Je, ni busara kujenga nyumba kwa milioni 150 kisha kukusanya kodi laki 6 kwa mwezi?

Je, ni busara kujenga nyumba kwa milioni 150 kisha kukusanya kodi laki 6 kwa mwezi?

Haya mambo ya mazoea tuachane nayo, tuendane na economic and Market trends.
5 to 10yrs ago watu walinunua viwanja kwa pesa nyingi sana , yaani from 30m to 60m . Leo hii wanauza kwa 20m tena kwa mbinde. Kuna majumba kibao mjini hayana wapangaji na hayauziki.
So sekta ya Real Estate inaporomoka na kupanda kama sector nyingine , but this time imeporomoka sana.
 
Kiwanja maeneo yaliyochangamka utanunua kwa pesa ngapi?unafahamu kwamba maeneo ya nje ya mji Kama Tegeta au Kimara maeneo karibu na barabarani hiyo pesa yote inaishia kwenye kiwanja?
Hizo bei zilikua wakati wa JK now 25million inakupa kiwanya kikubwa kabisa kufanya fujo zote vijana acheni stori za vijiweni
 
Haya mambo ya mazoea tuachane nayo, tuendane na economic and Market trends.
5 to 10yrs ago watu walinunua viwanja kwa pesa nyingi sana , yaani from 30m to 60m . Leo hii wanauza kwa 20m tena kwa mbinde. Kuna majumba kibao mjini hayana wapangaji na hayauziki.
So sekta ya Real Estate inaporomoka na kupanda kama sector nyingine , but this time imeporomoka sana.
Watu hawana pesa mkuu[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Hizo bei zilikua wakati wa JK now 25million inakupa kiwanya kikubwa kabisa kufanya fujo zote vijana acheni stori za vijiweni
Sio story za vijiweni inaonekana wewe ndio hujui thamani halisi ya pesa.
Hiyo ni Bei ya Goba au madale mkuu ambapo bado hapajachangamka vizuri.
Najua thamani ya viwanja,Mimi sio kijana ninayeishi kwa baba namiliki nyumba ndio maana naongea kitu ninachokijua.
 
Unachosahau ni kuwa baada ya miaka 29 lazima uwe umefanya ukarabati mara kadhaa (ikiwemo kubadilisha paa, nyaya za umeme na design kadhaa za nyumba. Pia, design za miaka hiyo usidhanie utampangisha mpangaji wa maana zaidi ya wanachuo na mateja
Mateja watapata wapi ela ya kupanga?
 
Nilikua nalipa nyumba laki 6 mwaka 2016 Mikocheni nimehamia Sinza kodi 250,000/= Tshs. Toka nimehama Mikocheni ile nyumba mpaka Leo haijapata mtu. Mwenye nyumba ananipigia simu nirudi atanipunguzia kodi 50% (300,000 Tshs.) Ha ha ha!
Chibu si ukampangishe bureau de change pale
 
Kwa ufupi tu, ASSET ni kile kitu kinachokuingizia PESA! Chochote kinachokuchulia PESA ni LIABILITY. Nyumba ya kuishi tu ni liability inachukua PESA in forms of kodi/malipo ya umeme, kodi ya ardhi, kodi ya jengo n.k. Lakini ka a umeipangisha, itakuletea PESA utakayotumia kulipia hizo bili. Hautatoa hiyo PESA kutoka kwenye aidha mshahara wako au vyanzo vingine vya mapato. Hiyo ni kwa ufupi tu.
Argument yangu bado ipo pale pale. Kama inatoa tu pesa haiingizi, si bora uigawe tu?
 
Wahindi walijenga nyumba asilimia 98 zilizotaifishwa na kufanywa NATIONAL HOUSING,soma katika hayo maghorofa kama hukuti majina ya kina LADWA,LALJI,KANJI nk,ni baada ya AZIMIO la Arusha ndiyo wahindi waliacha kujenga,unataka kutudanganya hata historia mbovu ambayo haijamaliza karne moja?
Na hii ndio hofu yetu watanzania wengi.
Huwa hatujiamini kwenye biashara,lakini sababu inatokana na lack of business knowledge.
Ndio maana wote tumekuwa na utamaduni wa kujenga tu au kuziacha hela benki kwenye saving account.
Ila wahindi huwa hawana hobby ya kujenga majumba wapatapo pesa Wana njia zingine za investment Kama kununua bonds/shares au other liquid assets Kama golds na kuzihifadhi ndani.
Siku akifirisika anauza kwa Bei ya juu na kuibuka tena.
 
Soma majina ya hizo nyumba kama hazikiwa za babu zao na leo wanapangishwa,waliacha kujenga baada ya AZIMIO LA ARUSHA,acheni uvivu wa kukifunza mambo.
Wale Watanzania wenzetu wenye asili ya Asia mbona huwa hawajengi? Wanaishi national house tu. Na Wana uwezo mkubwa tu maana watoto wait wanasoma shule za garama na wanaendesha magari ya kifahari.
 
