Je, Mwalimu alihodhi maendeleo na kupeleka Butiama??

Je, Mwalimu alihodhi maendeleo na kupeleka Butiama??

Zanaki,

..Joseph Kizurira Burito Nyerere aliwahi kuwa Naibu Waziri, enzi hizo wakiita Waziri Mdogo, katika serikali ya Mwalimu Nyerere. nadhani ilikuwa miaka ya 60/70.

..sasa kwasababu Mwalimu alifanya mabadiliko ktk uongozi, na hakumrudisha Joseph ktk nafasi yake, ndiyo maana Kuhani anadai Joseph alikuwa "fired."

..labda kuna wachangiaji wanaoweza kutueleza sababu zilizomfanya Mwalimu Nyerere, amuondoe Joseph Nyerere ktk serikali yake.

Naona mada yako inazidi kupanuka sana, kinachoongelewa sasa hapa ni zaidi ya ulichoweka kwenye heading ya hii thread. Je uko tayari kusema kwa wazi zaidi unachotaka kiwe main issue ya huu mjadala?
 
Huyu Manyerere Jacton kesha toka Mtanzania alipokuwa mhariri?Mwenye nyeti atupe.Maana kama kaandika makala Raia mwema inawezekana kesha mwaga manyanga.Huyu jamaa alitumika sana kuwasaidia Rostam na Edward.Habari kama vile Lowasa apokelewa na magari zaidi ya mia 300 monduli.Watu wa Raia mwema wakimuacha ataanza kuandika makala za kuwasifia watu wake.Toeni nyeti huyu mtu bado yuko Habari Corp?
 
Magabe Kibiti said:
Naona mada yako inazidi kupanuka sana, kinachoongelewa sasa hapa ni zaidi ya ulichoweka kwenye heading ya hii thread. Je uko tayari kusema kwa wazi zaidi unachotaka kiwe main issue ya huu mjadala?

Magabe,

..haiwezekani kuthibiti na kulazimisha mwelekeo wa mjadala ktk mazingira kama ya jamii forums.

..mchangiaji wa kwanza kuleta jina la Joseph Kizurira Nyerere ni Bibi Ntilie. Kuhani na Zanaki wameongezea tu.

..lakini sidhani kama kuna ubaya wowote ule wa kumjua zaidi Joseph Nyerere. huyu ni kati ya waasisi wa Umoja wa Vijana wa Tanu.

..binafsi naiamini sana jamii forums. hili ni jungu kuu kwelikweli. at the end of the day ukweli hujulikana.
 
Zanaki

..Joseph Kizurira Burito Nyerere aliwahi kuwa Naibu Waziri, enzi hizo wakiita Waziri Mdogo, katika serikali ya Mwalimu Nyerere. nadhani ilikuwa miaka ya 60/70.

..sasa kwasababu Mwalimu alifanya mabadiliko ktk uongozi, na hakumrudisha Joseph ktk nafasi yake, ndiyo maana Kuhani anadai Joseph alikuwa "fired."

Daaaaah, huwa akitokea mtu mmoja akanielewa huwa nafurahi sana. Ha haa haaaa

Ni hivi: Katika mabadiliko yaliyopita ya baraza la Mawaziri la Kikwete, wakina Mramba, Juma Mwapachu, Juma Ngasongwa, Margaret Sitta, Zakia Meghji, Diallo, wote hawa walikuwa fired!!!

Ambao hawakuwa fired japo hawakurudishwa ni wawili tu, Kingunge Mwiru na Joseph Mungai, ambao Rais alisema wameomba kupumzika. Kwa nini unadhani Rais ali take the trouble kueleza kwa nini kuna watu wawili hakuwarudisha ? Maana yake ni kwamba alitaka ijulikane ni hawa wawili tu ndio hawakuwa fired!!!

Ndio maana nimesema Nyerere alim fire mdogo wake kwenye baraza la Mawaziri. Na mimi sijawahi kuuliza ni kwa nini alim fire kwa sababu alikuja kuwa wino mmoja ( mlevi wa kuokotwa okotwa) wa matapu tapu Mwananyamala Komakoma alikoishi miaka yake ya post-government life. Joka Kuu, ahsante kwa kunielewa.

Zanaki,

Unanishangaza kujiweka kama hujui maana ya Waziri kuwa fired. Halafu unasema Butiku ndio alisoma Tanzia ya Joseph Nyerere kwa hiyo historia yangu ni mbovu. Lakini kumbuka mwanzo umesema hivi: "Mwalimu hakuhusika na haya maendeleo na yeye mwenyewe alikiri yote haya siku ya mazishi ya marehemu mdogo wake."

