Je, Mungu anapokupa jaribu anakuacha upambane nalo au anakuletea na usaidizi wake? Mjamzito anataka msaada wangu, hatujawahi kuwa na mahusiano

Mtu akiwa chini ya jaribu, asiseme: “Mungu ananijaribu.” Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu yeyote.

Yakobo 1:13...
Yakobo 1:14
[14]Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

Kwa hiyo nisimsaidie, maana hapa maandiko yanasema najaribiwa na tamaa yangu, kitu ambacho si kweli. Kwa ile mimba nitamani nini mimi hata mtalimbo hauwezi kushituka
 
Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.
Yakobo 1:12

Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu.
Yakobo 1:13
 
Najua wewe hauna PESA ila mpokee hapo Gheto kwako usimfukuze Wala usifanye naye ngono hakikisha unamshinda SHETANI , unaweza kuomba Mungu afungue milango mtakula na kusaza na hamtakwama Mungu wetu ni mkuu Sana hawezi kukuacha hivi hivi
 
-Kwa nini hataki kwenda kwao?
-Wewe mwenyewe huna kazi unadhani mtaishije na mjamzito kuna muda anahitaji uangalizi maalum? Mungu ni mwema akijifungua salama, utawezaje kujihudumia wewe, na yeye, na mwanae ilihali huna kazi?
_Huna mawasiliano na ndugu zake, akipata tatizo kubwa kiafya au hata akifa wewe utafanyaje?

Huyo ni kiumbe tena mwenye mahitaji
maalumu na anatarajia kuleta kiumbe kingine chenye mahitaji maalum. Ebu mwambie kuwa ni lazima upate mawasiliano na kwao in case of anything. Unaweza kuendelea kukaa naye ila kwao wawe na taarifa zake. Huwezi jua ukakutanishwa na rafiki yako ambaye ni kaka yake mliyepotezana mkaanza kusaidiana kumhudumia huyo dada.
Una roho nzuri sana mkuu lakini huyo ni mtoto wa watu usiongozwe na hisia za kutoa msaada ukasahau uhalisia wa maisha
 
Mtu kaachwa na bwanake halafu mtu baki anaumiza kichwa, kuna watu wana bahati, hicho kiumbe tumboni kitakuwa na kitu special sana
 
LIPIA TANGAZO.
Uomenyesha ni jinsi gani bichwa lako limepungukiwa hekima. Mleta mada hajataka kuomba pesa, kasema kwa kipindi hiki kigumu yuko tayari kufanya kazi yoyote sababu ya mjamzito, wewe unaleta uchekechea wako hapa.

Kwani ungesoma na usichangie ungepata hasara gani?
 
Msaidie na Mungu hatakupungukia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona unaendeshwa na mihemko kiasi hiki?

Naijua hiyoo....

Au wewe ndo huyo mwenye mimba anayepigiwa promo na kutumika kutolea tangazo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…