Je, ni kweli kuwa hadi Rais Magufuli anafariki mfuko wa UREA Kg 50 ulikuwa Tsh. 50,000/- leo umefika Tsh. 147,000/-


Punguza jazba mama, mambo kama haya hayahitaji hasira. Kunywa maji utulie halafu uje tena kueleza, sababu za kuzuia na si nani alizuia. Tukijua sababu, ndiyo tutajua namna bora ya kurekebisha mapungufu kama yapo.

BTW, pole kwa kugusa nerve zako maana umeongea kwa hasira sana.

Tuweke hisia kando na kutumia uwezo wetu wa kufikiri vizuri.

Uwe na asubuhi njema.
 
Anza kufikiri wewe unaekuja na negativty tu. Zitakujenga hizo. Umejazwa ujinga na umekujaa.

Kazi ya Mungu haina makosa.
 
Anza kufikiri wewe unaekuja na negativty tu. Zitakujenga hizo. Umejazwa ujinga na umekujaa.

Kazi ya Mungu haina makosa.

Ingependeza kama ungetenganisha hoja na mtoa hoja. Ninaloliona hapa hoja ya msingi umeitupia pembeni, na kuanza kumshughulikia mtoa mada. Anyways, sikulaumu, hiyo inatokana na aina ya watu walio na wanao kuzunguka. Umezoea kila unachoongea wanaokuzunguka hukichulia kama rejea yao. Hawakihoji, badala yake ni kukimeza kama dodoki. Sasa kwa upande wangu ni tofauti, nazungukwa na watu wanao hoji. Ukijibu hoja zao kwa njia bora yenye kuridhisha, watakuelewa. Vinginevyo siyo rahisi. Ndiyo maana mara zote nakuwa muangalifu sana kuongea bila kuwa na mantiki ya ninachoongea.

Faiza mambo yanabadirika, jaribu kudhibiti hisia ili upate kumjibu kila mmoja bila kumtweja, kumvunjia heshima, kumtisha n.k.

Pamoja na yote bado, suala la msingi la SABABU ZA KUSITISHA na SI NANI KASITISHA HALIJAJIBIWA.
 
Nimekwambia endelea na ujinga wako rasmi. Majibu yakutosha nimekupa na mafunzo ya kutosha nimeshakupa, yamekuingia, sasa unatapatapa tu kutafuta pakutokea.
 
Nimekwambia endelea na ujinga wako rasmi. Majibu yakutosha nimekupa na mafunzo ya kutosha nimeshakupa, yamekuingia, sasa unatapatapa tu kutafuta pakutokea.

Hakuna jibu ulilotoa zaidi ya kunishambulia kwamba mimi ni mjinga.

Hujatoa SABABU ZA KUZUIA ULE MRADI.

BTW nani aliyekupa mamlaka ya kumtangaza fulani kwamba ni mjinga.
Vigezo gani na vilikubalika na kupitishwa na chombo gani kwamba mtu awaye yote asipovifikia basi yeye ni mjinga!!?

Kwa mtu mwenye uelewa wa kawaida kabisa, anatambua kwamba hatuwezi wakati wote tukakubaliana katika mambo yote na watu wote. Nyakati nyingine tunatofautiana. Tuheshimu maoni ya watu wengine licha ya kuwa hatuyakubali. Huko kunaitwa kukubaliana kutokubaliana.
Tuache maoni ya kimagharibi yanayagikiri demokrasia ya magharibi ni ya dunia, yeyote ataeendea kinyume siyo mdemokrasia. Wanashindwa kuelewa kuwa demokrasia inajengwa na tamaduni na desturi za watu husika. Kwa kuwa tamaduni zinatofautiana, hali kadhalika demokrasia nayo itatofautiana.
Hivyo lazima tuwe na uwezo wa kuzikubali tofauti.
 
Magufuli Alikua na Uwezo wa Ziada usio wa kawaida .
Mbona sukari ilimshinda kama alikuwa na uwezo wa ziada?Sukari imemsumbua huku viwanda vya sukari vikiwa hapahapa nchini.Tunduma wanatumia sukari kutoka Zambia tsh 2000 kwa kilo wakati nchini ni kizungumkuti na ilimshinda.Na wamiliki wa viwanda vya sukari vya Zambia na tz ni wamoja.

Urusi ndio mzalishaji mkubwa wa mbolea duniani na kwa hali ilivyo sasa huyu hayati mnampa sifa za bure.

Mwendazake alikuta tsh against dollar haiko vizuri,amesadia nini?Ningemuona wa maana angeirudisha walau thamani sawa na utawala wa Mkapa ambapo watu waliweza kuagiza fuso kutoka dubai kwa around 20m ambapo yeye mpaka anakufa kuagiza fuso mpaka inafika nchini ni around 70m lakini yote hii sababu ya thamani ya dollar kupanda.

Zaidi ya roho mbaya hayati hakua na jipya.
 
Mie ni muuuzaji wabolea karibia za kampuni zote huo ndio ukweli
 
Hiyo 50,000 si kipindi kile inazalishwa kiwanda Cha Minjigu kule Arusha Jiwe akakiua?
 
Mkuu kuna hili lingine je vifurushi kupanda bei napo linachangiwa na vita ya urusi&ukrein
 
Hatukatai, pengine vita nayo imechangia kwa kiasi fulani kupanda kwa bei. Lkn tunataka kuona kwa upande wetu ndani, ni hatua zipi zinachuliwa kudhibiti hilo hata kwa kiasi tu.
Imepanda kabla ya vita mkuu wangu ndo maana nyanda za juu kusini msimu wa mahindi walishundwa kutumia mbolea sababu ya ghatama
 
Hapo ni ukweli mtupu. JPM alikuwa mfuatiliaji na alikuwa anazimudu hesabu, kwa hiyo ilikuwa bidhaa ikiongezwa bei anamwita Waziri, wanakaa chini wanaanza ku calculate ili kubaini uhalali wa kuongeza bei kwa kiasi kile. Akikuta hakuna ukweli ndani yake, anatoa maamuzi ya papo kwa papo kwamba bei haitakiwi kuongezeka kwenye bidhaa husika.
Kwa bahati mbaya kwa sasa siyo hivyo.

Kwa JPM ilikuwa ukitaka kupeleka hoja ya kupandisha bei za bidhaa ni lazima uwe umejipanga kweli kweli kwa sababu utapigwa maswali mengi kabla ya kufikia mwafaka.
 
Mbolea ipande huko duniani wewe usingizie kufa kwa Mwendazake!

Chuki zako kwa serikali ya awamu ya sita zitakuua bure!
Mbona Kikwete aliacha bei ya sukari sh 600/kg lakini Mwendazake alipoingia ikaruka hadi sh 1,800? Zungumzia hili pia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…