Je, Mwenyekiti wa Bunge la Katiba 2014 na Rais wa sasa, ni watu wawili Tofauti?

Kutoka 2014 hadi leo ni takriban miaka 9, nyakati zimebadilika kwa hiyo yale mawazo hayana nafsi. Twende na fikra mpya kabisa.

Kenya walipitisha wanayoiita Katiba ya wananchi mwaka 2010 na ndiyo ilimuwezesha Mwai Kibaki kutawala. Lakini alipokuja Uhuru Kenyatta mwaka 2017 kwenye awamu yake ya pili alaja na kitu kinaitwa BBI. Building Bridges Initiative ilkuwa inalenga kuzima mapengo waliyoyaona kwenye Katiba yao mpya.
 
Unaonaje tukishauri akae pembeni kupisha mabadiliko, maana ameonekana kuyumba kimaamuzi wakati tukiendelea na mchakato wa kupata Katiba mpya?
 
Mkuu angalia usije ukaambiwa umesema utamuangamiza raisi hawa mambuzi hawaeleweki tena
Hahaaa, usiogope, Uhaini ni vitendo Si maneno ya makabwela ya vijiweni, masokoni na mitandaoni.

NB: Gharama za kutosema ni kubwa kuliko Kutoa maoni juu ya nchi yetu nzuri TANZANIA.
 
Hahaaa, usiogope, Uhaini ni vitendo Si maneno ya makabwela ya vijiweni, masokoni na mitandaoni.

NB: Gharama za kutosema ni kubwa kuliko Kutoa maoni juu ya nchi yetu nzuri TANZANIA.
TANGANYIKA
 
Hivi katiba ya mwaka 1977 ilifata huo utaratibu kwa kifupi anafuja pesa na Hana Nia ya dhati kusimamia mchakato wa katiba mpya.
 
Kwahiyo unaniambe kwa katiba ya USA ambayo imetengenezwa miaka 200 iliyopita hiyo si itakuwa takataka sio au?
 
Yaani duniani khaa!!
 
Swali lako linafikirisha,

Kumbe inawezekana kumshtaki aliyekuwa mwenyekiti wa Bunge la Katiba 2014 maana ni watu wawili tofauti au sio?
Maana yangu ni kuwa ni Katiba Ina weka huo ulinzi wa yeye kuto shitakiwa Kwa jinsi yeyote Ile na siyo moral codes...So kama tunaishi na moral codes bila frame ya Katiba basi, kama Mimi nime m judge yeye immoral Kwa kitendo hicho kama ulicho sema basi let us use the same moral na siyo Katiba

Kama hiyo haiwezekani basi Katiba ndiyo msingi wa haya yote
 
Hapa ndipo inadhihirika wazi kwamba wengi hatuufahamu mfumo wetu unavyofanya kazi. Alifanikisha malengo ndiyo maana akapongezwaa! Unataka uzabwe kibao ndiyo uzinduke?
Akapongezwa kwa kuwa makamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…