wake ila anawa-pump mashabiki ili asionekane myonge. Ground invasion ya Gaza Waarabu wanadai imeanza takribani lisaa lililopita, ambavyo Israel inadai hiyo ni ground clearance kuondoka landmines, road blocks na vifusi vya majengo waliyolipua.

Hezbollah ilidai Gaza ikivamiwa inaingia vitani, basi sababu zake zimetimia leo iingie rasmi vitani hao Lebanon wahesabu umaskini.
Iran abaki na wanamgambo Wasyria na Wairaq wakijiunga wanafuatwa ukouko kwao bases za Marekani zipo, Houthi hata Saudi Arabia hawawezi sembuse ushirika wa Marekani. Iran ikibaki yenyewe unapiga serikali tu. Jambo wasilojua watu wengi ni kwamba mbwembwe za Iran zipo kwenye Revolutionary Guard Corps, jeshi la Ayatollah linalopendelewa naye. Fujo sio za jeshi la nchi ya Iran ambalo huisiwa sio waaminifu sana na hawapewi marupurupu makubwa.
 
Yaaani mmatumbi wa kisemvule umekaa uka chambua ukaona ndo ume chambua uchambuzi yakinifu kabisaa?
hivi zile Rockets zinazo rushwa kwa maelfu zingekua zina tua Tel aviv kila zinapo rushwa na huo mfumo kama haufanyi kazi si tunge kua tuna sikia idadi ya vifo ikiwa inaongezeka israel kila siku?
 
Back
Top Bottom