Je! Mungu ni yule yule?

Mungu wao angekuwapo, kusingekuwa na mabaya.

Kuwepo kwa mabaya ni ushahidi kwamba mungu huyo hayupo.

Ama sivyo, kwa nini mungu mwenye ujuzi wote, upendo wote na uwezo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana?
Sasa fanya hivi kwanza,tupe ushahidi wa kuwa haya mabaya yameumbwa na aliyeumba ni mungu,ukiweza hilo kisha utupe ushahidi wenye kueleza kuwa mungu hana uwezo wa kuumba mabaya au anao huo uwezo ila alisema hatoumba mabaya.
 
Haiwezekani kuwepo na Mungu mwenye uwezo wote, upendo, muumbaji wa vyote na aliyeko kila mahali huku tushuhudie mapungufu mengi kiasi hiki kwenye ulimwengu huu mnaosema kwamba kauumba yeye.
Unaposema mapungufu unazungumzia nini?na msingi wa hoja yako ya hayo mapungufu imetoka ndani ya vitabu vya vyenyd kumzungumzia huyo mungu au ni kimtazamo wako tu?
 
Unaposema mapungufu unazungumzia nini?na msingi wa hoja yako ya hayo mapungufu imetoka ndani ya vitabu vya vyenyd kumzungumzia huyo mungu au ni kimtazamo wako tu?
Ndani ya kitabu chenu kitakatifu cha biblia
 
Sasa fanya hivi kwanza,tupe ushahidi wa kuwa haya mabaya yameumbwa na aliyeumba ni mungu,ukiweza hilo kisha utupe ushahidi wenye kueleza kuwa mungu hana uwezo wa kuumba mabaya au anao huo uwezo ila alisema hatoumba mabaya.
Huyu Mungu huyu[emoji2] [emoji2] [emoji2] yani awe na uwezo wa kuzuia mabaya ila akae tu na kusema hatazuia?? Yataka uwe na moyo mzito sana kuamini hili
Maelezo yako tu hapo [emoji115] [emoji115] juu yanatosha sana kuonyesha kuwa hayupo
 
Huyu Mungu huyu[emoji2] [emoji2] [emoji2] yani awe na uwezo wa kuzuia mabaya ila akae tu na kusema hatazuia?? Yataka uwe na moyo mzito sana kuamini hili
Maelezo yako tu hapo [emoji115] [emoji115] juu yanatosha sana kuonyesha kuwa hayupo
Kama utaweza kujibu hayo maswali ndipo utaweza kupata jibu la hilo swali lako,maana uoga wenu ndio unaofanya kuja na hili jambo ambalo wenyewe mnajichanganya,mara mwengine aseme mungu asingeumba mabaya kama yupo mwengine aseme mungu angeyazuia mabaya kama yupo.
 
Yani unaniuliza kitu ambacho hakijawahi kutokea nilikiangalia wapi? Una hakika kuwa akili yako iko sawa?
We umesema ya kwamba Mungu hayupo, ndio nakuuliza ulimwangalia wapi ukakuta hayupo...?!
 


 
Hakuna mungu, huyo unayemsoma ni hadithi tu zimetungwa na watu.

Ukijua hili swali lako halitakutatiza.
Kwa hiyo Mkuu Kiranga huwezi kuamini kuwa Mungu yupo hadi umuone? Tutaaminije kuwa kuna mtu aliitwa Vasco da Gama ilihali hatumuoni. Kama historia iliyo ktk vitabu vya dini ni maneno ya watu tu unatushauri tusiamini historia kwa sababu ni hadithi tu zilizotungwa na watu?
Unataka kutuaminisha kuwa hata wajerumani hawakuitawala Tanganyika kwa sababu kina Gen. Smutts hatuwaoni?
Lakini nyinyi kina Kiranga msioamini uwepo wa supreme being, kama wengine wanavyoita, mna ushahidi gani wa coincidence ya namna hii, kuwa eneo moja watokee viumbe hai wa aina tofauti, wenye uwezo tofauti bila kuwa na mpangaji? Tizama tu ulivyo, macho mawili, Masikio mawili, siyo moja nk. Angalia hizo sense zinavyofanya kazi. Mfumo wa mwili na ubongo, kwamba vitu hivi vijitengeze vyenyewe kwa mpango mkuu kiasi hiki cha kustaajabisha. Hakuna ushahidi wa kisayansi hadi muda huu wa kuthibitisha hayo mnayoyasema. Hakuna pori lolote, mahali popote, ktk Dunia hii, ambapo imegundulika kuwapo na aina yoyote ya kiumbe kinachoanza kujiumba chenye mwelekeo wa baadaye kuja kuwa binadamu au ht Simba. Mfumo wa kujiumba ungekuwepo mfumo huo usingehangaika kutengeneza dume na jike ambao ni very sophisticated. Mfumo ungeendelea kuproduce viumbe kwa njia hiyo hiyo iliyoanza nayo. Kwa vyovyote, mfumo tulio nao wa reproduction ni planned very carefully. Tatizo lenu ni huyo, the great planner, hamumuoni, na nyinyi mnataka ushahidi wa 5 senses, kuona, kusikia, kugusa, kunusa na kuonja. Nyinyi ni sawa na watu waliokuta hoteli kubwa porini, wakaingia ndani, wakakuta kila kitu, wakala, wakaoga na kulala bila kumuona mwenye hoteli. Kesho wakaondoka na kuamua kuwa hoteli ilijijenga yenyewe kwa sababu hawakumuona mjenzi wa Hoteli.
Mpango wa Mungu unatisha, the universe inavyofanya kazi. Mwendo wa kasi wa Dunia ya speed zaidi ya 105,000 kwa saa, haijapungua wala kuongezeka. Na hii ni kuwahi majira ya siku na mwezi. All these are the plans of the Great Being.
Jamani, wakati fulani tunatakiwa kuamini ukuu na uwepo wa huyu Muumbaji na mpangaji Mkuu kwa kuona na kushuhudia uumbaji na ubunifu huu wa ajabu.
Sio lazima Mungu awaeleze kila kitu kuhusu yeye. Sio lazima Baba au Mama yako akueleze kila kitu kuhusu kupatikana kwako. Siyo lazima akuambie mimba yako ilipatikana muda gani, kwa staili gn ya kujamiana.
 
Nikuulize wewe ambae upeo wako umeishia kwenye kuangalia[emoji2] [emoji2]
Wa kwako uliishia kwenye kumtafuta kabisa...? Ukamkosa..

Ndio nakuuliza ulimtafutia wapi ukagundua hayupo...?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…