Je, Musa hakuandika kitabu cha Mwanzo??

Je, Musa hakuandika kitabu cha Mwanzo??

Mkuu tuache kuzunguka naomba unisaidie swali nimeuliza kama pentateuch ziliandikwa na musa kwenye zile siku 40 je habari za kifo chake, kanaan na wakaldayo aliziandika nani ilihali Musa alishakuwa amekufa

Yaani exodus 27 na kuendelea aliandika nani kama Musa alishakuwa ameshuka kutoka mlimani
Embu weka hiyo mistari
 
Nimemsikiliza ila anachozungumza kinakinzana na imani anayosimamia haimaanishi kua yupo neutral

Hujamsikiliza mpaka mwisho kwani time ya hiyo clip ni nusu saa na wewe umerukia kuandika hata dakika kumi haijafika
 
biblia yako imejaa upuuzi wa kutosha



YEHOVA ARUHUSU WATU KULA WATOTO WAO

Kumbukumbu la Torati 28:53

53 Nawe utakula uzao wa tumbo lako mwenyewe, nyama ya wana wako na binti zako aliokupa Bwana, Mungu wako; katika mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako.



YEHOVA KUWAPAKA MAVI MAKUHANI

Malaki 2:1-3

2 Kama hamtaki kusikia, na kama hamtaki kuitia moyoni, ili kulitukuza jina langu, asema Bwana wa majeshi, basi nitawapelekeeni laana, nami nitazilaani baraka zenu; naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamyatii haya moyoni.

3 Angalieni, nitaikemea mbegu kwa ajili yenu, nami nitapaka nyuso zenu mavi, naam, mavi ya vyakula vyenu; nanyi mtaondolewa pamoja nayo



YESU AWAAMBIA WAFUASI WAKE WANUNUE MAPANGA

Luka 22:36

Akawaambia, Lakini sasa mwenye mfuko na auchukue, na mkoba vivyo hivyo; naye asiye na upanga, na auze joho yake akanunue.











YEHOVA HATAKI BINADAMU AJUE MEMA NA MABAYA

Mwanzo 3:22

Kisha Mwenyezi-Mungu akasema, “Sasa, binadamu amekuwa kama mmoja wetu, anajua mema na mabaya. Lazima kumzuia kula lile tunda la mti wa uhai, kwani akilila ataishi milele!”



YEHOVA AUA HALAIKI NA KUWAACHA BIKRA

HESABU 31:15-17

15 Kwa hiyo Musa akawaambia: “Je, mmemhifadhi hai kila mwanamke?+ 16 Tazama! Hao ndio, kupitia kwa neno la Balaamu, waliowashawishi wana wa Israeli kukosa uaminifu+ kwa Yehova juu ya lile jambo la Peori,+ hivi kwamba tauni ikaja juu ya kusanyiko la Yehova.+ 17 Na sasa ueni kila mtoto wa kiume, na kumuua kila mwanamke ambaye amefanya ngono na mtu kwa kulala na mwanamume



YEHOVA ATAKA WATU WATII SERIKALI HATA KAMA HAIKUCHAGULIWA NA WATU

Warumi 13

13 Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu. 2 Kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala ana pinga chombo kilichowekwa na Mungu; na watu wanaoasi watajiletea hukumu.





YEHOVA MUASISI WA MFUMO-DUME

1 timotheo 2:11-12

11 Mwanamke na ajifunze akiwa kimya na kwa kujitiisha kikamili.+ 12 Simruhusu mwanamke kufundisha,+ wala kuwa na mamlaka juu ya mwanamume,+ bali kuwa kimya.



YEHOVA,MUASISI WA UTUMWA

Mwanzo 9:25-27

25 Basi akasema:“Alaaniwe Kanaani.

Na awe mtumwa wa hali ya chini kabisa kwa ndugu zake.”26 Naye akasema tena:“Abarikiwe Yehova, Mungu wa Shemu,Kanaani na awe mtumwa wake. 27 Mungu na ampe Yafethi nafasi ya kutosha,Akae katika mahema ya Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake pia.”



