Je, ni kwanini kila anaeanzisha biashara ya daladala lazima ife na afilisike?

Je, ni kwanini kila anaeanzisha biashara ya daladala lazima ife na afilisike?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
38,920
Reaction score
44,970
Hivi hii biashara ya daladala inachangamoto zipi hasa hadi kupeleke wamiliki wake kuamua kuyauza baada ya muda ili kuepuka kufilisika, nilitaka ninunue walau 2 nione inakuaje, lakini nakatishwa tamaa ninapoona biashara hizi huwa zinafilisi watu
 
Duh nunua mkuu mbona kuna Mabasi ya Zuberi na Super najmunisa tangu nimezaliwa nimeyakuta na bado yapo
 
Ku maintain magari ya biashara hususan ya usafiri wa watu si jambo rahisi!

Gari linapotumika mara kwa mara wear and tear yake nayo ni kubwa.

Kukiwepo na wear and tear maana yake lazima iwepo na repair.

Na repair za magari si hela ndogo.
 
Mmh.. mkuu nakushauri hebu kaa tuliza akili kwanza yawezekana kuna mengi yamekuvuruga.
Mana daladala zimejaa road na daily zinanunuliwa hili wazo umelitoa wapi? Wataka sema wamiliki wote washatangulia mbele ya haki! !! Hapana mkuu labda kama huu uzi wako umeleta kwa lengo la kuchekesha. Pole sana kwa mawazo mgando na mfu.
 
Ku maintain magari ya biashara hususan ya usafiri wa watu si jambo rahisi!

Gari linapotumika mara kwa mara wear and tear yake nayo ni kubwa.

Kukiwepo na wear and tear maana yake lazima iwepo na repair.

Na repair za magari si hela ndogo.

Plus madereva wanapiga sana...halaf kila siku ni fine na kuleta hesabu nusu.
 
Hizo zinazozagaa barabarani zinamililiwa na Masokwe????
Mnavosema kila anayeanzisha lazima biashara ife... Hata hapa naenda kupanda Daladala.
Acheni mawazo ya kiboya nyie.
Kaa na dereva kisha zungumza nae mawili matatu kuhusu kazi ya daladala..grammar ilotumika kwenye lugha ya heding isikutie upofu...boya wewe
 
upange mapato na matumizi vizuri usisahau daladala zinachosha sana magari kwa hiyo matengenzo na kulibadili baada ya muda kabla halijaanza kufyonza mapato kwa nguvu. Pia usisahau kubajeti pesa za kupolish viatu na kodi nyinginezo
 
Ni biashara nzuri sana kama ukinunua gari mpya, gari kama Eicher hurudisha hela kati ya miaka 1 na miezi 8_ 2yrs. Na ukiiangalia gari iliotumika miaka 2 ni bado iko poa sana! Mimi nina Eicher yenye miaka 3.9 mpaka sasa, huwa IPO servs j.Pili tu na siku zote za kazi IPO barabarani. 130,000 @ day"
Nakuhakikishia mkuu inafaida!
Wanaofilisika ni wale wanaonunua magari second hand, gari limetumika mtu karudisha hela yake na kapata na faida akiona tu injini linaanza kupungua nguvu hasubiri kufanya overhall, analiuza anapata faida zaidi na ananunua jipya lingine, anaeenda kuumia ni mnunuaji ambaye baada ya muda labda miezi 6 ya kupata hela vzr,
Linaanza season ya natengeneza mengi makubwa yanayohitaji hela nyingi na kama hakua amejipanga ndo hao wanaofilisika'
Na anaweza sema kalogwa kwsbb kila akitengeneza hiki kiazuka kile! MB🙁kwenye gari ukiona injini imechoka ujue vitu vingi vikubwa navyo vitafuatia!)
Na kitu lingine ktk daladala ni hesabu, ukiwa kubwa gari inachoka haraka sana na gari zenye hesabu ndogo ndo zile unaziona mchana imepaki wanakula,
Usiku unakuta imeoshwa vzr imepaki mapema na inakuwa haina Shida sana na trafiki (vyeti) ksb haina sababu ya kuvunja sana sheria za barabarani.
 
Ni biashara nzuri sana kama ukinunua gari mpya, gari kama Eicher hurudisha hela kati ya miaka 1 na miezi 8_ 2yrs. Na ukiiangalia gari iliotumika miaka 2 ni bado iko poa sana! Mimi nina Eicher yenye miaka 3.9 mpaka sasa, huwa IPO servs j.Pili tu na siku zote za kazi IPO barabarani. 130,000 @ day"
Nakuhakikishia mkuu inafaida!
Wanaofilisika ni wale wanaonunua magari second hand, gari limetumika mtu karudisha hela yake na kapata na faida akiona tu injini linaanza kupungua nguvu hasubiri kufanya overhall, analiuza anapata faida zaidi na ananunua jipya lingine, anaeenda kuumia ni mnunuaji ambaye baada ya muda labda miezi 6 ya kupata hela vzr,
Linaanza season ya natengeneza mengi makubwa yanayohitaji hela nyingi na kama hakua amejipanga ndo hao wanaofilisika'
Na anaweza sema kalogwa kwsbb kila akitengeneza hiki kiazuka kile! MB🙁kwenye gari ukiona injini imechoka ujue vitu vingi vikubwa navyo vitafuatia!)
Na kitu lingine ktk daladala ni hesabu, ukiwa kubwa gari inachoka haraka sana na gari zenye hesabu ndogo ndo zile unaziona mchana imepaki wanakula,
Usiku unakuta imeoshwa vzr imepaki mapema na inakuwa haina Shida sana na trafiki (vyeti) ksb haina sababu ya kuvunja sana sheria za barabarani.
Asante kwa Maelezo mazuri kiongozi yaani umeekeweka vizuri, umeongelea kuhusu kununua second hand unatushauri nini sisi wenye mitaji midogo tukitaka kununua binafs nahiaji hiace superoof
 
Back
Top Bottom