Mleta mada nakusifu kwa kuandika makala hii ndefu..
Mimi pia ni mtaalamu wa Nutrition lakini kiukweli ni mvivu kuandika..
Pengine yawezakuwa umetafsiri vibaya watu wanaposema dona ni nzuri kuliko sembe...
Sidhani hoja ya watu wengi wanaoshauri husimamia kwenye nguvu....
Mmi napenda Dona si kwasababu ya Nguvu bali katika kufanya diet. Kama ulivypeleza kuwa Dona in fibres nyingi, hivyo kusababisha kukaa tumboni mda mrefu na kuhisi umeshiba (satiety) hii inasaidia kutokutamani tena kula na hivyo mwili kuunguza mafuta yaliyohifadhiwa mbilini huku mmeng'enyo wa dona ukienda taratibu....
Sbembe huchakatwa haraka sana na hivyo kuzalisha glucose nyingi. Kuwa na glucose nyingi mwilini pasipo matumizi hasa kwa sisi tunaoishi mjini, (life style) ni sehem ya kuongeza uzito kwenye mwili na kunenepeana hovyoo...
Hivyo tukiachana na suala la virutubisho, bado dona ni bora kuliko sembe hasa katika kuzuia magonjwa ya moyo na obesity