PONOGRAFIA NDANI YA BIBLIA

Ezekieli 23:20

Aliwatamani sana wanaume wenye uume kama wa punda na manii kama farasi dume.”













YEHOVA BINGWA WA KUKOMOA NA KUTESA

Kumbukumbu la torati 28:28-35

28 Yehova atakupiga kwa wazimu+ na kupoteza uwezo wa kuona+ na kuchanganyikiwa kwa moyo.+ 29 Nawe kwa kweli utakuwa mtu anayepapasa-papasa katikati ya mchana, kama vile kipofu anavyopapasa-papasa gizani,+ nawe hutafanya njia zako zifanikiwe; nawe utakuwa mtu tu ambaye sikuzote hupunjwa na kunyang’anywa, pasipo mtu wa kukuokoa.+ 30 Utamchumbia mwanamke, lakini mwanamume mwingine atamlala kinguvu.+ Utajenga nyumba, lakini hutakaa ndani yake.+ Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutaanza kutumia matunda yake.+ 31 Ng’ombe-dume wako atachinjwa hapo mbele ya macho yako—lakini hutakula sehemu yoyote yake. Utanyang’anywa punda wako mbele ya uso wako—lakini hatarudi kwako. Kondoo wako watapewa adui zako—lakini hutakuwa na mwokozi yeyote.+ 32 Wana wako na binti zako watapewa watu wengine+ na macho yako yakitazama na kuwatamani sikuzote—lakini mikono yako itakuwa haina nguvu.+ 33 Mazao ya udongo wako na mazao yako yote yataliwa na watu ambao hukuwajua;+ nawe utakuwa mtu aliyepunjwa na kupondwa sikuzote.+ 34 Nawe utatiwa wazimu kwa kuona kwa macho yako mambo ambayo utaona.+ 35 “Yehova atakupiga kwa jipu hatari kwenye magoti yote mawili na miguu yote miwili, ambalo hutaweza kupona, kutoka wayo wa mguu wako mpaka utosi wa kichwa chako













YEHOVA AHAMASISHA WATU WAPIGANE

Kumbukumbu la torati 25:11

11 “Ikiwa wanaume wawili watapambana pamoja, na mke wa mmoja awe amekuja karibu ili kumkomboa mume wake kutoka mkononi mwa yule anayempiga, naye ameunyoosha mkono wake na kumkamata sehemu zake za siri,+ 12 basi ukate mkono wa mwanamke huyo.



YEHOVA APANDISHA JAZBA,AUA WATOTO 42 PAPO HAPO

2 wafalme 2:23-25

3 Naye akapanda kutoka hapo mpaka Betheli.+ Alipokuwa akipanda njiani, tazama, palikuwa na wavulana+ wadogo waliotoka katika jiji, nao wakaanza kumdhihaki,+ wakazidi kumwambia: “Nenda juu, wewe kipara!+ Nenda juu, wewe kipara!” 24 Mwishowe akageuka nyuma, akawaona, naye akawalaani+ katika jina la Yehova. Ndipo dubu-jike+ wawili wakatoka katika vichaka, wakaanza kuwararua vipande-vipande watoto 42 kati yao.+ 25 Naye akaendelea kutoka hapo mpaka Mlima Karmeli,+ na kutoka hapo akarudi Samaria.



YEHOVA APITISHA ADHABU YA KIFO KWA MLEVI

Kumbukumbu la torati 21:18-21

“Ikiwa mtu atakuwa na mwana ambaye ni mkaidi na mwasi,+ awe hasikilizi sauti ya baba yake au sauti ya mama yake,+ nao wamemrekebisha bali yeye hawasikilizi,+ 19 baba yake na mama yake watamshika na kumtoa nje mpaka kwa wanaume wazee wa jiji lake na kwenye lango la mahali pake,+ 20 nao watawaambia wanaume wazee wa jiji lake, ‘Huyu mwana wetu ni mkaidi na mwasi; hasikilizi sauti yetu,+ ni mlafi+ na mlevi.’+ 21 Ndipo watu wote wa jiji watampiga kwa mawe, naye lazima afe.



