Je ni kweli mashujaa FC wa Kigoma ni wachawi?

Je ni kweli mashujaa FC wa Kigoma ni wachawi?

carnage21

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2023
Posts
591
Reaction score
1,382
Kwa Ujumla jibu ni HAPANA.

Namna ya ushangiliaji wa Mashujaa FC umekua ukihusishwa na imani za uchawi jambo ambalo kiuhalisia siyo kweli bali ni namna ya kujitofautisha na ushangiliaji wa Mashabiki wa timu nyingine.

Tuanzie kwenye logo ya Mashujaa FC ukiiangalia ni logo inayotambulisha Mnyamapoli ambaye ni wa asili, Hapo kwenye "ASILI" ndipo na ushangiliaji wa mashujaa FC ulipoanzia na hatimaye Mashabiki wa mashujaa kuja na ushangiliaji wao wa kipekee ukiwahusisha watu waliobeba zana za jadi na kuvalia kijadi au kiasili.

Namna ya uvaaji wa nguo hiyo nyekundu inaitwa "Lubega" kwa Kiha. Hiyo ndiyo namna ya asili ya uvaaji ya watu wa kigoma "Waha" kama ilivyo kwa wamasai.

Chungu na mapambo yake ikiwemo kioo ni namna ya kunogesha tu mwonekano na wala siyo kwamba kimebeba uchawi ndani yake.

FB_IMG_16879406954464263.jpg
 
Timu zote Tanzania zinatumia uchawi, wanachoshindana na wataalam tu.

Inawezekana Mashujaa wana Mtaalam wa viwango vya juu, ila uchawi bila kuwa na timu bora ni kazi bure kabisa.

Simba walipigwa 3 kwa sufuri na Raja Casablanca kwa Mkapa mbele ya wachawi wao wote.
 
Mashujaa sio wachawi kilichofanyika ni mind game
Na hii ilifanikiwa nadhani mlioma tarik alivyopaniki mpaka akatoka kabisa mchezoni
 
Uchawi ni imani inayotupuleka puta.. kwa huo uchawi wao wabebe ligi kuu kisha mashindano ya caf.
 
Kwa Ujumla jibu ni HAPANA.

Namna ya ushangiliaji wa Mashujaa FC umekua ukihusishwa na imani za uchawi jambo ambalo kiuhalisia siyo kweli bali ni namna ya kujitofautisha na ushangiliaji wa Mashabiki wa timu nyingine.

Tuanzie kwenye logo ya Mashujaa FC ukiiangalia ni logo inayotambulisha Mnyamapoli ambaye ni wa asili, Hapo kwenye "ASILI" ndipo na ushangiliaji wa mashujaa FC ulipoanzia na hatimaye Mashabiki wa mashujaa kuja na ushangiliaji wao wa kipekee ukiwahusisha watu waliobeba zana za jadi na kuvalia kijadi au kiasili.

Namna ya uvaaji wa nguo hiyo nyekundu inaitwa "Lubega" kwa Kiha. Hiyo ndiyo namna ya asili ya uvaaji ya watu wa kigoma "Waha" kama ilivyo kwa wamasai.

Chungu na mapambo yake ikiwemo kioo ni namna ya kunogesha tu mwonekano na wala siyo kwamba kimebeba uchawi ndani yake.

View attachment 2671458
Uchawi kigoma ni wakuuliza? Watu wamekuja uwanjani na mafuvu ya binadamu, kwato za jogoo, na macho yà paka
 
Uchawi kigoma ni wakuuliza? Watu wamekuja uwanjani na mafuvu ya binadamu, kwato za jogoo, na macho yà paka

Ukibeba hivyo tayari wewe ni mchawi? Mnachotwa akili kiboya sana
 
Zote ni Imani...; Wanaokwenda Makanisani, Mahekaruni, Misikitini au kina John Terry Kuvaa Shin Guard hio hio kila Mechi akiamini ina bahati au Lauren kuweka sarafu kwenye soksi...

To each his / her own..., So long as imani zao haziumizi watu au kuchukua damu za watu; waache wafanye kile kinachowapa confidence.....
 
Back
Top Bottom