Je, ni kweli watu wote wanakula kwa jasho? Jinsi watu wasiofanya kazi walivyotokea duniani

Je, ni kweli watu wote wanakula kwa jasho? Jinsi watu wasiofanya kazi walivyotokea duniani

Apollo one spaceship

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2021
Posts
245
Reaction score
457
Wamepora mifumo na bidhaa ambazo zilipaswa kusaidia jamii nzima.

Wanatamani hata hewa waiwekee haki miliki ili tuwe tunainunua. Makampuni yangefyonza gesi yote ya oksejeni angani na kuimiliki. Watu wasiojiweza wangekufa kwa kukosa pesa ya kununua Oksijeni.

Kwenye mambo mengi wameshinda kwa kishindo. Bidhaa huzalishwa kwa kutumia malighafi na wafanyakazi. Wao wamevipa jina la "bidhaa" vitu ambavyo havijazalishwa. Wanakula donge nono bila kufanya kazi. Maskini ndio wahenyeka. Wengine ni wauza papuchi ilhali hawaizalishi.


Kitu chochote ambacho kinauzwa bila kuzalishwa au kufanyiwa ukarabati ni bidhaa batili kwa sababu hutengeneza kundi la watu wasiofanya kazi.

Mungu alisema mwanaume atakula kwa jasho. Shetani alivyo mjanja kuna watu amewatolea hilo jasho na kuwastarehesha
 
Back
Top Bottom