YEHOVA ANYANYAPAA VILEMA,WENYE PUA PANA(KAMA zA WATU WEUSI)

Mambo ya walawi 21:17-23

17 “Sema na Haruni, na kumwambia, ‘Mtu yeyote wa uzao wako katika vizazi vyao vyote ambaye ana kasoro+ asije karibu ili kuutoa mkate wa Mungu wake.+ 18 Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye kasoro, asikaribie: mtu aliye kipofu au kilema au mwenye pua pana au mwenye kiungo kimoja kilicho kirefu mno,+ 19 au mtu aliyevunjika mguu au aliyevunjika mkono, 20 au mwenye kijongo au aliyekonda au mwenye ugonjwa wa macho au mwenye vigaga au mwenye mba au aliyevunjwa mapumbu yake.+ 21 Mtu yeyote wa uzao wa Haruni kuhani ambaye ana kasoro hatakaribia ili kutoa matoleo ya Yehova kwa njia ya moto.+ Kuna kasoro ndani yake. Hatakaribia ili kuutoa mkate wa Mungu wake.+ 22 Anaweza kula mkate wa Mungu wake kutoka kati ya vitu vitakatifu zaidi+ na kutoka kati ya vitu vitakatifu.+ 23 Hata hivyo, hatakaribia pazia,+ wala hatakaribia madhabahu,+ kwa sababu kuna kasoro ndani yake;+ naye hatapatia unajisi patakatifu pangu,+ kwa kuwa mimi ni Yehova ninayewatakasa wao.



YEHOVA AFANYA MAUAJI YA HALAIKI,AUA WATOTO WACHANGA HADI WANYAMA

1 samweli 15:3

3 Sasa nenda, umpige Amaleki,+ umwangamize+ pamoja na vitu vyote alivyo navyo, usimhurumie, nawe uwaue,+ mwanamume na mwanamke, mtoto na mtoto anayenyonya,+ ng’ombe pamoja na kondoo, ngamia pamoja na punda.’



YEHOVA APATA KIU YA DAMU YA BINADAMU

Mwanzo 22:2

Mungu akamwambia, “Mchukue mwanao, Isaka, mwanao wa pekee umpendaye, uende mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuonesha.”



YESU AWATAKA WATUMWA KUTII MABWANA WAKATILI

1 Petro 2:18

18 Ninyi watumwa, watiini mabwana wenu kwa heshima yote, si wale mabwana walio wapole na wema peke yao, bali hata wale walio wakali.

"Yehovah atapaka watu mavi naam mavi ya vyakula vyao" Malaki 2:3

Yaani huyu yehovah hatarii
 
Mkuu sijaelewa umetasfrisi vipi hilo neno hajainuka..bila shaka hapa umelizungumzia kama neno linalowakilisha wakati ukiopita...ila kiuhalisi neno hilo linatumika kwa wakati uliopo pia..pili maneno hayo yameandikwa wakati musa akimuwekea mkono Yoshua ili aendelee kuwaongoza wana wa israel pia kumbuka #Musa alikua haandiki kile anachojisikia kuandika au anachopenda kuandika bali alikua anandikakile alichoelezwa na Mungu kupitia roho takatifu#
Mkuu cjui umeelewa concern yangu kwamba mtu anayesema WALA HAJAINUKA ni mtu mwingine.... Ikimaamisha Musa mwenyewe asingeweza kutoa hii kauli ya "majigambo" ilihali alishakuwa amekufa hivyo ni moja ya sababu kwamba tunaamini hakuandika kitabu cha mwanzo.

Kingine kuhusu hii sentensi ni kwamba ipo kwa wakati uliopita kimaandiko yaani mtu anasimulia experience ya jambo fulani na sio wakati uliopo sababu Musa amemaliza safari na amemkabidhi joshua alafu kauli itolewe kwamba WALA HAJAINUKA..... Haileti maana unless mwandishi alishaona manabii kama musa,joshua,obadiah n.k ndio akafikia hitimisho kuwa WALA HAJAINUKA.....

