Je, ni kweli kuwa Wanyama wa Tanzania huenda kupata mimba Kenya kama alivyosema Rais Samia?

... kupata watoto/kuendeleza kizazi sio jambo la mzaha lazima maandalizi yawepo hata wanyama wanajua hilo.
 
Hiki Ni kweli ndiyo ile world greatest wildebeest migration. Yakadiriwa wanyama Milion 20 huvuka mto Mara kati ya mwezi Julai na August kutoka Serengeti kwenda Masai Mara kutafuta maji na malisho. Na hurudi Tanzania mwezi November

Hata flamingo nao huja lake Natron kwa msimu fulani wanafanya mating, the wanaondoka kwenda kuzakua elsewhere
 
Kwa upana zaidi wa hii statement, Rais katuaibisha sana wanaume wa Tz.
kwani kulikua na kasoro gani angesema hao wanyama wanakuja kugongwa tz na kwenda kuzalia kenya?
kawapa wanaume wakenya silaha ya kututania..
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
MK254
 
Mimi naona kuna shida kwenye uwezo wa kuchambua mambo muhimu ya Taifa. Kwani hayo wanyama wana uraia?
 
Nina wasiwasi na uwezo wa kupambambanua na kuchambua mambo wa Rais wetu!
 
Je! ni kweli wanyama wa Tanzania wanakwenda kupata mimba.

Hapa naomba nizungumze juu ya makundi ya wanyama wawili ambao ni Nyumbu (wildabeest) na Pundamilia (Zebra) ambao wanaishi ndani ya Hifadhi ya Serengeti (Serengeti Migration)

SERENGETI MIGRATION
Hili ni kundi kubwa la Nyumbu (wildabeest) wapatao 3Mil pamoja na Zebra 2Mil wanaoshi pamoja na kufanya safari zao pamoja.
Kwanzia mwishoni mwa mwezi wa 12 makundi haya mawili huwa yamewasili eneo la kusini mwa Serengeti ambapo kuna tambarare kubwa na nyasi fupi zenye kiwango cha kutosha cha Madini ya calcium (kwa ajili ya maziwa ). Makundi haya hulitumia eneo hilo kwa muda wa miezi 4 kwa ajili ya kuzaa watoto (breeding season) ifikapo mwezi Mach makundi haya huwa wameshamaliza uzazi na kuanza safari ya kwenda North Serengeti ready for crossing Mara River entering to Masai Mara Np in Kenya.
Kitendo cha kuvuka mto Mara huwa kinaanza mwezi wa 8 na 9 kisha mwezi wa 10 huvuka tena kurudi Serengeti Tanzania

GESTATION PERIOD
Wanyama hawa hubeba mimba kwa siku 217 mpaka miezi 4 na nusu.
Hapo utaona kuwa mimba hutungwa mwezi wa 8 na tisa (hutungiwa Kenya). Vile vile huzaa kwanzia mwezi wa 1 na 2 (Huzalia Tanzania)

Makundi haya huishi na kusafiri pamoja Madume na majike. Kimsingi hawaendi Kenya kutafuta Madume bali hukimbia kiangazi Kikali kinachopatikana ndani ya Hifadhi ya Serengeti mwezi wa 8 na 9.

Madame Samia yupo sahihi na anaelewa mambo kwa kina na wala sio mtu wa kukariri mambo na namba kama .........

Kenya kuna UHURU Tanzania tuna SULUHU sasa ushindwe mwenyewe
 
Kwahio Lodge na Guest za wanyama wetu ziko maeneo ya Kenya au sio πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚!!
Ila hospitali za kujifungua ziko Tanzania, inapendeza sana!
 
Yawezekana kipindi baadhi wanyama wanapohamia Kenya ndio kipindi cha kuzaliana.ni vitu vinavyowezekana.fuatilia sana habari za wanyama utapata jibu.
 
Tanzania kwa sasa ni Ke (kwa sababu Rais ni ke).

Kenya ni me.

Ukute Rais wetu kawaza Kama hivyo juu.
 
Kwa upana zaidi wa hii statement, rais katuaibisha sana wanaume wa Tz.
kwani kulikua na kasoro gani angesema hao wanyama wanakuja kugongwa tz na kwenda kuzalia kenya?
kawapa wanaume wakenya silaha ya kututania..
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
MK254
πŸ˜†πŸ˜
Hapana bana, hatujazalilishwa.
Hapo Kenya hutumika kama Guest House tu, yani hao wanyama wanaishi Tanzania kwa maisha yao yote ila mwezi mmoja kila mwaka Huenda kenya for honeymoon kisha kurudi Tanzania.

Mama yupo vizuri sana kwa Tamathali za semi ila ukiwa mwepesi kichwani anakuacha mtupu
 
Kipi cha ajabu hapo?
 
Sio wanyama tu hata ndege na samaki wa bahari ya Hindi
 
Ni utaratibu wa kila mwaka ambapo nyumbu uhama kwenda Kenya wakisha beba mimba hurudi kuzalia Serengeti, ( kusini mwa Serengeti) soma kuhusu Wilderbeest migration.
 
Wanyama wanapandana (mating)kwa msimu, basi msimu huu unakuwa baada ya migration kutoka TZ kwenda Kenya, na warudipo wana mimba. Ndio maana Tz kuna wanyama wengi zaidi ya kenya. Pia hao wanyama wanaopandana ni wakewale waliovuka pamoja
[emoji848] na wakishazaa wanazaa majike tu au..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…