Je, natakiwa kuwa na roho mbaya Ili nifanikiwe?

Je, natakiwa kuwa na roho mbaya Ili nifanikiwe?

Prakatatumba abaabaabaa

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2022
Posts
1,842
Reaction score
6,087
Ni jioni Sasa napanda Kitandani kupumzisha fuvu langu nikitafakari mambo yaliyotokea leo.

Mpaka muda huu nimepokea simu 3 kutoka kwa washikaji zangu tuliosoma nao chuo wanafunga ndoa simu za usumbufu ni Kila siku, jirani yangu hapa mtoto wake anapata kipaimara kesho anaomba mchango, napigiwa simu na baba yangu mdogo nitume mchango wa harusi ya dada angu, mjomba ananipigia simu nim-support kwenye ndoa anayofunga. Mimi sikufanya sherehe ya ndoa kwa sababu ya kuepuka gharama na kusumbuana na watu, nilienda na wife kwa mchungaji tukamaliza ofisini.

Marafiki zangu wanaomba pesa kidogo tu hata ya vocha 5000-10,000 (Hawa ni washikaji zangu haswa ambao siwezi kuwatupa).

Bado mdogo wako anakutafuta umpe Hela ya graduation ya form four, Hapo sijarudi kwenye familia yangu hapa mambo ni mengi mnoo Bado wazazi wa pande zote mbili, Kodi ya nyumba n.k kipato chenyewe 400,000/= kwa Mwezi.

Nimeona Ili kuepuka lawama kutoka kwa watu nawaza kubadilishana Laini ya simu kabisaaa, Kuna kitu nimekigundua mtu Ukiwa na roho nzuri basi sahau kuishi Maisha unayoyawaza utajikuta nusu au robo tatu ya kipato Chako wanatumia wengine.
 
Unahitaji mfumo mzuri wa maisha na matumizi mazuri ya resources, sio roho mbaya.

Kumbuka roho mbaya itakutenga na watu wenye manufaa na wewe, tumia akili sana kuwaminya wanyonyaji wa maendeleo yako, usiwaonyeshe wazi wazi ila waweza kuwakwepa huku unawachekea maana hujui utawahitaji lini.
 
Wanaume wote mnaohonga ili mpate Nyapu ikiwemo wewe unayesoma hapa jua ni Punguwani na limbukeni,

Wanawake Wote mnaohongwa ili utoe uchi wewe Ni Malaya muuza uchi.

Mwanamaume Anayezidiwa akenda zake Liverside usijali hio inajulikana ni Biashara..
Wapiga Nyeto Hoyeeeeeeeee....
Waaminifu kwa wenza hongereni.

Rubish.
 
Umekasirishwa na kuongeza A mwisho wa ID yako?

Next time usituchokoze watu wa kanda ya ziwa

Kama unadhani nimekasirika basi utakuwa na matatizo. Na kama hicho nilicho andika ni uchokozi basi tatizo lako litakuwa ni kubwa mara mbili yake.

Nimemuuliza " wewe ni msukuma" kwa sababu najua:

1. Wasukuma ni wakarimu sana.

2. They are so generous.

3. They are so giving.

4. Wana upendo na huruma.

5. Hawawezi kumkatalia mtu mwenye shida pindi awaliliapo shida.

N.a. hata wao wenyewe wakiwa na shida huwa hawapendi kuwasumbua watu wengine kwa sababu hawapendi kuonekana na shida. Unaweza KUKUTANA na.msukuma kapigwa bangili ( pingu) akamuuliza " Ngosha vipi kuna nini ?" Akakujibu " Ndoho tabu lolo" yani hakuna shida.


Kuna .msukuma.mmoja alikamatwa uzururaji pale urafiki. Ndugu zake wasukuma wameenda kuonana na mkuu wa kituo akawauliza " mna shida gani" wakamjibu " ndoho tabu"

So wewe ngosha wacha utoto huo wa kukasirishwa na kikomenti kilicho taka kabila lako hata kama.ningekuwa nimewatukana wasukuma.kweli
 
Sidhani kama ni roho mbaya pale unapoacha kumsaidia mtu kwa sababu jambo lipo nje ya uwezo wako.

Usijibebeshe mzigo wa kusaidia kila mtu, na wakati mwingine unatanguliza lile lililo na umuhimu zaidi, sio kila jambo ni la kulipa kapaombele.
 
Hapana.

Yule anaefanya ubahili basi anaifanyia ubahili nafsi yake, fanya utakavyofanya vile utakavyo fanya ndivyo utakavyolipwa
 
Unahitaji mfumo mzuri wa maisha na matumizi mazuri ya resources, sio roho mbaya.

Kumbuka roho mbaya itakutenga na watu wenye manufaa na wewe, tumia akili sana kuwaminya wanyonyaji wa maendeleo yako, usiwaonyeshe wazi wazi ila waweza kuwakwepa huku unawachekea maana hujui utawahitaji lini.
Ni kweli, maana nikisema nisaidie Kila mtu sitoboi
 
Back
Top Bottom