Mfano siku nyerere anamuachia mwinyi alafu mtu aseme HAJATOKEA Rais kama Nyerere ilihali hata mwinyi hajaanza kuongoza ita make sense kweli??
 
Nakubaliana na wewe kwamba musa alipewa maagizo akawaambie kwa sababu alikuwa nao karibu lakini kulikuwa na muweka kumbukumbu wake alieitwa yoshua
Lakini mpaka joshua anakufa hakukuwa ma kabila la wakaldayo sasa iliwezekanaje Joshua akarefer kabila ambalo halipo duniani yaani mtu aandike kwenye gazeti kuwa kabila la WAAMALEKI linaishi moshi ilihali hilo kabila bado hatujawahi liona moshi unafkiri message itaeleweka kweli?? Huoni alieandika hapa aliishi miaka mingi baada ya joshua baada ya kabila hili kuwepo duniani
 
We unavionaje hivo Vitabu?
Vinahekima?
Kina hekima sana tu mkuu ila mie nina shida na uandishi tu.... Je kwanini waseme kimeandikwa na Musa na wasiseme aliyekicompile alikuwa ni nani na kama anaaminika isije ikawa compiled na wapagani wachache wakaingiza maoni yao kwenye Biblia hasa mwanzo 6 na 10 ambazo zimezaa utata mkubwa sana kwenye kitabu cha mwanzo.
 
Embu weka hiyo mistari
Siwezi copy sura zote 14 mkuu ila kapandisha mlimani kwenye kutoka 24 sasa kama aliandika pentateuch huko je sura ya 27 na kuendelea iliandikwa lini na wapi ilihali inaeleza maisha ya baada Musa kushuka toka mlimani

Yaani kama pentateuch yote iliandikwa kwenye zile siku 40 zile sura zilizofuata baada ya tukio la kutoka mlimani zimeandikwa na nani na lini ilihali Musa alishakuwa ameshuka??
 
Nimekwambia sitaki kuamini. Nataka kujua.

Unaniuliza kama naamini katika physical world au ulimwengu usioonekana.

Umenielewa wewe?

Unaelewa kwamba inawezekana kitu kikawa katika physical world halafu kisionekane pia na hivyo swali lako halina mantiki?
kukuelewesha itakuwa ngumu sana.
tatizo hutaki kuelwa Ila unataka kubishana na kufanya hoja & mawazo yako ndiyo yawe huru.
kama upo na utayri wa kutaka kuelewa kubali kuwa humble
 
kukuelewesha itakuwa ngumu sana.
tatizo hutaki kuelwa Ila unataka kubishana na kufanya hoja & mawazo yako ndiyo yawe huru.
kama upo na utayri wa kutaka kuelewa kubali kuwa humble
Unataka kunielewesha kwa fact au kwa imani?
 
Lakini mpaka joshua anakufa hakukuwa ma kabila la wakaldayo sasa iliwezekanaje Joshua akarefer kabila ambalo halipo duniani yaani mtu aandike kwenye gazeti kuwa kabila la WAAMALEKI linaishi moshi ilihali hilo kabila bado hatujawahi liona moshi unafkiri message itaeleweka kweli?? Huoni alieandika hapa aliishi miaka mingi baada ya joshua baada ya kabila hili kuwepo duniani
Ndio maana nikasema hawakuandika kwa akili zao wenyewe Bali walisaidiwa kutoka juu
Ndio maana nikasema ukisoma kwa makini kitabu cha mwanzo ambacho huonyesha asili ya vitu vilipotokea utagundua aliyekuwa anatusimulia ni Mungu mwenyewe ambaye yeye anajua linalokuja mbele kuliko sisi binadamu
 
Mkuu cjui umeelewa concern yangu kwamba mtu anayesema WALA HAJAINUKA ni mtu mwingine.... Ikimaamisha Musa mwenyewe asingeweza kutoa hii kauli ya "majigambo" ilihali alishakuwa amekufa hivyo ni moja ya sababu kwamba tunaamini hakuandika kitabu cha mwanzo.