Kwa maana hiyo unatuambia Julius aliongea siku ya msiba wa Joseph, akamsifia mdogo wake kwa kuleta hayo maendeleo. Ndio hiyo nasema "tanzia," yani kutoa wasifu wa marehemu! Hata kama Butiku alisoma Tanzia, hata Nyerere nae anaweza kusemwa alitoa tanzia hata kama hakuwa ana kikaratasi mkononi.

Nyerere alim fire Joseph Nyerere kwenye Uwaziri.
 
Kuhani,
Sawa kama unavyosema, Nyerere alim"fire" mdogo wake kwenye uwaziri. Sababu hata mimi sizijui kama vile mpaka leo sielewi ni kwa nini alim"fire" Babu kwenye uwaziri kama tulivyojadilia kule kwenye thread ya Babu. If you have any inside information it would be nice to hear it. Mimi hapa naapa sijui na hata wakati huo I was too young to ask. But if you have any info please share it with us.
 
jokaKuu,
Nakupata vizuri sana. Nimerudia kuisoma tena ile makala. Ninachofahamu mimi ni kwamba jitihada nyingi za maendeleo Butiama zilifanywa na marehemu Joseph Nyerere. Hata katika mazishi yake Mwalimu alikiri kuwa hajaifanyia Butiama kitu na hizi shule na hospitali mnazoziona alizianzisha Joseph. Sasa kuwa na posta sioni noma na wewe unaweza kuelewa usumbufu kwa Mwalimu kwenda Musoma mjini kupata barua zake. Pia ukiisoma makala utaona kuwa maendeleo yote hayo anayoyataja Jackton yalianza kufifia baada ya kifo cha Joseph Nyerere. Hata hivyo haiwiani kabisa na heading ya topic kuwa Mwalimu alihodhi maendeleo--inaashiria kuwa alitumia fedha ambazo labda zilikuwa zitumike Bariadi au Mugango na kuzipeleka Butiama. Bado nakupa changamoto ukipata muda utembelee Butiama ukajionee mwenyewe. Na kuhusu Butiama kuwa mji Mwalimu hakukubaliana na wazo hilo kwa sababu Butiama hakuna ardhi ya kutosha na kama Butiama itaamuliwa kuwa mji basi watahitaji eneo la kujenga makao makuu na miundombinu yote inayoendana na mji wa kisasa. After all Butiama is only 26 miles away from Musoma mjini do they really need another city especially now that the road is good and you can be in Musoma in 45 minutes?

Haya ni maneno ya wanaotaka kumchafua Marehemu badala ya kumuacha apumzike katika pumziko lake la milele kwa amani. Nimefika seheni nyingi sana Tanzania wakati Mwalimu akiwa madarakani na Butiama ikiwa ni mojawapo. Kuna sehemu nyingine nyingi tu zilikuwa na maendeleo makubwa ukilinganisha na Butiama.

Nyerere kama tunamvyomfahamu Watanzania wengi hakuwa na ubaguzi au upendeleo wa namna hiyo i.e kuhakikisha maendeleo yote yanapelekwa Butiama kwanza kabla ya mahali pengine popote pale Tanzania. Kama ingekuwa hivyo basi Butiama ingekuwa inafanana na ile miji mikali sana katika nchi za Ulaya au Amerika.
 


Haya ni maneno ya wanaotaka kumchafua Marehemu badala ya kumuacha apumzike katika pumziko lake la milele kwa amani. Nimefika seheni nyingi sana Tanzania wakati Mwalimu akiwa madarakani na Butiama ikiwa ni mojawapo. Kuna sehemu nyingine nyingi tu zilikuwa na maendeleo makubwa ukilinganisha na Butiama.

Nyerere kama tunamvyomfahamu Watanzania wengi hakuwa na ubaguzi au upendeleo wa namna hiyo i.e kuhakikisha maendeleo yote yanapelekwa Butiama kwanza kabla ya mahali pengine popote pale Tanzania. Kama ingekuwa hivyo basi Butiama ingekuwa inafanana na ile miji mikali sana katika nchi za Ulaya au Amerika.

Bubu Ataka Kusema,

"Muache apumzike" maana yake nini, tusimseme vibaya, au tusimjadili kabisa, au tuongelee mazuri yake ?
 
i agree with you. maendeleo gani butiama? no running water ( kulikuwa na mradi wa mkono kwa mkono kupeleka maji butiama, shule ya msingi butiama hoi kama zingine, kituo cha afya taabani kama vingine, hali ya umasikini kama vijiji vingine tanzania! indeed there was nothing exeptional about butiama. hata makumbusho ya mwalimu nyerere yalikuwa yanasikitisha. poorly maintained! poorly marketed! only last week nilikuwa arkansas kutembelea clinton presidential library...now thats a way to be remembered!

bottomline: butiama was no Gbadolite!
 
Back
Top Bottom