Upumbavu wamekupa,wao wanamajumba CANADA,hapa walijenga wao majumba yote ya msajili baada ya kutaigishwa wakaacha,we zubaa tu,soma majengo ya msajili yana majina ya kinanani.
Hahahaha,kumbe umegundua mkuu.
Mimi nilikuwa na rafiki zangu wahindi tunafanya nao kazi ndio walinifungua akili.
Walikuwa wananiuliza umeinvest kiasi gani Hadi Sasa na akaunti yako Ina pesa kiasi gani?
Mimi nikawa nawajibu sina kitu hela zote nimenunua kiwanja na kuanza ujenzi,Kisha wananiuliza kwa mfano ukifukuzwa kazi ghafla utafanya nini?
Basi walikuwa wananicheka sana.
 
stupid mind
Mkuu mm nimeamua ku-invest kwenye Career & biashara za vifaa vya ujenzi at least kila mwezi na-save 500,000/= kutoka kwenye mshahara pia nina Hardware Tegeta hata ikitokea lolote naweza ku-survive kwa kipindi kirefu. Sasa wewe jiloge ukajenge Msata kazi izingue utakula tiles
 
Wahindi walijenga nyumba asilimia 98 zilizotaifishwa na kufanywa NATIONAL HOUSING,soma katika hayo maghorofa kama hukuti majina ya kina LADWA,LALJI,KANJI nk,ni baada ya AZIMIO la Arusha ndiyo wahindi waliacha kujenga,unataka kutudanganya hata historia mbovu ambayo haijamaliza karne moja?

Wahind hawataki kurudia upuuzi waliofanya [emoji23][emoji23]
 
Ngwanakilala,
Mi sahihi, mfano kama jmri wak ni miaka kuanzia 50 na kwenda mbele ,maana nguvu zinaanza pungua na ufanisi..
Utapata kodi (cash) pamoja na ongezeko LA thamani ya eneneo (20% Kwa mwaka) na. Zaidi
 
Ngwanakilala,
Pia kuna tatizo naliona hapa.
He, nia ilikuwa iwe nyumba ya kupangisha toka mwanzo? Imejengwa wapi?
Nauliza maana kwa hela hiyo upo uwezekano wa kujenga nyumba tatu za kupangisha na kuingiza 1.5M kwa mwezi.
Naandika from practical experience.
 
Naomba kukurekebisha. Thamani ya Ardhi huongezeka kadri muda unavyosonga, bali thamani ya nyumba hupungua kadri muda unavyozidi kusonga. Jaribu kufikiria leo hii unajenga nyumba yako kwa sh 100M, je ukitaka kuiuza baada ya miaka 15 unadhani utauza utaiuza kwa zaidi ya 110 ?
Bei ya nyumba inatokana na sifa mbalimbali kama location yake, improvements unazofanya kila mara n.k. Mfano kuna nyumba nilinunua 2005 kwa mil kadhaa. Nikakarabati kidogo ikapanda thamani. Leo nikiuza ni pesa ndefu sema fixed assets kwa sasa kuuzika kwa bei nzuri ni mtihani. Kama huna tatizo la fedha kamwe usiuze asset kwa sasa hailipi. Na ukichukulia mkopo kwa thamani ya asset yako kama ni ya thamani kubwa na mkopo mkubwa usipokuwa makini utaikabidhi huko taasisi za fedha jumla.
 
Bei ya nyumba inatokana na sifa mbalimbali kama location yake, improvements unazofanya kila mara n.k. Mfano kuna nyumba nilinunua 2005 kwa mil kadhaa. Nikakarabati kidogo ikapanda thamani. Leo nikiuza ni pesa ndefu sema fixed assets kwa sasa kuuzika kwa bei nzuri ni mtihani. Kama huna tatizo la fedha kamwe usiuze asset kwa sasa hailipi. Na ukichukulia mkopo kwa thamani ya asset yako kama ni ya thamani kubwa na mkopo mkubwa usipokuwa makini utaikabidhi huko taasisi za fedha jumla.
'Leo nikiuza ni pesa ndefu sema fixed assets kwa sasa kuuzika kwa bei nzuri ni mtihani'.

Umejichanganya kwny hio sentensi.

Sasa utamuuzia nani akupe hio pesa ndefu?
 
'Leo nikiuza ni pesa ndefu sema fixed assets kwa sasa kuuzika kwa bei nzuri ni mtihani'.

Umejichanganya kwny hio sentensi.

Sasa utamuuzia nani akupe hio pesa ndefu?
Kajichanganya wapi?? Mbona kaongea vizuri tu...Amesema kwa sasa haiuziki kwa hizo bei kubwa.
 
Back
Top Bottom