Kingine kuhusu hii sentensi ni kwamba ipo kwa wakati uliopita kimaandiko yaani mtu anasimulia experience ya jambo fulani na sio wakati uliopo sababu Musa amemaliza safari na amemkabidhi joshua alafu kauli itolewe kwamba WALA HAJAINUKA..... Haileti maana unless mwandishi alishaona manabii kama musa,joshua,obadiah n.k ndio akafikia hitimisho kuwa WALA HAJAINUKA.....

Mfano siku nyerere anamuachia mwinyi alafu mtu aseme HAJATOKEA Rais kama Nyerere ilihali hata mwinyi hajaanza kuongoza ita make sense kweli??
Hapa tunatofautiana jambo moja! Musa hakua akiandika maneno yake mwenyewe bali maagizo aliyopewa ma Mungu kupitia roho takatifu. Kwahiyo hilo neno HAJAINUKA au HAJATOKEA halimishi ni Musa aliandika kwa kujigamba bali ni Mungu alimwambia aandike vile kwa sababu ya imani Mungu aliyoiona kwa Musa. Kumbuka hili sio jambo pekee Musa alikoandika linalomuhusu yeye binasfi. Kuna wakati alimkosea Mungu na akapewa adhabu ya kutoingia nchi ya ahadi na bado aliandika mambo hayo. Hizo ndizo sababu zinasomfanya Musa kuwa mmoja wa watumishi waadilifu kabisa wa Yehova

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Hapa tunatofautiana jambo moja! Musa hakua akiandika maneno yake mwenyewe bali maagizo aliyopewa ma Mungu kupitia roho takatifu. Kwahiyo hilo neno HAJAINUKA au HAJATOKEA halimishi ni Musa aliandika kwa kujigamba bali ni Mungu alimwambia aandike vile kwa sababu ya imani Mungu aliyoiona kwa Musa. Kumbuka hili sio jambo pekee Musa alikoandika linalomuhusu yeye binasfi. Kuna wakati alimkosea Mungu na akapewa adhabu ya kutoingia nchi ya ahadi na bado aliandika mambo hayo. Hizo ndizo sababu zinasomfanya Musa kuwa mmoja wa watumishi waadilifu kabisa wa Yehova

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Lakini mkuu neno hili WALA HAJAINUKA limeandikwa baada ya Musa kufa je kama ni Mungu ndio alimuambia aandike ni muda gani ilihali limetamkwa baada ya kifo cha Musa ikimaanisha kulikuwa na mtu wa tatu aliyeripoti hii habari..... Na ndio naibua swali hapo kuwa alikuwa nani?? Na kama alikuwa mtu mwingine je kwanini tuambiwe muandishi wa kitabu cha mwanzo hadi kumb. Ni Musa

Hapo ndio nataka kuelewa mkuu
 
Hivi vitabu vinaitwa vitabu vya musa sio vitabu alivyondika musa

sababu ya kuviita vitabu vya musa ni kwa sababu matukio ya musa toka misri mpaka mlima sinai yaliacha maandiko ambayo kwa hayo watu waliweza kuandika story kamili kama mungu alivyokusudia

mfano
unaweza kusoma kitabu kinaitwa kitabu cha mkwawa
haimaanishi mkwawa ndie aliyeandika lakini matukio ya mkwawa ndio yamesababisha tupate story nzima
 
Hivi vitabu vinaitwa vitabu vya musa sio vitabu alivyondika musa

sababu ya kuviita vitabu vya musa ni kwa sababu matukio ya musa toka misri mpaka mlima sinai yaliacha maandiko ambayo kwa hayo watu waliweza kuandika story kamili kama mungu alivyokusudia

mfano
unaweza kusoma kitabu kinaitwa kitabu cha mkwawa
haimaanishi mkwawa ndie aliyeandika lakini matukio ya mkwawa ndio yamesababisha tupate story nzima
Mkuu kwenye machapisho yooote ya kiimani wanasema AUTHOR wa VITABU VYA MUSA ni Moses..... Ndio maana ikaleta maswali. Ila hiki unachosema ndio sahihi kwamba kuna WATU waliandika na wakatumia Musa kama chanzo cha taarifa zao.
 
Back
Top Bottom